BrAsMaRiLiSaShElMa
Senior Member
- Sep 23, 2016
- 149
- 181
Kwako OCD NYAMAGANA,
C.C. RPC MWANZA;
Bila kupoteza muda napenda nieleze juu ya uovu unaofanyika hapa eneo la SAHARA, mkabala na Posta Pamba Road.
Katika eneo hili kuna pilika nyingi za kibiashara, ambapo watu wengi kutoka sehemu mbalimbali hufika hapa ili kujipatia mahitaji yao mbalimbali.
Penye wengi pana mengi; wapo watu wanaofanya biashara zao halali na watoa huduma mbalimbali; lakini pia wapo watu waovu ambao wanawaibia watu wengine fedha na mali zao kwa ulaghai na utapeli na hata kwa kuwanyang'anya kibabe.
Miongoni mwa hawa watu waovu, lipo genge la watu ambalo linaweka banda kama ofisi kwa ajili ya kufanya uhalifu.
Watu hawa wamejenga hema au banda ambamo wameweka vitu vya kudanganyia watu kama TV, Redio, Generator, Sub Woofer n.k; huku wakiwashawishi wapitanjia wacheze kamari kwa kuweka fedha, ili eti waweze kujipatia vitu hivyo!
Watu hao wako kundi kubwa; wapo wakinamama, wapo vijana na watu wa makamo. Hawa wote hufanya kazi kwa pamoja huku wengine wakijifanya nao kuwa wateja, na hata kujifanya wameshinda zawadi au fedha kutoka kwa waendesha mchezo huo, kumbe ni wenzao.
Hufanya haya yote ili kuwashawishi wapitanjia waone kwamba kumbe kweli inawezekana mtu kunufaika na kamari ile, hivyo mtu hujitosa kuweka fedha zake ili ajipatie moja ya vifaa hivyo au azalishe fedha yake, lakini mwisho wake huwa ni kilio!!
Watu hawa ni hatari; wakikuona unamtahadharisha mtu asikubali kucheza kamari hiyo, basi watakusonga, kukupiga na hata kukupora mali yako na hutapata msaada maana watu wanawaogopa.
Haya yanafanyika wakati mkabala na banda lao ng'ambo ya barabara kuna askari polisi wenye silaha wanachunga benki ya posta; na mbele kidogo kabla ya kufika keep left ya Nyerere Road kuna kituo cha polisi Pamba Road.
Afande OCD Nyamagana, ina maana kweli wewe hujawahi kupata taarifa juu ya hawa wachezesha kamari ambao wanachezesha hadharani barabarani kutwa nzima siku 7 kwa wiki? Au unataka tuamini maneno yao kwamba huwa wanapeleka mgao sehemu sehemu?
Sipendi kuamini maneno yao hayo, lakini sielewi kwa nini watu hawa waendelee kuibia watu hadharani tena bila hofu wakati wewe upo Mjini na maofisa wako wengi wenye mbinu, weledi, vifaa na uwezo wa kisheria; kwa nini jambo kama hilo halikomeshwi?
Katika makabila kadhaa ya Tanzania na baadhi ya nchi jirani MULIRO maana yake ni MOTO; tunataka hicho kibanda kiwake moto kiteketee kabisa, kisiwepo tena hapo SAHARA; kinafedhehesha dola.
C.C. RPC MWANZA;
Bila kupoteza muda napenda nieleze juu ya uovu unaofanyika hapa eneo la SAHARA, mkabala na Posta Pamba Road.
Katika eneo hili kuna pilika nyingi za kibiashara, ambapo watu wengi kutoka sehemu mbalimbali hufika hapa ili kujipatia mahitaji yao mbalimbali.
Penye wengi pana mengi; wapo watu wanaofanya biashara zao halali na watoa huduma mbalimbali; lakini pia wapo watu waovu ambao wanawaibia watu wengine fedha na mali zao kwa ulaghai na utapeli na hata kwa kuwanyang'anya kibabe.
Miongoni mwa hawa watu waovu, lipo genge la watu ambalo linaweka banda kama ofisi kwa ajili ya kufanya uhalifu.
Watu hawa wamejenga hema au banda ambamo wameweka vitu vya kudanganyia watu kama TV, Redio, Generator, Sub Woofer n.k; huku wakiwashawishi wapitanjia wacheze kamari kwa kuweka fedha, ili eti waweze kujipatia vitu hivyo!
Watu hao wako kundi kubwa; wapo wakinamama, wapo vijana na watu wa makamo. Hawa wote hufanya kazi kwa pamoja huku wengine wakijifanya nao kuwa wateja, na hata kujifanya wameshinda zawadi au fedha kutoka kwa waendesha mchezo huo, kumbe ni wenzao.
Hufanya haya yote ili kuwashawishi wapitanjia waone kwamba kumbe kweli inawezekana mtu kunufaika na kamari ile, hivyo mtu hujitosa kuweka fedha zake ili ajipatie moja ya vifaa hivyo au azalishe fedha yake, lakini mwisho wake huwa ni kilio!!
Watu hawa ni hatari; wakikuona unamtahadharisha mtu asikubali kucheza kamari hiyo, basi watakusonga, kukupiga na hata kukupora mali yako na hutapata msaada maana watu wanawaogopa.
Haya yanafanyika wakati mkabala na banda lao ng'ambo ya barabara kuna askari polisi wenye silaha wanachunga benki ya posta; na mbele kidogo kabla ya kufika keep left ya Nyerere Road kuna kituo cha polisi Pamba Road.
Afande OCD Nyamagana, ina maana kweli wewe hujawahi kupata taarifa juu ya hawa wachezesha kamari ambao wanachezesha hadharani barabarani kutwa nzima siku 7 kwa wiki? Au unataka tuamini maneno yao kwamba huwa wanapeleka mgao sehemu sehemu?
Sipendi kuamini maneno yao hayo, lakini sielewi kwa nini watu hawa waendelee kuibia watu hadharani tena bila hofu wakati wewe upo Mjini na maofisa wako wengi wenye mbinu, weledi, vifaa na uwezo wa kisheria; kwa nini jambo kama hilo halikomeshwi?
Katika makabila kadhaa ya Tanzania na baadhi ya nchi jirani MULIRO maana yake ni MOTO; tunataka hicho kibanda kiwake moto kiteketee kabisa, kisiwepo tena hapo SAHARA; kinafedhehesha dola.