Geita yatangaza uhaba mkubwa wa walimu hasa wa Sayansi na Hisabati

Serikali haina uwezo wa kuajiri hiii porojo tupu
Uchumi hauwezi kwenda kwa kuajiri tuu, lazima Halmashauri zichukue hatua wanazoweza kama kuajiri walimu kwa mikataba kwa mapato yao ya ndani badala ya kuhangaika eti na walemavu na wamama.
 
Tatizo la uhaba wa Walimu wa Masomo ya Sayansi na Hisabati kwa Shule za Sekondari mkoani Geita limefikia asilimia 56 hadi sasa, hali inayosababisha wanafunzi wengi kutofanya vizuri kwenye masomo hayo na kuathiri maendeleo ya elimu mkoani hapa.

Akitoa taarifa ya elimu mkoani hapa wiki iliyopita, Ofisa Elimu Mkoa wa Geita, Anton Mtweve alisema hadi mkoa huo una uhitaji mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi 1,715, huku waliopo ni 744 na upungufu ni walimu 972.

Alisema pia shule za sekondari mkoani hapa zinakabiliwa na upungufu wa walimu wa masomo ya sanaa 430 ambapo kwa sasa kuna walimu wa masomo hayo 2,106 ikilinganishwa na mahitaji ya walimu 2,416.

Mtweve alisema kwa upande wa shule za msingi mkoani hapa nazo zinakabiliwa na upungufu wa walimu 7,565 kwani waliopo ni 8,796 ikilinganishwa na mahitaji ya walimu 16,361 sawa na asilimia 46.2.

"Tofauti ya uwiano kati ya walimu na wanafunzi ni kubwa sana ikilinganishwa na mwaka jana, hali hiyo imesababishwa na ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali na darasa la kwanza mwaka huu," alisema.

Akitoa taarifa ya hali ya ufaulu kwa shule za msingi na sekondari mkoani hapa, Mtweve alisema ndani ya kipindi cha miaka mitatu (2018-2020), kiwango cha ufaulu kwa mtihani wa taifa wa darasa la saba na kidato cha nne umekuwa wa kupanda na kushuka.

"Kwa mtihani wa taifa wa darasa la saba mwaka 2018 ufaulu ulikuwa asilimia 88.53, mwaka 2019 asilimia 79.12 na mwaka jana ulifikia asilimia 82.49, huku kwa mtihani wa taifa wa kidato cha nne mwaka 2018 ufaulu ulikuwa asilimia 91.7, mwaka 2019 asilimia 87.13 na mwaka jana ufaulu ulifikia asilimia 89.15," alisema.

Akizungumzia changamoto ya uhaba wa walimu wa masomo ya sanyansi, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyamule aliziagiza halmashauri zote kuangalia namna ya kupata walimu wa muda wanaoweza kupunguza ukubwa wa tatizo hilo na kuinua ufaulu wa masomo hayo.
RC atakuwa mgeni kwenye hii nchi au kwenye takwimu. Hili ni tatizo la nchi nzima, kila RC aliamua atie takwimu za mahitaji ya waalimu mkoani mwake atajiona yeye ni ana nafuu kubwa.
 
zamu ya geita iliishia machi 17... tupo unguja kwa sasa na tanga.

ajira za majuzi ummy na shemdoe walimwaga walimu Wa kutosha kwao kama alivyofanya jaffo kupeleka walimu chato.
 
Hivi mbona mnaziiamini Sana siasa za kwamba walimu wanatosha ilihali mmtengaziwa tu jamaaani

Elimu Bure imesababisha influx ya wanafunzi wengi ilihali influx ya walimu imekuwa ndogo saaa na kucover ongezeko la mapema la wanafunzi
 
Acha mamb yako bhana sio kwel kuwa mwalimu alipata D pale DUCE tumesoma watu kibao wenye ufauli mzur tuu nikiwemo mimi na A
Achana naye huyo amekariri. Ni miongoni mwa vilaza ambao bado wameshikilia mentality ya kudhani mwalimu ni mtu aliyefeli lakini ukimwambia aweke matokeo yake mezani kulinganisha ufaulu anatoka nduki
 
Nawasalimu kwa jina divided republic of Tanzania nanyi mnajibu uzembe uendelee!!
Tatizo la uhaba wa Walimu wa Masomo ya Sayansi na Hisabati kwa Shule za Sekondari mkoani Geita limefikia asilimia 56 hadi sasa, hali inayosababisha wanafunzi wengi kutofanya vizuri kwenye masomo hayo na kuathiri maendeleo ya elimu mkoani hapa.

