Bill
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 8,277
- 8,492
Imeelezwa kuwa gharama za kuendesha kesi za kupinga matokeo ya uchaguzi ni Tshs Bilioni 2 kwa uchache na hizi gharama zinalipwa na waTZ waliodhulumiwa haki zao na watawala walioamua kujitangazia watu waliowataka.
Gharama hizi ni matokeo ya Katiba yetu mbovu, NEC isiyo huru, wasimamizi wa kura kwenye majimbo wasio huru.
Tumeanza kwa kulipa Pesa Bilioni 2 ikiwa ni gharama ya Katiba mbovu na NEC isiyo huru, kinachofuata waTZ watalipa DAMU YAO ikiwa ni matokeo ya watawala wetu kung'ang'ania katiba hii mbovu na NEC isiyo huru.
MABADILIKO YA KATIBA NI LAZIMA ILI KUEPUKA UMWAGAJI WA DAMU YA WATZ
Source - Tanzania Daima
Bilioni 2/- kutumika kesi za uchaguzi
na Irene Mark
ZAIDI ya sh bilioni 2.2 zitatumika kwa ajili ya kusikiliza kesi 43 za uchaguzi, kupinga matokeo ya ubunge katika vituo 11 vya Mahakama Kuu hapa nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Jaji Kiongozi Fakhih Jundu, alisema fedha hizo zinatakiwa kuifikia Mahakama kabla ya Februari mwakani wakati shughuli za mhimili huo zitakapoanza.
Alisema, kesi zilizofunguliwa hadi Desemba 10 mwaka huu zinalazimika kusikilizwa na kumalizika katika kipindi cha miaka miwili ambapo Mahakama Kuu itasikiliza kesi kwa mwaka mmoja na kutoa nafasi ya mwaka mwingine kwa ajili ya watakaokata rufaa kupinga hukumu zitakazotolewa.
Jaji Kiongozi huyo alibainisha kwamba kutokana na idadi ya Majaji waliopo, kila kesi inakadiriwa kusikilizwa ndani ya siku zisizopungua 45 huku ikikadiriwa kuwa na wastani wa mashahidi 15 kwa kila kesi.
"Inakisiwa kuwa kila kesi itasikilizwa kwa muda wa siku zisizopungua 45 vile vile wastani wa mashahidi 15 wanakadiriwa kuwepo kwenye kila kesi na ili haki iweze kutendeka, jaji hatasikiliza kesi katika kituo chake cha kazi hivyo tutalazimika kuwasafirisha majaji kutoka kituo kimoja kwenda kingine," alisema Jaji Kiongozi Jundu.
Katika ufafanuzi wa gharama za uendeshaji wa kesi hizo, Jaji huyo alisema kiasi cha sh 52,644,000 zitatumika kwa kila kesi hivyo kiasi cha sh 2,263,692,000 zitatumika kugharamia uendeshaji wa kesi zote 43 zinazopinga matokeo ya ubunge.
"…Hizi ni fedha nyingi na lazima serikali izitoe, tumeshaiandikia hazina itutafutie fedha hizi. Mahakama haina pesa, huu ni mzigo wa serikali lazima ibebe mzigo huu.
"Nasema lazima serikali izitoe kwa sababu ni matakwa ya demokrasia… na hizi ni gharama za demokrasia ni vizuri wote tufahamu hivyo," alisisitiza Jaji Kiongozi Jundu na kuongeza kwamba hiki ni kipindi cha likizo ya Mahakama hadi Februari mwakani tutakapoanza kazi.
Kadhalika, Jaji huyo alitoa rai kwa walalamikaji kujiandaa vema huku akiitaka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni mdau mkubwa kujiweka sawa ili kuziwezesha kesi hizi kufanyika bila vikwazo.
"Isije ikawa mtu kafungua kesi akiwa hajajiandaa ndiyo maana kwa kuzingatia gharama hizi ipo sheria inayomtaka mlalamikaji anayepinga matokeo kupeleka mahakamani kiasi cha sh milioni tano.
"Hizi ni kesi nzito lazima kujipanga mtu asiende kwa kujaribu kwa sababu mwisho wake matokeo yatakua mabaya kwa aliyefungua kesi itambidi kulipa faini… nawashauri kama mtu ameshindwa asubiri kipindi kijacho," alisisitiza Jaji huyo.
Aidha, alibainisha kuwa usikilizwaji wa kesi hizi utaathiri mwendelezo wa kesi nyingine kama za mauaji na nyinginezo hali inayoweza kusababisha malalamiko kutoka kwa wananchi wengine. Jaji Jundu aliitaja mikoa inayoongoza kwa wingi wa kesi hizo na idadi yake kwenye mabano kuwa ni Tabora (9), Dar es Salaam na Mwanza (7), Mtwara (5), Mbeya (4), Moshi (3), Dodoma, Iringa na Arusha (2) wakati Bukoba na Sumbawanga (1).
