Ferruccio Lamborghini
JF-Expert Member
- Apr 15, 2020
- 1,664
- 2,517
Mwanaume anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 18 hadi 22 ameuawa na mwili wake kuchomwa moto na wananchi wakidai kuwa alijaribu kutaka kumbaka mwanafunzi wa kidato cha pili katika Sekondari iliyopo Kata ya Bombambili mjini Geita.
Tukio hilo limetokea leo Alhamisi Februari 24, 2022 saa 12.30 asubuhi wakati mwanafunzi huyo akiwa njiani kwenda shule.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amethibitisha kutokea tukio hilo na kueleza kuwa mwanafunzi huyo alitoka nyumbani alfajiri kuwahi shuleni na akiwa njiani ndipo alipokamatwa na kijana huyo akimvutia kichakani kwa lengo la kumbaka.
“Alipomkamata mwanafunzi alipiga kelele na wananchi walikusanyika na kumzingira. Walianza kumuokoa mwanafunzi na kumpeleka shule kisha kumshambulia kijana huyo hadi kumuua na mwili wake kuchomwa moto,” amesema Kamanda Mwaibambe.
Kufuatia tukio hilo, Mwenyekiti wa mtaa huo Salum Maige anashikiliwa na Polisi kusaidia kufahamika kwa wote waliohusika kwenye mauji hayo.
“Marehemu alishazingirwa hatuoni sababu za kumuua zaidi ya kumfikisha kwenye vyombo vya sheria. Kwa kuwa mauaji yamefanywa na wananchi wa eneo hilo tunamshikilia mwenyekiti ili asaidie polisi kuwapata wahusika,” ameongeza.
Mwananchi
Tukio hilo limetokea leo Alhamisi Februari 24, 2022 saa 12.30 asubuhi wakati mwanafunzi huyo akiwa njiani kwenda shule.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amethibitisha kutokea tukio hilo na kueleza kuwa mwanafunzi huyo alitoka nyumbani alfajiri kuwahi shuleni na akiwa njiani ndipo alipokamatwa na kijana huyo akimvutia kichakani kwa lengo la kumbaka.
“Alipomkamata mwanafunzi alipiga kelele na wananchi walikusanyika na kumzingira. Walianza kumuokoa mwanafunzi na kumpeleka shule kisha kumshambulia kijana huyo hadi kumuua na mwili wake kuchomwa moto,” amesema Kamanda Mwaibambe.
Kufuatia tukio hilo, Mwenyekiti wa mtaa huo Salum Maige anashikiliwa na Polisi kusaidia kufahamika kwa wote waliohusika kwenye mauji hayo.
“Marehemu alishazingirwa hatuoni sababu za kumuua zaidi ya kumfikisha kwenye vyombo vya sheria. Kwa kuwa mauaji yamefanywa na wananchi wa eneo hilo tunamshikilia mwenyekiti ili asaidie polisi kuwapata wahusika,” ameongeza.
Mwananchi