Gharama za Baraza la Kikwete -Tutafika ??

Chifu Ihunyo

Member
Jul 3, 2006
63
10
Jamani tutafika au wachambuzi mnasemaje ?

Gharama za Baraza la Kikwete
Fungu la mishahara yao lazidi la Mkapa
Magari ya mawaziri yagharimu bil. 6.4


Na Tamali Vullu, Dodoma


BARAZA la Mawaziri la sasa linalipwa mishahara ya sh 1,012,764,000 kwa mwaka ikilinganishwa na baraza lililopita ambalo lilikuwa likilipwa sh 777,492,000.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia, aliliambia Bunge jana kuwa katika baraza la sasa lenye mawaziri 30 wanalipwa mishahara ya sh 533,628,000; na naibu mawaziri 31 wanalipwa sh 479,136,000.

Ghasia alisema katika baraza lililopita lilikuwa likilipwa mishahara ya sh 499,284,000 kwa mawaziri; na naibu mawaziri 18 walilipwa sh 278,208,000 kwa mwaka.

Alisema gharama za ununuzi wa magari ya mawaziri 30 wa awamu ya nne ni sh bilioni 3.15 na naibu mawaziri 31 ni sh bilioni 3.255.

Baraza lililopita lilikuwa na mawaziri 28, gharama ya magari yao ilikuwa sh bilioni 2.94 na kwa naibu mawaziri ununuzi wa magari yao uligharimu sh bilioni 1.89.

“Gharama za mishahara katika Baraza la sasa ukilinganisha na Baraza lililopita zimepanda kwa asilimia 32.6,” alisema.

Waziri huyo alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Grace Kiwelu (CHADEMA), aliyetaka kujua kiasi cha fedha kinachotumika katika Baraza la Mawaziri kama mishahara; na gharama za ununuzi wa magari pamoja na kiasi kilichoongezeka kikilinganishwa na baraza lililopita.

Katika swali la nyongeza, Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), alihoji kama Ofisi ya Waziri Mkuu inaweza kufuta kauli yake kuwa gharama ni ndogo na haina madhara yoyote.

Akijibu hoja hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Juma Akukweti, alisema bado anasimamia kauli yake na kwamba kwa mazingira ya kazi ya sasa, inastahili kuwa hivyo.
 
Lakini wengi wanasema ndiye mkombozi wa Tanzania maana kaitwa Nabii nk .Sasa kwa namna hii kweli JK tutapiga hatua ?Au unawapa fadhila washikaji kwa kampeni ?
 
Maslahi aliyoweka mbele Kikwete ni ya marafiki zake, sio ya Watanzania kwa ujumla. Hata katika teuzi zake, anaangalia urafiki kwanza, taifa baadaye. Ndio maana hajazi nafasi kwa kuangalia Mtanzania anayefaa zaidi ni nani, bali rafiki ambaye bado hajapewa asante ni yupi.

Ili kukidhi gharama hizi kubwa za kuwanufaisha marafiki zake, imebidi kusitisha utekelezaji wa miradi muhimu kwa taifa kama ule wa ujenzi wa barabara toka Mtwara hadi Mwanza. Ilikuwa imepangiwa kukamilishwa mwaka huu, lakini JK ameiondoa kwenye bajeti.

Watanzania tumebebeshwa mzigo mkubwa wa mawaziri 60. Hata ungefukuza kazi arobaini kati yao wakabaki 20 tu, wangetosha na kazi zingefanyiaka hata vizuri zaidi. Ni mzigo wa bure, wa JK kupongeza wenzake tu.

Itabidi Watanzania wanaosafiri toka Dar kwenda Mwanza na Bukoba waendelee kuomba njia Kenya, na hata Uganda. Na miradi mingine kabambe iliyokuwa inapangwa, kama ujenzi wa daraja toka Kigamboni hadi Feri, ndio isahauliwe kabisa. Pesa zitaishia kwa wenziye JK. Nyie mlie tu.

