Gerala Hando wa Clouds Radio anajipendekeza kwa JK na CCM

Mbona mkuu amechambua vzr swala ni kwamba kinachofanyika hakiko kwenye mipango na wala hakilingani na hali halisi..
Mkuu tangu ln huyo jamaa km mwandish mwenye heshima?!.
Na hy ndy radio bora?!.
Ok,km ni hvyo utalalamika sana!..
 
Engineer Mtolera,
Ningetegemea kuwa katika fani yako ungekuwa ni mtu mwenye picha nzuri ya mambo jinsi yanavyotendeka ovyo, Lazima ujue kuwa serikali tumeipa dhamana ya kusimamia rasilimali zetu kwa uaminifu na umakini. Kufanya wajibu wake sio favour, Ni kodi zetu kwanini kusifia?Na tunatarajia return kubwa kutokana na kodi zetu, na siyo kubabaisha halafu mnasifia kitu gani?!! Ni miraadi mingapi inafanywa chini ya kiwango? Barabara ya Mbagala leo hii inarudiwa, kosa ni la nani? Nyinyi kama mainjinia mnatusaliti sana kwa tamaa ya Pesa!!:frusty:
Lazima kila mtu afanye wajibu wake kwa uaminifu mkubwa.
kaka
tatizo sio engineers kupenda pesa,tatizo ni yule anaetaka kutendewa kazi kulazimisha kazi iishe hata kama ni ya chini ya kiwango na mhusika akihitaji hivyo wewe kama mkandarasi unategemea kufanya nini? je utaondoka site? tambuwa kuwa mkataba unakuhitaji kumaliza kazi kwa siku tulizopangiana,lakini pesa zako hazitoshi kukamilisha kazi hiyo,mwisho wa siku unaruhusu kupunguza materials sehemu nyingine ili kufidia muda,
usitupe lawama kwa engineers,tupa lawama kwa mtoa kazi huku ana pesa za mawazo.
 
Hapa dawa ni kwa asiependa yanayoendelea basi na asipite juu ya hizo barabara. Na asipande treni za Mwakyembe. Acheni kujishaua.
 
Hivi hii awamu ya nne kuna barabara gani ya maana amabyo iliianza na sasa imeshakamilika . Kwa mfano awamu ya tatu walianza na dar-mwz na wakatoka ikiwa imebaki vipande vichache vya kumalizia ambavyo awamu ya nne imechukuwa miaka yote mitano ya mwanzo kuvimalizia. Tatizo la awamu ya nne hawana vipaumbele walivyoviweka na kuhakikisha vinatekelezwa wanaibuka tu kila kona wakizinduazindua tu lakini hakuna kinachokamilika. Halafu barabara zingine ni purely misaada ambayo hakuna hata centi ya serikali pale kwa hiyo hamna cha kujisifia pale. Awamu ya tatu waliamua kutenga kiasi fulani kutoka mapato ya ndani kwa ajili ya barabara and it worked very well! Hawa wa awamu ya nne wanataka kufanya mambo kiujanjaujanja tu kitu ambacho haitasaidia! Lazima wakubali kuachana na matumizi mabaya ya kaodi za umma ndipo wataweza kufanya kitu substantial otherwise wataishia tu kuzindua na kufungua miradi ambayo haijakamilika wakidhani watu watadanganyika!

kudos...well said mkuu
 
kaka
tatizo sio engineers kupenda pesa,tatizo ni yule anaetaka kutendewa kazi kulazimisha kazi iishe hata kama ni ya chini ya kiwango na mhusika akihitaji hivyo wewe kama mkandarasi unategemea kufanya nini? je utaondoka site? tambuwa kuwa mkataba unakuhitaji kumaliza kazi kwa siku tulizopangiana,lakini pesa zako hazitoshi kukamilisha kazi hiyo,mwisho wa siku unaruhusu kupunguza materials sehemu nyingine ili kufidia muda,
usitupe lawama kwa engineers,tupa lawama kwa mtoa kazi huku ana pesa za mawazo.

Mkuu sasa hizo quotations zinazofanyika zinakuwa kiini macho? Na hii miradi inayofadhiliwa na mashirika ya Kimataifa nayo pesa yake ni kiduchu?
 
Mlioandika hii na kuchangia hii thread kwa negativity Acheni utoto Wa shule nyinyi.
Mnachemka hamjistukii nyinyi!
 
Haya majamaa bana!
Angesifia M4C ingekuwa ndo jembe la clouds na mgemwagia sifa za kumwaga mpaka kusaza.
Mmechemka sana aisee!
 
MWANDISHI MWENYE HESHIMA??????WA CLOUDS???SIJAWAHI ONA WATAENDELEA NA USHOSTOGA MPAKA 2090 HUKO KWA SASA HAWANA NAFASI YA KUWA NA HESHIMA THEIR SELLING MTANDAO WA NuSU SHILINGI
 
Watangazaji wote wa clouds tabia zao ndo hizohizo.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Mkuu sasa hizo quotations zinazofanyika zinakuwa kiini macho? Na hii miradi inayofadhiliwa na mashirika ya Kimataifa nayo pesa yake ni kiduchu?
wewe unaongelea mashirika ambayo hadi leo baadhi hayajaleta pesa walizohaidi,na imepelekea serikali kutafuta pesa sehemu nyingine ili kufidia gharama ambazo mkandarasi ataziongeza kama muda wa mkataba utapita
elewa kuwa kila katapila linapopaki pale site ni pesa hiyo,sasa wafadhiri baadhi huchelewa kuleta pesa na si wakutegemea sana
 
Watu bwana! kumbe kuzungumza hata zuri moja analofanya Rais na Serikali ni ujinga? mbona Serikali imefanya mambo mengi mazuri sasa ibezwe kwa lipi?

Ni wajibu wa Serikali kutimiza wajibu wake hata isiposifiwa, wao si ndo wanaokusanya kodi? kwa mtazamo wangu hatupaswi kuisifu kwani ndo wajibu wake. Ila isipotimiza wajibu ni lazima ikosolewe.
 
Anataka apewe ukoo wa wilaya,unajua huyu jamaa alishawahi kugoma kupanga kugomea kipindi cha power breakfast yeye,masoud kipanya na Phina Mango pale clouds wakitaka mambo fulani yarekebishwe ,ila siku iliyofuatia jamaa kwa jinsi asivyojiamini akaenda kupiga magoti kwa kusaga na Ruge akarudishwa halafu wenzake Phina na Masoud wakafukuzwa,jamaa hajiamini hata kidogo!
 
Back
Top Bottom