Gharama za matibabu ya wafanyakazi wa ndani wauguapo ni jukumu la nani?

Huduma za afya zina gharama na hii ndiyo sababu watu wengi wanaishi kwa kudra za Mwenyezi Mungu. Wengine wanakwenda kupiga ramli kwa kuanguka na kuzimia bila kujua kuwa hii ni dalili ya hatari na inahitaji uchunguzi wa kitaalamu. Wengi huponea hutoa sadaka kanisani ili waombewe. Kuna wanaokwenda kwa Mwamposa kisa wanaharisha. Hili si kusudio la mada.

Nia yangu ni kuongelea matibabu ya hawa wanaotusaidia kazi za ndani. Kuna wanao ambiwa wajinunulie Bima ya Afya kutoka kwenye mishahara wao. Wengine wanaunganishwa kwenye bima ya familia (Hawa ni wachache sana).

Kuna mama mmoja alimtoa binti wa kazi Dodoma, binti alikua mdogo kama miaka 16. Wazazi wake walimtoa kutokana na ugumu wa maisha wakitegema kurushiwa hata 20,000 kutoka katika mshahara wake kila mwezi.

Yule mtoto alikuwa mgonjwa, alianguka mara nyingi baada ya kuamka asubuhi. Yule mama alimpeleka hospitali. Vipimo vya siku ile vilimgharimu laki tatu na mtoto aligundulika na matatizo ya moyo.

Yule mama alilaani sana kutumia laki tatu hospitali. Alimsimanga binti kuwa kama ulijua ni mgonjwa kwanini ulikubali kuja kwangu. Baada ya pale alimrudisha kwao. Ukizingatia hali za maisha ya wazazi wa binti Yule ni wazi kuwa hawataweza kumtibu mtoto wao.

Tunapotoa ajira kwa hawa ndugu zetu wanaotusaidia majukumu ya kulea watoto na wazazi wetu, tukumbuke pia kuwa wao ni binadamu na kuwe na utaratibu wa kuwasaidia katika matibabu. Mnaweza kushauriana nae apate Bima yake ya Afya.
Ndio maana wanaamua kwenda uarabuni tu.
 
Wa kwangu alikuja mjamzito hakuniambia na hatukumstukia. Baada ya miezi miwili kabanwa na tumbo ghafla usiku nikamkimbiza rabinisia nikijua ni tumbo tu la kawaida food poisoning. Kumbe ni uchungu wa kujifungua, kajifungua hapo maana kulikuwa hakuna muda wa kumuhamisha hospitali. Mbaya zaidi alilazwa pale siku kadhaa bili ilipoletwa nilichanganyikiwa akili iliniruka sitakaa nisahau kamwe. Niliapa sitokuja kuwa na msichana wa kazi daima
Dah polee. Ikawaje? Ulimrudisha kwao? Au ndugu zake uliwapata wamchukue?
 
Aisee!

Bora wanaojiongeza wanaenda huko uarabuni, watatumwa tumwa sana lakini wanaondoka na vilaki kadhaa kwa mwezi.

Akikaa mwaka au miaka anarudi na mtaji, kuliko huu utumwa wanaofanyiwa na wanawake wenzao wa bongo.

Hapa huwezi kuwaskia ma feminist uchwara wa bongo, wakiongelea haki za wadada wa kazi.
Basi mlipe laki mbili maana najua unaielewa elfu hamsini kwa mwezi mzima na bado atume kwao na ajinunulie hata brazzier, underwear nk.

Kimsingi ukitaka ajitegemee mpe laki tatu ya serikali kima Cha chini itakuwa sawa Ila unapompa 50,000 jamani dah nyie watu aisee.

Imagine anaumwa malaria, anachukua pikipiki kwenda dispensary na kurudi let's say elfu nne, kupima malaria 3000, dawa anabaki na nini?

Najua huwezi kutimiza mahitaji ya mtu mzima lakini umlipe mtu na umpatie marupurupu ambayo yapo equitable na kazi anayofanya.

Dada anaamka saa 11 wengine 10 alfajiri, aandae watoto, apige pasi nguo zote , ahakikishe wamekunywa chai kabla basi la shule halijapita, awasindikize watoto kwenye school bus, arudi aandae chai yenu, bado hajatumwa vocha dukani, Mara nguo hutaki kuivaa akupasie nyingine, yani mpaka mnaondoka ameshachoka hapo ndio anaanza kufanya usafi, afue apike, Yani dah tuwe wanadamu wewe kumtibia tu? Only that???? Tena sio anaumwa kila siku
 
Wa kwangu alikuja mjamzito hakuniambia na hatukumstukia. Baada ya miezi miwili kabanwa na tumbo ghafla usiku nikamkimbiza rabinisia nikijua ni tumbo tu la kawaida food poisoning. Kumbe ni uchungu wa kujifungua, kajifungua hapo maana kulikuwa hakuna muda wa kumuhamisha hospitali. Mbaya zaidi alilazwa pale siku kadhaa bili ilipoletwa nilichanganyikiwa akili iliniruka sitakaa nisahau kamwe. Niliapa sitokuja kuwa na msichana wa kazi daima
Polee sanaa …. Lakini hiii inaonyesha jinsi gani hatuko karibu kuwafuatilia hawa wanaotusaidia kazi maana kwa miezi miwili ni mingi kujua kama binti ni mja mzito.
 
Polee sanaa …. Lakini hiii inaonyesha jinsi gani hatuko karibu kuwafuatilia hawa wanaotusaidia kazi maana kwa miezi miwili ni mingi kujua kama binti ni mja mzito.
Sasa unamfatiliaje kwa mfano? Ulitaka nimuulize kama anaingia kwenye siku zake kila mwezi? Nimkague tumbo?
 
Back
Top Bottom