Akitoa taarifa ya elimu mkoani hapa wiki iliyopita, Ofisa Elimu Mkoa wa Geita, Anton Mtweve alisema hadi mkoa huo una uhitaji mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi 1,715, huku waliopo ni 744 na upungufu ni walimu 972.

Alisema pia shule za sekondari mkoani hapa zinakabiliwa na upungufu wa walimu wa masomo ya sanaa 430 ambapo kwa sasa kuna walimu wa masomo hayo 2,106 ikilinganishwa na mahitaji ya walimu 2,416.

Mtweve alisema kwa upande wa shule za msingi mkoani hapa nazo zinakabiliwa na upungufu wa walimu 7,565 kwani waliopo ni 8,796 ikilinganishwa na mahitaji ya walimu 16,361 sawa na asilimia 46.2.

"Tofauti ya uwiano kati ya walimu na wanafunzi ni kubwa sana ikilinganishwa na mwaka jana, hali hiyo imesababishwa na ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali na darasa la kwanza mwaka huu," alisema.

Akitoa taarifa ya hali ya ufaulu kwa shule za msingi na sekondari mkoani hapa, Mtweve alisema ndani ya kipindi cha miaka mitatu (2018-2020), kiwango cha ufaulu kwa mtihani wa taifa wa darasa la saba na kidato cha nne umekuwa wa kupanda na kushuka.

"Kwa mtihani wa taifa wa darasa la saba mwaka 2018 ufaulu ulikuwa asilimia 88.53, mwaka 2019 asilimia 79.12 na mwaka jana ulifikia asilimia 82.49, huku kwa mtihani wa taifa wa kidato cha nne mwaka 2018 ufaulu ulikuwa asilimia 91.7, mwaka 2019 asilimia 87.13 na mwaka jana ufaulu ulifikia asilimia 89.15," alisema.

Akizungumzia changamoto ya uhaba wa walimu wa masomo ya sanyansi, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyamule aliziagiza halmashauri zote kuangalia namna ya kupata walimu wa muda wanaoweza kupunguza ukubwa wa tatizo hilo na kuinua ufaulu wa masomo hayo.
 
Ummy Mwalimu ni muongo sana..

Tatizo la uhaba wa Walimu wa Masomo ya Sayansi na Hisabati kwa Shule za Sekondari mkoani Geita limefikia asilimia 56 hadi sasa, hali inayosababisha wanafunzi wengi kutofanya vizuri kwenye masomo hayo na kuathiri maendeleo ya elimu mkoani hapa.

Akitoa taarifa ya elimu mkoani hapa wiki iliyopita, Ofisa Elimu Mkoa wa Geita, Anton Mtweve alisema hadi mkoa huo una uhitaji mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi 1,715, huku waliopo ni 744 na upungufu ni walimu 972.

Alisema pia shule za sekondari mkoani hapa zinakabiliwa na upungufu wa walimu wa masomo ya sanaa 430 ambapo kwa sasa kuna walimu wa masomo hayo 2,106 ikilinganishwa na mahitaji ya walimu 2,416.

Mtweve alisema kwa upande wa shule za msingi mkoani hapa nazo zinakabiliwa na upungufu wa walimu 7,565 kwani waliopo ni 8,796 ikilinganishwa na mahitaji ya walimu 16,361 sawa na asilimia 46.2.

"Tofauti ya uwiano kati ya walimu na wanafunzi ni kubwa sana ikilinganishwa na mwaka jana, hali hiyo imesababishwa na ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali na darasa la kwanza mwaka huu," alisema.

Akitoa taarifa ya hali ya ufaulu kwa shule za msingi na sekondari mkoani hapa, Mtweve alisema ndani ya kipindi cha miaka mitatu (2018-2020), kiwango cha ufaulu kwa mtihani wa taifa wa darasa la saba na kidato cha nne umekuwa wa kupanda na kushuka.

"Kwa mtihani wa taifa wa darasa la saba mwaka 2018 ufaulu ulikuwa asilimia 88.53, mwaka 2019 asilimia 79.12 na mwaka jana ulifikia asilimia 82.49, huku kwa mtihani wa taifa wa kidato cha nne mwaka 2018 ufaulu ulikuwa asilimia 91.7, mwaka 2019 asilimia 87.13 na mwaka jana ufaulu ulifikia asilimia 89.15," alisema.

