Geita: TAKUKURU yabaini ‘upigaji’ miradi ya Tsh bilioni 18

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,808
11,973
Miradi 15 yenye thamani ya Tsh. Bilioni 18.3 Mkoani Geita imebainika kuwa na upungufu wa kutozingatiwa kwa vigezo na masharti ya mikataba, hiyo imesababishwa na kukosekana kwa usimamizi wa wataalamu wa Halmashauri.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imebainisha na kueleza hayo yamebainika katika utafiti wao uliofanyika Januari hadi Machi, 2022, wakieleza kuwa kuna baadhi ya mafundi walioshinda zabuni za ujenzi hawajaonekana eneo la mradi, wamewaacha mafundi wasaidizi bila usimamizi wala maelekezo eneo la ujenzi.

Mkuu wa #TAKUKURU Geita, Leonidas Felix amesema mbali na hapo, kuna miradi minne ya elimu yenye thamani ya Tsh milioni 340 imebainika kuwa na viashiria vya ufujaji na ubadhirifu wa fedha, ameeleza kuwa uchunguzi unaendelea Mkoani hapo.


0001.jpg

0002.jpg


0003.jpg

0004.jpg

0005.jpg
 
Ni vyema Chombo chetu cha TAKUKURU kikajikita kwenye Kuzuia zaidi kuliko kusubiria kuchunguza!!

Kuzuia uhalifu kutawezesha kuokoa fedha za umma kuliko kuchunguza.

Okoeni fedha za umma, fuatilieni miradi mikubwa inayo endelea.

Mfano mzuri ni jinsi TAKUKURU pamoja na vyombo vingine vilivyo fuatilia kwa karibu mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa fedha za COVID19, hakuna hata shilingi iliyo liwa, thamani ya fedha ilionekana kila mahali yalipo jengwa.
Hivyo ndivyo vyonbo vyetu vinapaswa vifanye kazi.

Ufuatiliaji wa karibu ktk kila miradi inayo endelea ni muhimu sana, ujenzi wa mabarabara za TARURA ambazo kwa sasa simeshika kasi kila kona ya nchi n.k n.k.................

Endapo TAKUKURU itaamua kufuatilia kwa karibu kila miradi ya Serikali na taasisi zake hakika fedha za umma zitatumika vizuri na thamani ya fedha itaonekana.
 
Hivi tajiri akifadhiri wacheza filamu mpaka uzinduzi wake nje na ndani ya nchi bila mkataba wa makubaliano Fulani hii si ni rushwa ya kuomba kikubwa kuliko rushwa aliyotoa? TAKUKURU wangechunguza hawa wafadhili.
 
Kazi nzuri Sana Bw. Leonidas Felix Rugemarila utafika mbali komaa Wananchi wapate haki na kuzuia leakages za mipunga ya maendeleo
 
No vyema Chombo chetu cha TAKUKURU kikajikita kwenye Kuzuia zaidi kuliko kuchinguza.

Kuzuia uhalifu kutawezesha kuokoa fedha za umma kuliko kuchunguza.

Okoeni fedha za umma, fuatilieni miradi mikubwa inayo endelea.

Mfano mzuri ni jinsi TAKUKURU pamoja na vyombo vingine vilivyo fuatilia kwa karibu mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa fedha za COVID19, hakuna hata shilingi iliyo liwa, thamani ya fedha ilionekana kila mahali yalipo jengwa.
Hivyo ndivyo vyonbo vyetu vinapaswa vifanye kazi.
Ufuatiliaji wa karibu ktk kila miradi inayo endelea ni muhimu sana, ujenzi wa mabarabara za TARURA ambazo kwa sasa simeshika kasi kila kona ya nchi n.k n.k.................
Endapo TAKUKURU itaamua kufuatilia kwa karibu kila miradi ya Serikali na taasisi zake hakika fedha za umma zitatumika vizuri na thamani ya fedha itaonekana.
Kweli
 
Ni vyema Chombo chetu cha TAKUKURU kikajikita kwenye Kuzuia zaidi kuliko kusubiria kuchunguza!!

Kuzuia uhalifu kutawezesha kuokoa fedha za umma kuliko kuchunguza.

Okoeni fedha za umma, fuatilieni miradi mikubwa inayo endelea.

Mfano mzuri ni jinsi TAKUKURU pamoja na vyombo vingine vilivyo fuatilia kwa karibu mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa fedha za COVID19, hakuna hata shilingi iliyo liwa, thamani ya fedha ilionekana kila mahali yalipo jengwa.
Hivyo ndivyo vyonbo vyetu vinapaswa vifanye kazi.

Ufuatiliaji wa karibu ktk kila miradi inayo endelea ni muhimu sana, ujenzi wa mabarabara za TARURA ambazo kwa sasa simeshika kasi kila kona ya nchi n.k n.k.................

Endapo TAKUKURU itaamua kufuatilia kwa karibu kila miradi ya Serikali na taasisi zake hakika fedha za umma zitatumika vizuri na thamani ya fedha itaonekana.

TAKUKURU wangejikita kuchunguza pesa za capitation (elimu bure) zinaliwa sana na walimu wakuu mkoan Geita, TAKUKURU chunguzeni
 
Takukuru wangejikita kuchunguza pesa za capitation (elimu bure)zinaliwa sana na walimu wakuu mkoan geita,takukuru chunguzeni
Mkuu tupiganie Katiba Mpya , Kwenye Katiba mpya aliyeshiriki wizi wa Plea Bargain haiwezekani awe Mwanasheria Mkuu wa Serikali , Hayo ni Matusi
 
Miradi 15 yenye thamani ya Tsh. Bilioni 18.3 Mkoani Geita imebainika kuwa na upungufu wa kutozingatiwa kwa vigezo na masharti ya mikataba, hiyo imesababishwa na kukosekana kwa usimamizi wa wataalamu wa Halmashauri.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imebainisha na kueleza hayo yamebainika katika utafiti wao uliofanyika Januari hadi Machi, 2022, wakieleza kuwa kuna baadhi ya mafundi walioshinda zabuni za ujenzi hawajaonekana eneo la mradi, wamewaacha mafundi wasaidizi bila usimamizi wala maelekezo eneo la ujenzi.

Mkuu wa #TAKUKURU Geita, Leonidas Felix amesema mbali na hapo, kuna miradi minne ya elimu yenye thamani ya Tsh milioni 340 imebainika kuwa na viashiria vya ufujaji na ubadhirifu wa fedha, ameeleza kuwa uchunguzi unaendelea Mkoani hapo.


Tuko bize na royal tour bana?!
Hata ndoo ikiwa na matundu bado itajaa maji tu chifu! Watalii wanaleta madola!
 
Takukuru wangejikita kuchunguza pesa za capitation (elimu bure)zinaliwa sana na walimu wakuu mkoan geita,takukuru chunguzeni
Toa taarifa za ukweli na uhakika.
kama ni za kweli uchunguzi utafanyika na wahusika watafikishwa Mahakamani kukabili tuhuma zao.
 
Back
Top Bottom