Gharama za matibabu katika hospitali zetu: Napendekeza tuangalie kwa macho yote

Chendembe

JF-Expert Member
Oct 20, 2019
416
462
Wadau, nimekuwa mhanga wa gharama za matibabu hali iliyonisukuma kuandika mada hii.

Aidha, nimeguswa kwa masikitiko kauli mbalimbali za viongozi wetu katika suhala la afya nchini.

Nategemea na ukoo wangu, ivyo, sinashaka mnafahamu ninavyosumbuka. Hali hii inanifanya kuwaza kipi bora kufanywa na Serikali kwa Sasa; Kuendelea kujenga majengo au kuongeza upatikanaji wa dawa au kutoa ruzuku kwa sekta ya afya ili gharama zishuke?

Jamani, hali ni mbaya, watu wanashindwa kumudu gharama za afya na kupelekea watu kununuwa vijidawa bila vipimo au kutibiwa kienyeji na wengine kufia majumbani.

Tumezika Jana dada yetu ambaye alilazwa hospitali Fulani na baada ya kuzidiwa, akapewa rufaaa kwenda Mhimbili, kilichotokea ni uzuni, mume alilia Kama amechomwa moto na kulazimisha mgonjwa apewe ruhusa arudishwe nyumbani. Dokta alimruhusu na kafa nyumbani. Tulipomuuliza shemu, alijibu heri nimzike mwenyewe kuliko Jiji.

Nashauri tozo zielekezwe katika ruzuku ya matibabu na ziada tu ndo iangalie ujenzi mpyaa.

Pia, ruzuku isaidie kushusha gharama za kukata bima ya afya kwa wananchi.

Zaidi, nashauri kuundwa kwa mamlaka ya kudhibiti gharama za matibabu nchini.

Nawasilisha
 
Pole sana mkuu, atleast serikali ihakikishe wananchi wake wana bima ya afya kupata basic health care na referrals services
Sema sasa health industry ni “biashara”
 
Kinachosikitisha ni kuwa, pamoja na gharama kuwa juu huduma ni mbovu. You don’t get value for your money.
kuna hizi bima wamezibatiza timiza, wekeza na najali afya.

hata kama una hizi bima lkn service nyingi haziko covered na hizi hivyo inabidi ulipie cash.
 
Pole sana mkuu, atleast serikali ihakikishe wananchi wake wana bima ya afya kupata basic health care na referrals services
Sema sasa health industry ni “biashara”
Biashara yeyote ili ifanikiwe inahitaji kuendeshwa kwa ufanisi na wateja waridhike nayo. America unalipia huduma ya afya lakini unapata tiba bila usumbufu.
 
Serikali inaamini ikishaweka majengo kazi imeisha wakati walitakiwa wawekeze kwenye kuzalisha wataalamu wengi, manesi, madaktari, matabibu, maabara na famasia lakini pia wawaajiri ikienda sambamba na kununua vifaa tiba vyenye ufanisi na vya kisasa, na kuhakikisha upatikanaji wa madawa unakua vizuri wakati wote walau kwa vituo vya afya, zahanati, hosptali za wilaya, mikoa na za rufaa ikiwemo zile za kanda
 
Lakini pia maslahi ya wauguzi na madaktari maana Botswana daktari analipwa mara tatu hadi nne ya daktari wa Tanzania, yaani atawezaje kujisumbua kumtibu mgonjwa wakati bado anastress, akigeuka hivi vifaa tiba hakuna
 
Wao wana access ya kwenda India kupata huduma za afya daraja la mwanza hadi daraja la pili kwa level ya kidunia, ndio maana wala hawajali kabisa
 
Back
Top Bottom