Gharama za trekta mpya

Fredrik

Member
May 22, 2013
7
0
Habari zenu jf members, naomba mnijuze ni gharama kiasi gani inahitajika nikihitaji trekta mpya?Kwa anaefahamu vizuri
 
Mkuu!!

Weka details zaidi za ombi lako kama Aina ya trector, HP ngapi? Wapi Utaitumia ( Kuzingatia udongo wa sehemu hiyo - Trector ya kulima Kibaigwa ni tofauti na ya kulima mashamba ya Mpunga Ifakara), unataka Trector Used au Mpya, unaweza kuagiza used kutoka UK (Farm Condition then baada ya kuifikisha TZ ukaifanyia Cosmetics unazotaka wewee, lakini kwa ushauri wangu, ningekushauri nenda / nunua MF, John Deer, Ford, International. Hizi mkuu spare parts availability zipo kibao. Ila wengine watakuja na mawazo zaidi.
 
sijui kwa nini watu wakitaka ushauri juu ya ununuzi wa trekta wanakuwa too general.hilo Ombi lako ni kama mtu anayeomba ushauri juu ya kununua gari bila kutoa aina ya gari.funguka zaidi upate ushauri unaokufaa.Pia kuna Uzi upo jukwaani humu unahusika na swali lako hilo utafute.Una majibu mengi mazuri.by the way andaa not less than 25m for a good,reliable tractor
 
TRECTA NZURI LINATEGEMEA NA MAHITAJI YAKO Eg. FORD 5600,5610,6600,6610 NI MAZURI SANA KWA KILA ARDHI IWE MBUGA , KICHANGA AU UDONGO MFINYAZI WEWE UTALIMA. MASSEY FERGUSION 240 NE MODEL (135 OLD MODEL ), NI NZURI SANA KWA UTUMIAJI WA MAFUTA NA KUWA NA SPEEDI SHAMBANI LAKINI HAINA UWEZO MKUBWA KWENYE MAENEO YA MBUGANI INAHITAJI ARDDHI NYEKUNDU AU KICHANGA HUWEZI PASUA MBUGA NA MF 240. MF 160,165,170,175,178 NI NZURI PIYA HAYA MENGI NI USED KWA HAPA KWETU TANZANIA YANA RANGE 18MILIONI HADI 25MILIONI YAPO KIGOGO ROUND ABOUT, KARIAKOO MTAA LIVINGISTONE.SIKUSIKU, MAGOMENI. AINA NYINGINE NI JOHN DEER YANAPATIAKANA MIKOCHENI NDIPO OFISI ZAO ZILIPO, SWALAJI 744 NA 844 NI NZURI SANA KWA ULAJI WA MAFUTA NA SPEED SHAMBANI BEI 29MILIONI WAPO KIJITONYAMA MAKUMBUSHO KAMA UNATOKA MJINI KUSHOTO. AINA NNYINGINE NI FARM TRACT 60, 70 BEI ZAKE 19MILIONI NA 28MILIONI WAUZAJI SUMA JKT KWA MKOPO PIYA UNAPATA, WAUZAJI WENGINE WAPO NYERERE ROAD.
 
Back
Top Bottom