Geoffrey Mwambe: Hotel kubadilisha jina, haimaanishi kwamba wanakwepa kodi, acheni kudanganywa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,802
11,961
Mkurugenzi mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), amewatoa hofu Wananchi kuhusu hotel kubadilisha jina. Ameyasema hayo leo wakati akiongea na Wahariri wa Vyombo vya habari jijini Dar Es Salaam.

Watu wamekuwa wanapotosha kwamba hotel ikibadilisha jina basi ni njia ya kukwepa kodi, hilo si kweli na msikubali kudanganywa.

Watu wanabadilisha majina ya hotel mara nyingi ni kubadilisha brand yao. Na hausiani chochote na kodi kwani hakuna kipya kinachoongezeka wala kupungua kwenye uwekezaji huo ambacho kinagusa kodi. Na utaratibu upo wa kisheria ambao wanafuata ili kubadilisha jina.

Wengi wanatumia majina ya Hotel za huko nje mfano Serena, kempinski, hyatt nk. Mwisho wa siku unakuta wanashindwa kuelewana na wenye jina la hotel, matokeo yake wanabadilisha jina lingine eidha laweza kuwa jina la hotel lingine.

Hivyo kawaomba watu wabadili mtizamo wao pindi hotel inapo badilisha jina, hakuna Kodi inaibiwa.
 
Mzee baba alishazisema Co. za simu zinazobadili majina yao kwamba zilifanya kwa kukwepa kodi esp. Pale grace period ya 5 yrs ilipokua inaisha.
 
Watu Kuna kitu hawakielewi hasa waswahili ngozi nyeusi. Biashara unaweza uza bidhaa au huduma. Lakini pia waweza uza duka lako au kampuni yako kwa mtu.mwingine.Mfano kampuni ya mafita ya shell yaweza uza kampuni yake yote na Mali zake zote vikiwemo.vituo vyote vya mafita kwa Kampuni ya mafuta ya Total .

Akishanunua Total anabadili jina la vituo.vyote vya mafita kutoka She'll na kuwa Total.Lakini kila kitu kinaendelea Kama kawaida kwa mwendeshaji mpya hawi kakwepa Kodi au Nini.Ni.kama mtu ukinunua daladala ya mtu inayofanya kazi unabadili jina

Waswahili Hadi biashara huwa zinatufia mikononi tujizoeze kutangaza kuziuza tukiona zinatuelemea ziwe hotel,kampuni,shule,maduka no usisubiri Hadi zife
 
Back
Top Bottom