Geita Gold Fc 0-1 Yanga Sc | NBC PL | CCM Kirumba

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Jan 1, 2017
20,713
45,096
Ni mechi kubwa kwa wapenzi wa soka wa Kanda ya Ziwa. Geita Gold itakuwa inawakaribisha Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC katika Dimba la CCM Kirumba pale jijini Mwanza.

Geita imehamishia mchezo huu katika dimba hilo badala ya Nyankumbu ili kuongeza kipato. Kitendo hiko kimekemewa sana na mashabiki wa Geita.

Kocha Mkuu wa Geita, Fred Felix Minziro anasema timu yake iko vizuri wachezaji wana morali na mechi na leo wako tayari kupambana na kuvuna alama 3.

Yanga itaingia uwanjani ikimkosa Saido Ntibazonkiza aliyebaki Dar, huku winga Chico Ushindi naye akikosekana katika mchezo huu.

Mechi ni saa 10:00 jioni kupitia Azam Sports 1HD na updates zitakujia hapahapa, usikose kujumuika nasi...

======

Mpira umekwisha kwa Geita kukubali kichapo cha bao moja bila majibu kutoka kwa Young Africans, goli pekee la mchezo likifungwa na Fiston Mayele dakika ya kwanza.
 
Dozi inaendelea leo

FNAl2FqWYAYGSos.jpeg
 
Mode toeni uchafu huu. Sio kila timu mtu apandishe uzi jf, timu zote za mchangani hizi iweje iletwe humu na wakati Facebook ipo? Eti leo Manyema acheze na Mlale mtu aanzishe uzu humu,tuwe serious jamani sio kila kitu hadi aseme Putin mode mjiongeze tu Active Mhariri na Boqin mpo live na mmeona uchafu huu.
Asante kwa ushauri tumepokea taarifa hizo na kwa bahati mbaya tunakutarifu uzi huu utakuwa wa Moto 🔥.

Ila Geita ikifungwa tunafuta uzi ila Geita ikishinda tuna ubana kabisa kwenye jukwaa hili na uwe special thread.

Asante
 
Back
Top Bottom