Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Maisha ya vijana wa siku hizi yamebadilika sana linapokuja swala la kutafuta mwenza, tofauti na miaka ya zamani. Siku hizi vijana wengi hutumia mitoko kama njia ya kutafuta mwenza kwani kwa kuwa na mtoko na mwanamke aliyevutiwa naye humpa fursa ya kujuana na mwanamke huyo ili kupata fursa ya ya kufanya maamuzi sahihi.
Mtoko *(date) ni ghali sana, na kwa bahati mbaya gharama za mitoko mara nyingi zinakuwa hazipangwi bali hutokea tu, kulingana na makubaliano wa wawili wapendanao, na gharama hizi huwaweka wahusika katika wakati mgumu na pengine kuwaingiza katika madeni.
Ipo dhana imejengeka kwamba wanaume ndio huumia zaidi kwa gharama za mitoko kutokana na kwamba imezoeleka kuwa wao ndio wanaopanga mitoko hiyo, hivyo wao ndio hubeba gharama hizo za mitoko. Tumeshuhudia hata hapa JF katika jukwaa hili la MMU, kuwaona wadada wakishupalia kwamba hawapaswi kulipa chochote wakati wa mtoko kwa sababu wao ndio wamealikwa.
Lakini jambo ambalo wengi hawalijui hususan wanaume ni kwamba, wanawake hubeba gharama kubwa kwa ajili ya mitoko. Unaweza kujiuliza kwamba gharama hizo ni zipi?
Ni swali zuri, lakini kabla sijajibu swali labda nikuulize swali moja. Hivi unajua ni kiasi gani wanawake hujiuliza kwamba ni kivazi gani watupie wakati wa mtoko?
Kwa taarifa yenu, wanawake huwa wanafanya maandalizi makubwa sana kabla ya mtoko na maandalizi hayo yanaanzia kwa kununua kivazi kipya (hii hutokeas sana), kutengezeza nywele , kutengezeza kucha na mambo ya vipodozi na vikorokoro vingine kabla ya kwenda kwenye mtoko. Mwanamke huweza kubeba gharama hizi kwa mtoko wa kwanza, wa pili na watatu… na hiyo itategemea viwanja anavyokutania na mwenzi wake.
Swali ambalo ninataka tulijadili hapa ni Je, ni nani huwa anaumia kwa gharama za mitoko kati ya mwanamke na mwanaume?
Naomba mtiririke hapa maana kesho na mie nina Ki-Date……….LOL