Gharama za Kuendesha Barbershop Business

hekimatele

JF-Expert Member
May 31, 2011
9,884
2,781
Msaada wadau, kuna mtu yeyote mwenye experience na biashara ya Barbershop hapa mjini anieleze gharama halisi ya ku set up a modern barbershop kwa sasa inaweza kugharimu kiasi gani na estimated revenue per chair inaweza kuwa kiasi gani kwa wiki. Ahsanteni sana kwa ushauri wenu maridhawa.
Wasalaaaaam
 
Mi nna ki-barbershop changu pale Dodoma, gharama za kufungua mpaka ianze kazi zinatofautiana kutokana na Mwenyewe unataka iwe classic kiasi gani. Kwa mfano viti vipo vya kuanzia 350,000 mpaka vya 1,400,000 so ni wewe tu na mfuko wako. Mapato ya wiki inategemea na kinyozi wako ni Mkali kiasi gani na location ya barbershoo yako. Kuhusu namna ya kuendesha ilk usipate usumbufu wala kuibiwa Mimi niliamua kumkabidhi kinyozi kila kitu mi nnalipia kodi ya fremu tu, mafuta, dawa, umeme, maji na posho ya msaidizi wa kinyozi ni juu yake ilimradi tumewekeana kiasi anachotakiwa kunipa mwisho wa wiki anantumia kwa M-Pesa. Kwahiyo ukipata kinyozi asiyehitaji kusimamiwa unafanya na mambo mengine ya maendeleo, kwa mfano mi nipo Chuo Moro saluni ipo Dodoma na nnaweza nsifike hata mwezi ila mambo yanenda
 
Inategemeana na mfuko wa hela yako ulivyo na sehemu unayotaka kufungua hiyo barbershop yako, uwe na fedha za kukodi flemu, kwa kukisia flemu haizidi 200,000/=, vifaa mara nyingi huanzia shs 150,000/= na vifaa vingine vinazidi 1,500,000/= sasa inategemea kapu la mfuko wako ulivyo,
Iinaitajika uwe na kinyozi mwenye ujuzi wa kutosha na stadi wa kazi, na uwe na mdada wa kufanya massage kwa wateja wataoingia katika hiyo barbershop yako, kwani itavuta wateja wengi kuja hapo na kupata income unayotaka. kama utakuwa na uwezo wa vitu vyote hapo basi unaweza anzisha hiyo barbershop yako
 
Back
Top Bottom