Gharama za matengenezo ya Nyerere Road zimehalalishwaje?

MpendaTz

JF-Expert Member
May 15, 2009
2,184
879
Hivi karibuni niliona sehemu ya barabara ya pugu ikiwa inafanyiwa marekebisho ambayo yanatokana na kutuama kwa maji maeneo ya karibu na Q/plaza.

Nasikia hata misafara ya wakubwa iliwahi kutaka kukwama pale.

Lakini maamuzi ya matumizi makubwa namna hii ya fedha za umma yanatakiwa yawe yanazingatia utaalamu zaidi.

Ile barabara haikuwa na hilo tatizo kwa miaka mingi tu baada ya kujengwa na ikitumika bila shida wakati ile mikondo ya maji ilipokuwa wazi. Nadhani kilichotokea ni kwamba wameuziwa watu viwanja kwenye ile mikondo wakaijaza na kujenga majumba ya biashara na kusababisha maji kukosa pa kutokea.

Lakini serikali badala ya kuliangalia kwa busara zaidi na kitaalam, haraka ikaanza kuwaza ni nani apewe hiyo tenda.

Maamuzi kama haya huchangia sana kudhoofisha uchumi wa nchi changa.

Naomba tutafakari.
 
Ndugu Yangu Najua Umetoa Mfano wa eneo Hilo kwa sababu Unajua Huenda Watu wenye Uchungu na Nchi Hii wanapita!!

Kumbe Mawazo yako yanaweza kuwa Ndio au Sio!!

Kwa Taarifa, wenye Uchungu na Nchi hii walikufa na Nyerere!! Hili tatizo limeenea Kila kona ya Nchi Hii, ila hali ni Mbaya kwa Maeneo ambayo Ujenzi wenyewe unafadhiliwa na Hela za Ndani!! Kwani Utaona Mambo Mengi Yanafanywa Kwa Hisia Bila Kushirikisha Utaalamu Ili Mkandarasi Husika aweze kupata Faida Kubwa!!

Ni wazi ijulikane kuwa 'Hakuna mkandarasi anayeweza kufanya kazi nzuri bila kuwa na Michoro na Standard ya kile anachokifanya!'

Mifano ya Kazi za aina hii na ambazo serekali imepata Hasara Kubwa ni:

1. Barabara ya Kigogo first Inn - Mwembechai!! (Hii barabara ndio inakaribia Kukamilika ila kwa Nyuma maeneo ya Mianzini Ina Mashimo Mengi) Je kwa hali hii watanzania tumelaaniwa na Hatuna uchungu na Kodi Zetu?

2. Barabara ya Shekilango - very poor construction Without Design!!

3. Barabara ya Mwika sinza makaburini kuja Sam Nujoma - Very Poor quality of Construction na imeshaanza kuharibika

4. Barabara Uwanja wa ndege Kuelekea Kisarawe!! - Very poor quality
 
Umezidi kunitesa kimawazo. Sasa ina maana japo ni barabara yao haswa wenye kupenda safari za nje kila leo wameshindwa kabisa kutafakari linalotokea? Sababu gani zimewafanya wakagombea uongozi wa hii nchi?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom