Greatest Of All Time
JF-Expert Member
- Jan 1, 2017
- 20,713
- 45,096
Ni mechi kubwa kwa wapenzi wa soka wa Kanda ya Ziwa. Geita Gold itakuwa inawakaribisha Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC katika Dimba la CCM Kirumba pale jijini Mwanza.
Geita imehamishia mchezo huu katika dimba hilo badala ya Nyankumbu ili kuongeza kipato. Kitendo hiko kimekemewa sana na mashabiki wa Geita.
Kocha Mkuu wa Geita, Fred Felix Minziro anasema timu yake iko vizuri wachezaji wana morali na mechi na leo wako tayari kupambana na kuvuna alama 3.
Yanga itaingia uwanjani ikimkosa Saido Ntibazonkiza aliyebaki Dar, huku winga Chico Ushindi naye akikosekana katika mchezo huu.
Mechi ni saa 10:00 jioni kupitia Azam Sports 1HD na updates zitakujia hapahapa, usikose kujumuika nasi...
======
Mpira umekwisha kwa Geita kukubali kichapo cha bao moja bila majibu kutoka kwa Young Africans, goli pekee la mchezo likifungwa na Fiston Mayele dakika ya kwanza.
Geita imehamishia mchezo huu katika dimba hilo badala ya Nyankumbu ili kuongeza kipato. Kitendo hiko kimekemewa sana na mashabiki wa Geita.
Kocha Mkuu wa Geita, Fred Felix Minziro anasema timu yake iko vizuri wachezaji wana morali na mechi na leo wako tayari kupambana na kuvuna alama 3.
Yanga itaingia uwanjani ikimkosa Saido Ntibazonkiza aliyebaki Dar, huku winga Chico Ushindi naye akikosekana katika mchezo huu.
Mechi ni saa 10:00 jioni kupitia Azam Sports 1HD na updates zitakujia hapahapa, usikose kujumuika nasi...
======
Mpira umekwisha kwa Geita kukubali kichapo cha bao moja bila majibu kutoka kwa Young Africans, goli pekee la mchezo likifungwa na Fiston Mayele dakika ya kwanza.