Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,580
- 217,963
Diwani wa Zamani wa Njombe kupitia Chadema , George Sanga na wenzake leo anatimiza miaka 2 kamili Jela , kwa makosa ya uongo ya Mauaji aliyobambikiwa na watawala wa awamu ya 5 , ili kumkomoa kwa kuwa mwanachama wa Chadema na kumzuia kugombea uchaguzi wa 2020 ili Mgombea wa ccm apite bila kupingwa .
Sanga alikamatwa September 26 /2020 na ile serikali ya vitisho iliyokosa hoja na kutegemea utekaji na kusweka rumande hadi leo hii , ambapo kesi yake hiyo ya uongo inaendelea kupigwa danadana .
Nachukua nafasi hii kuwaomba viongozi wa Chadema Makao Makuu kuvunja Majadiliano ya Maridhiano haraka sana ikiwa Wanachama wake wanaendelea kusoteshwa Gerezani kwa kesi za Uongo , Marehemu wote waliouawa kwa sababu za kuwa kwao chadema , WAMEKUFA KISHUJAA na Mungu awapokee na awape Pumziko jema la milele , Amina
Namuomba Mwenyezi Mungu kuwajaalia nguvu , Afya njema na uvumilivu WanaChadema wote waliobambikwa kesi za uongo kwa sababu za Uchaguzi wa 2020 .
Sanga alikamatwa September 26 /2020 na ile serikali ya vitisho iliyokosa hoja na kutegemea utekaji na kusweka rumande hadi leo hii , ambapo kesi yake hiyo ya uongo inaendelea kupigwa danadana .
Nachukua nafasi hii kuwaomba viongozi wa Chadema Makao Makuu kuvunja Majadiliano ya Maridhiano haraka sana ikiwa Wanachama wake wanaendelea kusoteshwa Gerezani kwa kesi za Uongo , Marehemu wote waliouawa kwa sababu za kuwa kwao chadema , WAMEKUFA KISHUJAA na Mungu awapokee na awape Pumziko jema la milele , Amina
Namuomba Mwenyezi Mungu kuwajaalia nguvu , Afya njema na uvumilivu WanaChadema wote waliobambikwa kesi za uongo kwa sababu za Uchaguzi wa 2020 .