GNLD products zinasaidia mtu mwenye shida ya kupata mimba? Ushauri tafadhali

Truly

JF-Expert Member
Jan 27, 2011
228
32
Wana JF heshima mbele.

Nina rafiki yangu ana 33 years. Ni miaka miwili na nusu toka aolewe. Alipata mimba lakini ilitoka ikiwa na miezi 3. Toka hapo hajafanikiwa kupata mimba nyingine. Alishaenda kwa daktari akapewa clomid kwa miezi mitano lakini hakushika mimba.

Shangazi yake akamwambia kuna bibi mmoja anatoa dawa za asili. Wakaenda akapewa dawa ya kuweka kwenye uji halafu aweke na asali. Bishost akanywa kwa siku 7 after memstrual period. Toka anywe hiyo dawa ni miezi miwili na nusu hajapata period.Kapima mimba kwa home pregnancy test mara 4 zote ni negative.Ameboreka period zimepotea na mimba hana.kuna mtu kamwambia atumie GNLD products.

Kaniomba ushauri je, atumie hizo products. Mimi sina uzoefu na hizo products mwenye uzoefu nazo naomba anijuze kabla bishost hajaingia gharama ya laki mbili kununua.Kaandikiwa products aina ne bei yake laki 2 kaambiwa zitamsaidia na atashika mimba.

Ya kweli hayo isijekuwa anaibiwa buree.
 
Back
Top Bottom