Mkuu umeme wa elf 2 kwa nyumba milion 1 ni shngap kwa mweziKwanza sidhani kama REA inalipa...bush kule umeme wa elfu mbili (2000) mwezi mzima..
Hii ndio ile roho ya KWANINI?
Mkuu umeme wa elf 2 kwa nyumba milion 1 ni shngap kwa mweziKwanza sidhani kama REA inalipa...bush kule umeme wa elfu mbili (2000) mwezi mzima..
Hii ndio ile roho ya KWANINI?
Mimi nilishangaa sana. Manguzo yale ya miti hata hawa wauza mbao waliojijenga na uzoefu wa muda mrefu si wanaweza. Hata wakijenga mitambo ya kuchemsha nguzo za miti na kutia dawa, kutengeneza za simenti na za vyuma sitarajii ivuke bilioni 10 na hapo wakizalisha nyingi.Bilioni 30 kilikuwa kiwanda Cha kutengeneza nuklia? Hicho kiwanda ni very simple na gharama nafuu sana hata 1 bilioni hakifiki.
Politiki kitu Mbaya sanaNipo kwenye rekodi hapa ya kumtetea waziri Kalemani huko nyuma lakini leo naomba Rais Samia amfukuze tena ikibidi haraka Sana huyu waziri.
Kwa mujibu wa maagizo aliyowapa Tanesco waziri Kalemani anataka sasa karibu watu wote Tanzania nzima wakitaka kuunganishiwa Umeme walipe Elfu 27 tu bila kujali gharama halisi za kuvuta umeme kwa mtu huyo anasema Serikali imepitisha hela ya ruzuku kwa Tanesco.
Sasa hebu twende taratibu huku tunatumia akili kidogo. Mtu anajenga ghorofa lenye apartments 20. Mfano Masaki huyu mtu sio masikini why asigharamie gharama halisi?
Why Tanesco ijinyime mapato Kwa kutoa ruzuku hadi Kwa matajiri wa Masaki Hadi Upanga?
Anaejenga Fremu 20 Mbeya mjini au Dodoma mjini? Why alipe elfu 27 wakati Tanesco wananunua hizo Mita moja laki moja 20?
Kwanza hii tafsiri yake ya Mjini kuwa ni Ilala City Center kaitoa wapi?
Anajua maana ya Urban and Rural? Anajua history ya kuanzisha REA?
Why anakuja kuleta siasa za kutafuta umaarufu Kwa nguvu Kwa gharama za kuiua Tanesco??..kama mpaka sasa Tanesco haipati Faida inaishi kwa ruzuku. Why anakuja na maamuzi ya kupunguza mapato kwa Tanesco?
Mapato ya service charge yamefutwa. Mapato ya kulipisha fomu yamefutwa. Sasa hata gharama za kuvuta Umeme iwe Upanga au Masaki ziwe za REA kweli?
Huyu waziri anafanya siasa za hatari za kujifanya 'mtetezi wa wanyonge aliebaki'. Itasababisha Tanesco huko mbeleni ishindwe kujiendesha wala kulipisha wateja wake gharama halisi za Umeme.
Anataka aonekane yeye alipokuwepo gharama zilishuka wakati si kweli.
Gharama zipo zile zile anachofanya ni kutumia ruzuku ya serikali ambayo sio ya uhakika na haina guarantee ya kuwepo kila mwaka.
Tayari foleni ya umeme unaohitaji nguzo Tanesco inafika miezi sita sasa na bado waziri anaongeza tatizo badala ya kupunguza.
Utaratibu wa REA ulikuwepo kabla ya hata Kalemani hajawa waziri. REA ibaki REA kwa wananchi wa vijijini na wenye vipaji vya chini.
Kulazimisha REA itumike nchi nzima ni siasa za kufeli na kuja kulaumiana huko mbele wakati huduma itakapokuwa ngumu kupatikana baada ya mapato kushuka REA hadi Masaki na Sinza?
Wenye Bar na mafremu 40?
Wenye ghorofa zenye apartment 40?
Hi ruzuku ni pesa ambayo wananchi hasa masikini wanachangia. Why itumike kufaidisha hadi matajiri kwa siasa tu?
Viongozi wa Tanesco kuanzia Bodi hadi CEO wake wote wapigwe chini kwa kukubali maagizo haya ya huyu waziri...
Watu wenye uwezo walipie gharama halisi za umeme.
REA ibaki vijijini na kwa watu masikini.
27,000 Bado ni nyingi,ilitakiwa umeme ufungwe Bure kabisaaaa.Kwa hapo itakuwa kakosea,
Kwa wa mijini labda angepunguza kutoka Tsh. 321000 hadi 121000/=
27,000 Bado ni nyingi,ilitakiwa umeme ufungwe Bure kabisaaaa.
Tanesco makao makuu watabishaWameanza vizuri laki 5 na 20 ilikuwa pasua kichwa ila 27,000/= sio mbaya!! wananchi wengi watafunga umeme ,wengi walikuwa wanashindwa kuunganisha umeme gharama zilikuwa kubwa sana,kwa hili TANESCO wataongeza mapato sana maana wataongeza watumiaji wa umeme.
Tanesco makao makuu watabisha
1. Gharama za elfu 27 ni kwa wale wa single phase tu.Na sasa anataka mtu hata aliejenga fremu 40 za biashara nae alipe elfu 27.
Au ghorofa Upanga la apartment 40 alipe elfu 27.. imagine that
Haya maelezo (namba 2) umeyatoa wap? Waziri kasema sehemu zote kasoro ilala ambako hata hawahitaji kwa sasa1. Gharama za elfu 27 ni kwa wale wa single phase tu.
2. Gharama hizo haziwahusu watu wa Dar es salaam, wao watalipa gharama za kawaida.
3. Nia ni kuhakikisha umeme unafika nchi nzima. Ili nia hiyo itimie ni vyema kupunguza gharama za kuunganisha umeme.
4. Umeme kwa sasa unazalishwa mwingi. Hakuna haja kuwa na umeme unaobaki bila matumizi wakati unaweza kuwaunganishia watu na wakalipa bill/luku shirika likapata mapato.
5. Kwa mujibu wa taarifa ya Waziri Kalemani bungeni ya bajeti ya wizara yake, alisema Tanescoa imeacha kutegemea ruzuku ya serikali kuu tangu mwaka huu wa fedha kuanza. Kwahiyo, Tanesco inajitegemea siku hizi.
2. Gharama hizo haziwahusu watu wa Dar es salaam, wao watalipa gharama za kawaida.