Idimi
JF-Expert Member
- Mar 18, 2007
- 14,970
- 10,462
Mkuu, kama huna uhakika na kinachoongelewa sio lazima kuchangia mada. Nimekaa mikoa tofauti tofauti yenye mambo hayo. Radi za kishirikina zipo. Kama unaamini Mungu yupo, amini na kwamba ushirikina UPO. Kuna watu wanazuia mvua kunyesha mahali fulani, na hainyeshi. Uliza watu wa Kakonko ama Kibondo mkoani Kigoma. Hayan ni mambo ya kawaida sana kwao. Kwenye maeneo wanapofyatulia matofali, huwa wanazuia mvua isinyeshe iwapo matanuri hayajaiva ama iwapo matofali hayajakauka vizuri. Kama hujafanya utafiti USIBISHE bro.Hakuna radi huku, ni stori za kusogezea muda tu, na pengine wanaokuambia hivyo wana nia ya kukutapeli. Kimbilio pekee ni MUNGU, achana na ushirikina, utaabika duniani na mbinguni