NetMaster
JF-Expert Member
- Sep 12, 2022
- 1,454
- 4,853
Kwanza kabisa nimpongeze Gentamycine kwa kuwa shabiki wa mpira zaidi kuliko shabiki wa timu, Ni mtu ambae Timu yake ikicheza hovyo hawezi kumezwa na ushabiki kuipamba, hata kwa haya mafanikio ya Yanga huwa hasiti kukubali kwamba Yanga wapo mbele kitu ambacho ni nadra kwa shabiki wa Simba, Lakini hii haimaanishi anafurahishwa na maendeleo ya Yanga, NO! Hutumia hali ya Yanga kuwakumbusha Simba kwamba wawe serious, wasibweteke, wasajili wachezaji wazuri, n.k ili wao Simba wawe mbele kuzidi Yanga.
Sasa tukija katika upande wa ushabiki wake wa Simba, hapa sasa ndipo Imeshakuwa kawaida kukuta nyuzi zake hata tatu kwa siku humu ndani zikiashiria maumivu ayapatayo kwa Yanga kuendelea ubabe wa ligi.
Kwa hali hii kiutani utani tunaweza kumpoteza mwana JF mwenzetu.
Nashauri akae mbali sana na mambo ya mpira.
Sasa tukija katika upande wa ushabiki wake wa Simba, hapa sasa ndipo Imeshakuwa kawaida kukuta nyuzi zake hata tatu kwa siku humu ndani zikiashiria maumivu ayapatayo kwa Yanga kuendelea ubabe wa ligi.
Kwa hali hii kiutani utani tunaweza kumpoteza mwana JF mwenzetu.
Nashauri akae mbali sana na mambo ya mpira.