BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
Na Saed Kubenea
MABILIONI ya shilingi za walipa kodi, ambayo Edward Lowassa alishinikiza yalipwe kwa kampuni ya kutengeneza matairi ya General Tyre (GT), yameteketea.
Taarifa kutoka kiwandani, mkoani Arusha zinasema kiwanda kimefungwa na haijulikani kitapata wapi na lini mtaji mwingine wa kukifufua.
Lowassa, kabla ya kujiuzulu nafasi ya waziri mkuu, alishinikiza wizara ya fedha na mipango, chini ya Zakia Meghji, kutoa Sh. 10 bilioni kwa General Tyre ili kulinda kiwanda hiki kisifilisike.
Hivi sasa suala hili liko mezani kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye General Tyre inaomba akubali kuwa fedha zilizotolewa zilitumika vizuri, kinyume cha taarifa ya maodita waliopitia hesabu za kampuni hiyo.
General Tyre inaomba pia serikali iongeze fedha nyingine, juu ya mabilioni ambayo matumizi yake hadi sasa bado ni utata mtupu.
Kwa mujibu wa barua ya Katibu wa Lowassa wakati huo, B. Olekuyan kwa Katibu wa Meghji, Kumb. Na. PM/P/I/567/40 na iliyobeba kichwa cha maneno, General Tyre East Africa LTD Arusha,
Lowassa aliagiza kama ifuatavyo:
Taarifa zinasema Mramba na Lowassa waliafikiana serikali itoa fedha kwa GT, kwa mujibu wa barua ya 28 Juni 2007 iliyotoka kwa Mramba kwenda kwa Meghji.
Naye Mramba anajenga hoja ya kutolewa kwa fedha hizo haraka na bila masharti. Anaonya kwamba kuchelewa kutekeleza agizo la Lowassa kutasababisha kiwanda kufungwa.
Ushauri wangu kwako (Meghji) ni kwamba ujitahidi kuweka dhamana kwa ajili ya fedha hizo za NSSF haraka iwezekanavyo. Kama fedha zikikosekana, kiwanda hicho chaweza kufungwa, inasema barua hiyo ya Mramba kwa Meghji.
Hata hivyo, pamoja na kutolewa kwa mabilioni hayo ya shilingi, kiwanda hicho kimefungwa mwaka jana.
Aliyekuwa mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya kiwanda hicho, William Shelukindo, mbunge wa Bumbuli (CCM), amethibitishia gazeti hili kuwa kiwanda kimefungwa pamoja na mabilioni ya shilingi yaliyomwagwa humo.
Hata hivyo mabilioni hayo ya shilingi yameghubikwa na utata. Nyaraka ambazo gazeti hili limepata zinaonyesha kuwa siyo fedha zote zilizopelekwa kiwandani Arusha.
Nyaraka zinaonyesha kuwa Sh. 1 bilioni zililipwa kwa kampuni ya ukaguzi ya DAI Consulting kutoka nchini Afrika Kusini. Kampuni ya DAI ilipewa fedha hizo na NSSF kama gharama za ushauri kwa GT.
Lakini GT inalalamika, katika barua yake kwa Pinda, kuwa malipo ya Sh. 1 bilioni zilizotolewa kwa DAI Consulting ni fedha nyingi ikilinganishwa na kazi iliyofanyika.
Meneja Mkuu wa GT, Deven Lohani, raia wa Nepal, katika barua yake ya 17 Agosti 2009 kwa Waziri Mkuu Pinda, anaorodhesha malalamiko kuhusu usahihi wa matumizi ya mabilioni hayo.
Hata hivyo, kampuni ya matairi inasema haikuwa na njia nyingine ya kupinga malipo hayo kwa kuwa hiyo ilikuwa sehemu ya mkataba wa kupewa fedha hizo na NSSF. Kampuni ya DAI iliteuliwa na NSSF, inasema GT.
Ni muhimu kufahamu kwamba kampuni ya DAI Consulting ilipendekezwa kwetu na NSSF. Katika kipindi hicho GT ilikuwa na matatizo makubwa ya kifedha na ililazimika kukubali sharti hilo, inasema sehemu ya barua ya GT kwenda kwa Pinda.
Meneja Lohani ameeleza kuwa tatizo kubwa lilikuwa ni kiasi hicho kutolewa kwa mafungu-mafungu na si kwa jumla kama ilivyokuwa ikitarajiwa.
Shellukindo, hata hivyo, aliliambia MwanaHALISI kuwa kwa kadri anavyofahamu, nyingi ya fedha zilizotolewa kwa ajili ya kuifufua GT, zilitumika kwa ajili ya kulipa madeni mbalimbali yaliyokuwa yakiikabili kampuni hiyo.
Siwezi kusema kwa hakika ni kiasi gani kilitolewa na serikali katika kuifufua GT. Nilicho na uhakika nacho ni kuwa fedha nyingi zilitumika kulipa madeni ya kampuni, alisema Shellukindo.
Kwa kauli ya Shellukindo, Sh. 10 bilioni zilizotolewa na NSSF kwa udhamini wa serikali hazikutumika kufanya kazi iliyokusudiwa.
MABILIONI ya shilingi za walipa kodi, ambayo Edward Lowassa alishinikiza yalipwe kwa kampuni ya kutengeneza matairi ya General Tyre (GT), yameteketea.
Taarifa kutoka kiwandani, mkoani Arusha zinasema kiwanda kimefungwa na haijulikani kitapata wapi na lini mtaji mwingine wa kukifufua.