Augustine Moshi
 
Hivi kuna mtu anaweza kusema kwa nini JK aliamua kuwa na utitiri wa mawaziri namna hii ? Alitaka ku achieve nini na hao mawaziri wote wanafanya kazi zipi ambazo zimeibadili TZ ambayo siku za JKN,AHM, na BM hazikuwepo ? Naomba mnisiadie hapa wachunguzi wa mambo
 
Ikumbukwe kwamba ziko gharama nyingi za mawaziri ambazo hazikutajwa bado. Bunge limeelezwa gharama za mishahara na magari tu. Ziko gharama za matibabu (na nasikia wana haki ya kutibiwa nje, kwa harama za walalahoi, kwani hospitali za wananchi haziwafai), gharama za malazi na marupurupu mengine mengi ya mawaziri.

Jibu la swali lako Chifu Ihunyo ni kama hivi: JK aliamua kuwa na utitiri wa mawaziri ili kuwapa marafiki wengi uwaziri. Si kweli kwamba program yake inahitaji mawaziri wengi. Program ipi?

Augustine Moshi
 
Haya maoni hapa chini niliyaposti kwenye sehemu ya Elimu ya ukumbi huu, lakini nimeona watu hawasomi huko. Jamani, yaani ni siasa tu basi? Nayaposti hapa kwa Chifu Ihuyo, huenda yakajadiliwa yanavyostahili.

Augustine Moshi
======================

Naona Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi ameshatoa bajeti ya wizara yake. Inapatikana hapa http://www.tanzania.go.tz/bspeech2006_07f.html

Itabidi tusubiri bajeti ya Wizara ya Sayansi na Elimu ya Juu (ipo tena kweli?) kabla hatujafahamu ni sehemu gani ya bajeti nzima ya serikali imeelekezwa kwenye Elimu.

Kwa sasa, inatosha kusema kwamba bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ya sh. 239, 650,710,900 (roughly shilingi 240 billion) ni 4.9%tu ya bajeti yote ya serikali ya Tanzania, ambayo ni shilingi trillion 4.85. Linganisha hii na bajeti ya Elimu ya Kenya ambayo kwa fedha zetu, ni shilingi trillion 1.485, na ni sawa na 27% ya bajeti yote ya serikali ya Kenya.

Itabidi tujadili hili jambo kwa undani. Haitoshi kusema tunakazania Elimu. We must put our money where our mouth is.

Augustine Moshi
 
A Moshi,

Mwalimu wetu wa mahesbu, naomba nitoe ka wazo ka kukusumbua kidogo.

Je unaweza ukatuwekea Jedwali likionyesha kila budget ya Wizara na %ge yake na mpaka sasa msimamo ukoje.
 
Ogah ameuliza:Je unaweza ukatuwekea Jedwali likionyesha kila budget ya Wizara na %ge yake na mpaka sasa msimamo ukoje.

Siwezi, kwani bado bajeti za wizara nyingi hazijatolewa bado. Ukiangalia kwenye national website yetu (www.tanzania.go.tz), utagundua kwamba hadi sasa bajeti speeches chache tu ndiyo zimeshatoka.

Kwenye ippmedia.com, inaashiria kwamba kwa sasa Bunge linajadili bajeti ya Wizara ya Sayansi na Elimu ya Juu, lakini hiyo speech bado kuwekwa kenye website yetu. Ikishawekwa, tutajumlisha fedha zake na zile za Mama Sitta ili tupate kujua kiasi gani hasa kitatumika kwenye Elimu.

Augustine Moshi
 
Bahati nzuri nasikia na yeye yuko Ujerumani anaangaliwa afya yake mkubwa huyu kweli iko kazi kubwa mno tungoje tuone kwa nini kaweka utitiri wa walaji wenzake
 
Haya Inflation ndio imeingia na habari za uhakika wengi wa mawaziri wetu hawana kazi za kufanya. Nchi yetu ilivyo na matatizo hatuoni aibu kuwa na wachache wanaolipwa kama wafalme kukidhi mahitaji yao.
 
Huyu mshukaji toka mwaka wa kwanza alishaprove failure ila bado akaendeleza mazingaraombwe yake kwa expense ya watanzania alivyoona hela hazitoshi akaabza kutembeza bakuli ndo mana akamfikia vasco
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom