NgimbaErick
Member
- Mar 31, 2020
- 85
- 131
Naomba kwanza niliweke wazi jambo hili kwamba … Kama kweli upo serious na Biashara yako, basi mambo yafuatayo hutoyaona kama ni Gharama bali ni Uwekezaji.
Sasa ntajaribu kuelekeza kwa ufupi kulingana na uzoefu wangu. Maana kwenye hili suala la gharama za website kuna mambo mengi mno, so sitoweza kuelezea kiiila kitu.
Ntakwenda kuelezea mambo ambayo watu wengi wamekuwa wakiulizia kuhusu gharama za kuanzisha website.Pia Kama utakuwa na swal, basi utauliza hapo chini kama kawaida.
Nakala hii itakuwa na sehemu nne,
- Gharama za Website yenyewe kama yenyewe.
- Gharama za utengenezaji.
- Gharama za uendeshaji wa website.
- Hitimisho na Ushauri.
- GHARAMA ZA UTENGENEZAJI
- Hapa kuna vitu 3 muhimu;
- Domain.
- Hosting.
- Vifaa vya ziada vya kutengenezea website.
- DOMAIN
- Hii ni kama address ya website yako (mf; cocacola.com)
- Huwa zinatofautiana bei kulingana na aina ya extension(yani; .co.tz, .com, au .net n.k) unayotaka.
- Kwa wastani zinauzwa kuanzia Tsh. 15,000 mpak Tsh 30,000+ na unakuwa unailipia kila baada ya mwaka 1.
- Huuzwa na makampuni mengi tu ikiwemo; Namecheap, Godaddy, Google Domains, Dudumizi n.k,
- HOSTING
- Ni huduma inayohakisha website uloijenga inaonekana kwenye internet.
- Hizi pia hutofautiana kulingana na mahitaji yako pia na uwezo wako, kama unahitaji hosting nzuri zaidi yani, yenye kasi na usalama zaidi inamaana gharama zitakuwa tofauti na hosting zingine za kawaida.
- Kwa wastani zinagharimu kuanzia Tsh. 10,000 mpaka Tsh 200,000+ kwa mwezi. na unakuwa unailipia kila baada ya mwezi na kuendela.
- Hutolewa na makampuni mengi ikiwemo; Interserver, Dreamhost, Duhosting n.k,
- VIFAA VYA ZIADA
- Sasa kama vile unavyojenga nyumba, ukitaka nyumba yako iwe na utofauti zaid basi kuna gharama utaingia kuupata huo utofauti.
- Pia kwenye ujenzi wa website huwa kuna vifaa vya ziada unavyokuwa unavihitaji ili kuweka upekee na ubora zaidi kwenye website yako.
- Unaweza ukavipata bure au kwa fedha kiasi, vifaa hivi ni kama Website Builders, CDN, Design Tools, Plugins, Themes, Templates, n.k
- Gharama zake kwa wastani ni kuanzia, Tsh 0. mpaka Tsh. 300,000+ vingi huuzwa kwa mara moja tu.
- Ni hivi jinsi unavyohitaji kujenga website yako ndo unakuwa unajua kama utavihitaji au la … ila domain na hosting ni lazima.
2. GHARAMA ZA UTENGENEZAJI.
- Hapa kuna vitu viwili tofauti;
- Kuna Kutengeneza Mwenyewe
- Kuna Kutengenezewa na Mtu
- KUTENGENEZA MWENYEWE
- Kama Website yako Unatengeneza mwenyewe ina maana hamna gharama za kulipia, ila utakuwa unatumia muda wako tu.
- Kwahiyo hakuna Fedha za kulipia huduma ya utengenezaji wa website hapa.
- KUTENGENEZEWA NA MTU
- Kama unatengenezewa na mtu, inamaana lazima kuna Fedha itabidi umlipe kwa ajili ya huduma na kazi aliyoifanya.
- Pia hapa kwenye Kutengenezewa website na mtu, kuna vitu viwili:-
- Kutengenezewa Website kwa kutumia Template.
- Kutengenezewa Website ya Kipekee (Custom Website).
- KUTENGENEZEWA WEBSITE KWA KUTUMIA TEMPLATE
- Website Template inakuwa ni Website ambayo imeshatengenezwa na mtu flani kwa ajili ya watu wote wanaohitaji kutengeneza website kwa hiyo unakuwa unaichukua kwa hiyo website ambayo tayari imetengenezwa kisha unaanza kubadilisha vitu kulingana na mahitaji yako, vitu kama picha, maneno, rangi na mwandiko.
- Naelewa inachanganya kidogo lakini ndivyo ilvyo hapo, kuwa mtu unayempa kazi hatengenezi website yote anachukua website iliyo tengenezwa tayari na mtu mwingine alafu anabadili badili vitu.
- Ukweli ni kuwa si rahisi mtu kukuambia kuwa atatengeneza website yako kwa kutumia template ila nlichokiona wengi wanaofanya hivi hutoza Tsh. 100,000 mpaka Tsh. 400,000 kwa website moja na hutumia siku 3 mpaka 7 kukamilisha kazi, kwasababu hamna kazi kubwa hapo zaidi ya kubadili badili vitu.