Lowassa, kabla ya kujiuzulu nafasi ya waziri mkuu, alishinikiza wizara ya fedha na mipango, chini ya Zakia Meghji, kutoa Sh. 10 bilioni kwa General Tyre ili kulinda kiwanda hiki kisifilisike.
Hivi sasa suala hili liko mezani kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye General Tyre inaomba akubali kuwa fedha zilizotolewa zilitumika vizuri, kinyume cha taarifa ya maodita waliopitia hesabu za kampuni hiyo.
General Tyre inaomba pia serikali iongeze fedha nyingine, juu ya mabilioni ambayo matumizi yake hadi sasa bado ni utata mtupu.
Kwa mujibu wa barua ya Katibu wa Lowassa wakati huo, B. Olekuyan kwa Katibu wa Meghji, Kumb. Na. PM/P/I/567/40 na iliyobeba kichwa cha maneno, General Tyre East Africa LTD Arusha,
Lowassa aliagiza kama ifuatavyo:
Tuliishaliamulia suala hili kwamba wapewe government guarantee kulinda kiwanda hiki, mkopo wa awali na ajira za Watanzania. Kama WF (waziri wa fedha) ana maoni tofauti alete kwenye kikao. Vinginevyo atekeleze kabla ya tarehe 15/7/2007.
Katika barua hiyo, ambayo katibu wa Lowassa alikuwa anapeleka pia kwa waziri wa viwanda biashara na masoko, wakati huo Basi Mramba, anaelekeza nakala yake ipelekwe kwa mawaziri wote wanaohusika ili wajue msimamo wa waziri mkuu.
Taarifa zinasema Mramba na Lowassa waliafikiana serikali itoa fedha kwa GT, kwa mujibu wa barua ya 28 Juni 2007 iliyotoka kwa Mramba kwenda kwa Meghji.
Naye Mramba anajenga hoja ya kutolewa kwa fedha hizo haraka na bila masharti. Anaonya kwamba kuchelewa kutekeleza agizo la Lowassa kutasababisha kiwanda kufungwa.
Ushauri wangu kwako (Meghji) ni kwamba ujitahidi kuweka dhamana kwa ajili ya fedha hizo za NSSF haraka iwezekanavyo. Kama fedha zikikosekana, kiwanda hicho chaweza kufungwa, inasema barua hiyo ya Mramba kwa Meghji.
Hata hivyo, pamoja na kutolewa kwa mabilioni hayo ya shilingi, kiwanda hicho kimefungwa mwaka jana.
Aliyekuwa mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya kiwanda hicho, William Shelukindo, mbunge wa Bumbuli (CCM), amethibitishia gazeti hili kuwa kiwanda kimefungwa pamoja na mabilioni ya shilingi yaliyomwagwa humo.
Hata hivyo mabilioni hayo ya shilingi yameghubikwa na utata. Nyaraka ambazo gazeti hili limepata zinaonyesha kuwa siyo fedha zote zilizopelekwa kiwandani Arusha.
Nyaraka zinaonyesha kuwa Sh. 1 bilioni zililipwa kwa kampuni ya ukaguzi ya DAI Consulting kutoka nchini Afrika Kusini. Kampuni ya DAI ilipewa fedha hizo na NSSF kama gharama za ushauri kwa GT.
Lakini GT inalalamika, katika barua yake kwa Pinda, kuwa malipo ya Sh. 1 bilioni zilizotolewa kwa DAI Consulting ni fedha nyingi ikilinganishwa na kazi iliyofanyika.
Meneja Mkuu wa GT, Deven Lohani, raia wa Nepal, katika barua yake ya 17 Agosti 2009 kwa Waziri Mkuu Pinda, anaorodhesha malalamiko kuhusu usahihi wa matumizi ya mabilioni hayo.
Hata hivyo, kampuni ya matairi inasema haikuwa na njia nyingine ya kupinga malipo hayo kwa kuwa hiyo ilikuwa sehemu ya mkataba wa kupewa fedha hizo na NSSF. Kampuni ya DAI iliteuliwa na NSSF, inasema GT.
Ni muhimu kufahamu kwamba kampuni ya DAI Consulting ilipendekezwa kwetu na NSSF. Katika kipindi hicho GT ilikuwa na matatizo makubwa ya kifedha na ililazimika kukubali sharti hilo, inasema sehemu ya barua ya GT kwenda kwa Pinda.
Meneja Lohani ameeleza kuwa tatizo kubwa lilikuwa ni kiasi hicho kutolewa kwa mafungu-mafungu na si kwa jumla kama ilivyokuwa ikitarajiwa.
Shellukindo, hata hivyo, aliliambia MwanaHALISI kuwa kwa kadri anavyofahamu, nyingi ya fedha zilizotolewa kwa ajili ya kuifufua GT, zilitumika kwa ajili ya kulipa madeni mbalimbali yaliyokuwa yakiikabili kampuni hiyo.
Siwezi kusema kwa hakika ni kiasi gani kilitolewa na serikali katika kuifufua GT. Nilicho na uhakika nacho ni kuwa fedha nyingi zilitumika kulipa madeni ya kampuni, alisema Shellukindo.
Kwa kauli ya Shellukindo, Sh. 10 bilioni zilizotolewa na NSSF kwa udhamini wa serikali hazikutumika kufanya kazi iliyokusudiwa.