Gharama hizi ni matokeo ya Katiba yetu mbovu, NEC isiyo huru, wasimamizi wa kura kwenye majimbo wasio huru.
Tumeanza kwa kulipa Pesa Bilioni 2 ikiwa ni gharama ya Katiba mbovu na NEC isiyo huru, kinachofuata waTZ watalipa DAMU YAO ikiwa ni matokeo ya watawala wetu kung'ang'ania katiba hii mbovu na NEC isiyo huru.
MABADILIKO YA KATIBA NI LAZIMA ILI KUEPUKA UMWAGAJI WA DAMU YA WATZ
Source - Tanzania Daima
Bilioni 2/- kutumika kesi za uchaguzi
na Irene Mark
ZAIDI ya sh bilioni 2.2 zitatumika kwa ajili ya kusikiliza kesi 43 za uchaguzi, kupinga matokeo ya ubunge katika vituo 11 vya Mahakama Kuu hapa nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Jaji Kiongozi Fakhih Jundu, alisema fedha hizo zinatakiwa kuifikia Mahakama kabla ya Februari mwakani wakati shughuli za mhimili huo zitakapoanza.
Alisema, kesi zilizofunguliwa hadi Desemba 10 mwaka huu zinalazimika kusikilizwa na kumalizika katika kipindi cha miaka miwili ambapo Mahakama Kuu itasikiliza kesi kwa mwaka mmoja na kutoa nafasi ya mwaka mwingine kwa ajili ya watakaokata rufaa kupinga hukumu zitakazotolewa.
Jaji Kiongozi huyo alibainisha kwamba kutokana na idadi ya Majaji waliopo, kila kesi inakadiriwa kusikilizwa ndani ya siku zisizopungua 45 huku ikikadiriwa kuwa na wastani wa mashahidi 15 kwa kila kesi.
"Inakisiwa kuwa kila kesi itasikilizwa kwa muda wa siku zisizopungua 45 vile vile wastani wa mashahidi 15 wanakadiriwa kuwepo kwenye kila kesi na ili haki iweze kutendeka, jaji hatasikiliza kesi katika kituo chake cha kazi hivyo tutalazimika kuwasafirisha majaji kutoka kituo kimoja kwenda kingine," alisema Jaji Kiongozi Jundu.
Katika ufafanuzi wa gharama za uendeshaji wa kesi hizo, Jaji huyo alisema kiasi cha sh 52,644,000 zitatumika kwa kila kesi hivyo kiasi cha sh 2,263,692,000 zitatumika kugharamia uendeshaji wa kesi zote 43 zinazopinga matokeo ya ubunge.
"…Hizi ni fedha nyingi na lazima serikali izitoe, tumeshaiandikia hazina itutafutie fedha hizi. Mahakama haina pesa, huu ni mzigo wa serikali lazima ibebe mzigo huu.
"Nasema lazima serikali izitoe kwa sababu ni matakwa ya demokrasia… na hizi ni gharama za demokrasia ni vizuri wote tufahamu hivyo," alisisitiza Jaji Kiongozi Jundu na kuongeza kwamba hiki ni kipindi cha likizo ya Mahakama hadi Februari mwakani tutakapoanza kazi.
Kadhalika, Jaji huyo alitoa rai kwa walalamikaji kujiandaa vema huku akiitaka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni mdau mkubwa kujiweka sawa ili kuziwezesha kesi hizi kufanyika bila vikwazo.
"Isije ikawa mtu kafungua kesi akiwa hajajiandaa ndiyo maana kwa kuzingatia gharama hizi ipo sheria inayomtaka mlalamikaji anayepinga matokeo kupeleka mahakamani kiasi cha sh milioni tano.
"Hizi ni kesi nzito lazima kujipanga mtu asiende kwa kujaribu kwa sababu mwisho wake matokeo yatakua mabaya kwa aliyefungua kesi itambidi kulipa faini… nawashauri kama mtu ameshindwa asubiri kipindi kijacho," alisisitiza Jaji huyo.
Aidha, alibainisha kuwa usikilizwaji wa kesi hizi utaathiri mwendelezo wa kesi nyingine kama za mauaji na nyinginezo hali inayoweza kusababisha malalamiko kutoka kwa wananchi wengine. Jaji Jundu aliitaja mikoa inayoongoza kwa wingi wa kesi hizo na idadi yake kwenye mabano kuwa ni Tabora (9), Dar es Salaam na Mwanza (7), Mtwara (5), Mbeya (4), Moshi (3), Dodoma, Iringa na Arusha (2) wakati Bukoba na Sumbawanga (1).