Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
Baraza la Taifa la uhifadhi na usimazi wa mazingira nchini NEMC limeitoza faini ya shilingi milioni 30 gereza la Keko lililopo manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaaam kwa kosa la kutiririsha kinyesi katika makazi ya watu.
Sambamba na hivyo gereza hilo limetakiwa kuacha mara moja kutirisha kinyesi hicho sambamba na kujenga mifumo sahihi ya uhifadhia wa maji taka ndani ya gereza hilo.
Chanzo: ITV