mshale21
JF-Expert Member
- Apr 8, 2021
- 2,050
- 4,904
Jumapili ya Septemba 18, 2021 Serikali itaweka wazi kilichosainiwa na Mawaziri wa pande mbili za Muungano katika kutatua kero za Tanganyika na Zanzibar.
Ahadi hiyo imetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa wakati akizungumzia mipango ya Taifa leo alipokutana na waandishi wa habari ofisini kwake Jijini Dodoma.
Msigwa amesema siku hiyo atamuita mtaalam ambaye atajibu swali hilo moja kwa moja kutipia mitandao ya kijamii ili Watanzania wajue pande mbili zimesaini kitu gani kwani siyo siri.
Ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali lililouzwa na mwananchi kwa njia ya simu akitaka kujua vitu gani vimesainiwa na pande mbili katika mkutano wao.
Hivi Karibuni Makamu wa Rais Dk Philip Mpango aliongoza kikao cha pamoja kati ya Serikali ya Mapinduzi na Serikali ya Muungano kikilenga kupunguza changamotoza muungano ambazo zimedumu kw amuda mrefu.
“Swali zuri sana hili, lakini naomba nisimalize uhondo tusubiri siku ya Jumapili nitamleta mtaalamu hapa hapa atasimama na kutoa maelezo ya kina nini kimeuznguma na utekelezaji wake utakuwaje,” alisema Msigwa.
Msigwa amesema Tanzania imepania kumaliza migogo ambayo imekuwa ni kero kwa pande zote hivyo wananchi waendelee kuamini kuamini kuwa serikali yao iko kazini na mambo yanaendelea.
Ahadi hiyo imetolewa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa wakati akizungumzia mipango ya Taifa leo alipokutana na waandishi wa habari ofisini kwake Jijini Dodoma.
Msigwa amesema siku hiyo atamuita mtaalam ambaye atajibu swali hilo moja kwa moja kutipia mitandao ya kijamii ili Watanzania wajue pande mbili zimesaini kitu gani kwani siyo siri.
Ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali lililouzwa na mwananchi kwa njia ya simu akitaka kujua vitu gani vimesainiwa na pande mbili katika mkutano wao.
Hivi Karibuni Makamu wa Rais Dk Philip Mpango aliongoza kikao cha pamoja kati ya Serikali ya Mapinduzi na Serikali ya Muungano kikilenga kupunguza changamotoza muungano ambazo zimedumu kw amuda mrefu.
“Swali zuri sana hili, lakini naomba nisimalize uhondo tusubiri siku ya Jumapili nitamleta mtaalamu hapa hapa atasimama na kutoa maelezo ya kina nini kimeuznguma na utekelezaji wake utakuwaje,” alisema Msigwa.
Msigwa amesema Tanzania imepania kumaliza migogo ambayo imekuwa ni kero kwa pande zote hivyo wananchi waendelee kuamini kuamini kuwa serikali yao iko kazini na mambo yanaendelea.