- Unachopaswa kujua kuwa kuna Faida na Hasara za kutengenezewa kwa Tempalate;
- FAIDA
- Gharama ndogo
- Inachukua muda mchache
- HASARA
- Huna Control kubwa na Website yako
- Unaweza kukuta website yako inafanana na za watu wengi kwa muonekano hivyo kupunguza uaminifu kwa watumiaji ambao wameliona hilo.
- Inaweza kuharibu utendaji kazi wa website, kwa sababu unatumia mfumo wa mtu mwingine na sio mfumo wako binafsi.
- KUTENGENEZEWA WEBSITE YA KIPEKEE (CUSTOM WEBSITE)
- Nadhani kichwa kinajieleza vizuri “website ya kipekee” inamaana Muonekana na mfumo mzima wa website ni wako tu hakuna mwingine wa kufanana na wewe. Labda kama wamekuiga, na mpaka unafikia hatua ya kuigwa basi ujue we sio wa level hii tena.
- Hapa kila kitu kinatengenezwa kuanzia mwanzo kabisa yani from scratch.
- Kwa tanzania hapa website za kipekee, wastani watu hutoza Tsh 500,000 mpaka Tsh. 4,000,000+ kwa website 1. Gharama hutofautiana kulingana na mahitaji ya website.
- Pia website za namna hii, zina pande mbili;
- FAIDA
- Kuwa na muonekano wa peke yako utakaoifanya brand yako kuaminika zaidi.
- Una control kubwa na website yako, hivyo ni rahisi kuona mapungufu yanayoathiri performance na kuyabadili mara moja.
- Pia ni salama zaidi kwa sababu formula ya website ni ya kwako tu, so sio rahisi mtu kudukua.
- HASARA
- Gharama zaidi.
- Inachukua muda zaidi kutengeneza.
3. GHARAMA ZA UENDESHAJI WA WEBSITE
- Ukiachana na zile gharama za Domain, Hosting na Vifaa vingine vya kutengenezea Website, Usilolifahamu ni kuwa Website Baada ya Kutengenezwa inahitaji Uangalizi na Utunzaji la sivyo utakuwa ulifanya kazi bure.
- Unahitaji upate mtu atakayekuwa anaitunza kama unavyotunza bustani maua yasinyauke. Website nayo inahitaji matunzo na pia maboresho panapobidi ili kuongeza utendaji kazi wake.
- So, unajiuliza sasa ni matunzo gani hayo au uangalizi wa nini? Jibu ni kwamba kuna vitu vingi mno vinavyohitaji matunzo na uangalizi, kama ifuatavyo;-
- Security
- Unahitaji uwe unafanya security checks mara kwa mara ili kuepusha website yako kupotea kwenye internet pia kudukuliwa.
- Updates
- Internet na Tecnology inabadilika kila kukicha kwahiyo unahitaji kufanya upadates za vifaa unlivyotumia kwenye website ili kuepusha website kuvunjika.
- Backups
- Unahitaji kufanya Backups atleast kwa mwezi mara moja, incase website yako imevunjika au kupotea, basi utatumia backup files kuirudisha online, pasipo kuanza upya tena.
- Functionality
- Kuna wakati unaweza kukuta links, buttons, form au chochote kwenye website hakifanyi kazi sawa na mwanzo, so kuvigundua hivi itakuwa ngumu kama huna tabia ya kukagua mara kwa mara.
- Analytics
- Sio lazima lakini ni muhimu sana kujua idadi na taarifa za watu wanaotembelea website yako, ili kufahamu nini cha kufanya ili kufikia malengo yako.
- Performance
- Pia unahitaji kufanya ukaguzi na marekebisho ya kasi ya kufunguka kwa website, kwasababu website ikiwa nzito kufunguka inafanya watu kuacha kuitembelea.
- Sasa Gharama za kufanya hayo kama utakuwa umemkabidhi mtu unadhani itakuwa ni kiasi gani? Kwa Tanzania watu wengi hutoza kuanzia Tsh. 50,000 mpaka Tsh. 300,000 kwa mwezi, kulingana na aina ya website.
4. HITIMISHO + USHAURI
- Kama uko na Bajeti ndogo na unataka kitu kitakachofanya kazi, au pia project yako ni ndogo tu na sio ya muda mrefu, Basi sio Mbaya ukitumia Template kufanya iyo kazi.
- Lakini kama uko serious na Business yako na una malengo makubwa nayo, kumbuka unawekeza hapa … So, ni vema ukapata website ya kipekee (Custom Website).
Haya, Nashkuru sana kwa kuwa pamoja nami kwenye nakala hii, ila kama unaswali lolote, uliza tu ntakujibu kabisa.
Imeandaliwa na Erick Ngimba
email: hello@erickngimba.tech
web: www.erickngimba.tech