Akizungumzia changamoto ya uhaba wa walimu wa masomo ya sanyansi, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyamule aliziagiza halmashauri zote kuangalia namna ya kupata walimu wa muda wanaoweza kupunguza ukubwa wa tatizo hilo na kuinua ufaulu wa masomo hayo.
 
Tatizo la uhaba wa Walimu wa Masomo ya Sayansi na Hisabati kwa Shule za Sekondari mkoani Geita limefikia asilimia 56 hadi sasa, hali inayosababisha wanafunzi wengi kutofanya vizuri kwenye masomo hayo na kuathiri maendeleo ya elimu mkoani hapa.

Akitoa taarifa ya elimu mkoani hapa wiki iliyopita, Ofisa Elimu Mkoa wa Geita, Anton Mtweve alisema hadi mkoa huo una uhitaji mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi 1,715, huku waliopo ni 744 na upungufu ni walimu 972.

Alisema pia shule za sekondari mkoani hapa zinakabiliwa na upungufu wa walimu wa masomo ya sanaa 430 ambapo kwa sasa kuna walimu wa masomo hayo 2,106 ikilinganishwa na mahitaji ya walimu 2,416.

Mtweve alisema kwa upande wa shule za msingi mkoani hapa nazo zinakabiliwa na upungufu wa walimu 7,565 kwani waliopo ni 8,796 ikilinganishwa na mahitaji ya walimu 16,361 sawa na asilimia 46.2.

"Tofauti ya uwiano kati ya walimu na wanafunzi ni kubwa sana ikilinganishwa na mwaka jana, hali hiyo imesababishwa na ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la awali na darasa la kwanza mwaka huu," alisema.

Akitoa taarifa ya hali ya ufaulu kwa shule za msingi na sekondari mkoani hapa, Mtweve alisema ndani ya kipindi cha miaka mitatu (2018-2020), kiwango cha ufaulu kwa mtihani wa taifa wa darasa la saba na kidato cha nne umekuwa wa kupanda na kushuka.

"Kwa mtihani wa taifa wa darasa la saba mwaka 2018 ufaulu ulikuwa asilimia 88.53, mwaka 2019 asilimia 79.12 na mwaka jana ulifikia asilimia 82.49, huku kwa mtihani wa taifa wa kidato cha nne mwaka 2018 ufaulu ulikuwa asilimia 91.7, mwaka 2019 asilimia 87.13 na mwaka jana ufaulu ulifikia asilimia 89.15," alisema.

Akizungumzia changamoto ya uhaba wa walimu wa masomo ya sanyansi, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyamule aliziagiza halmashauri zote kuangalia namna ya kupata walimu wa muda wanaoweza kupunguza ukubwa wa tatizo hilo na kuinua ufaulu wa masomo hayo.
Wamfufue meko ndio awafundishe kua kipimo cha corona kinapima oil na papai,huko hawaitaji kujua sayansi wao ni kuloga na kuuana
 
Kama walimu wa sayansi wameisha si muwaajiri madaktari ma wafamasia wakafundishe
Nadhani shida Bajeti.Walimu wapo wamejishikiza praivetini huku.Ingawa hata wakiajiriwa wote wa Sayansi na Hisabati bado upungufu utakuwepo tu.Ok dear students in case you want to know me,I'm actually a teacher of very hard subjects.Very hard.Are we together?

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Nadhani labda zije tozo nyingine.Hizi si tumeambiwa kwa ajili ya mabarabara bush huko?

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
Pesa inayokusanywa ni nyingi mno inaweza kufanya mambo yote mawili kwa wakati mmoja. Na kumbuka hapo tozo peke yake hatujagusia kodi za kawaida zinazotokana na rasmali tulizonazo na zinazokusanywa kwa wananchi kila siku
 
Pesa inayokusanywa ni nyingi mno inaweza kufanya mambo yote mawili kwa wakati mmoja. Na kumbuka hapo tozo peke yake hatujagusia kodi za kawaida zinazotokana na rasmali tulizonazo na zinazokusanywa kwa wananchi kila siku
Vipi kuhusu deni letu la Trilioni 71.Hili huwa tunalirejeshaje?

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom