Lipijema
JF-Expert Member
- Mar 8, 2015
- 809
- 1,193
Nawasalimu, nilipo ni wilaya yetu ya Geita jimbo la Mbunge wetu machachari anayejulikana kama Kasheku Musukuma. Mvua ambayo huwa sisi wakulima huwa tunaita"Mvua ya kuaribu matofali" au " Mvua ya kuotesha nyasi" Leo imenyesha kuanzia asubuhi ya saa mbili hadi mida hii ndipo imeanza kupunguza kasi, hii mvua mara nyingi huwa ni ya siku moja tu kabla ya masika kuanza na kwa bahati mbaya huwa haitabiriki hata na TMA.