Geita: Auawa akidaiwa kujaribu kumbaka mwanafunzi

Ferruccio Lamborghini

JF-Expert Member
Apr 15, 2020
1,664
2,517
Mwanaume anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 18 hadi 22 ameuawa na mwili wake kuchomwa moto na wananchi wakidai kuwa alijaribu kutaka kumbaka mwanafunzi wa kidato cha pili katika Sekondari iliyopo Kata ya Bombambili mjini Geita.

Tukio hilo limetokea leo Alhamisi Februari 24, 2022 saa 12.30 asubuhi wakati mwanafunzi huyo akiwa njiani kwenda shule.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amethibitisha kutokea tukio hilo na kueleza kuwa mwanafunzi huyo alitoka nyumbani alfajiri kuwahi shuleni na akiwa njiani ndipo alipokamatwa na kijana huyo akimvutia kichakani kwa lengo la kumbaka.

“Alipomkamata mwanafunzi alipiga kelele na wananchi walikusanyika na kumzingira. Walianza kumuokoa mwanafunzi na kumpeleka shule kisha kumshambulia kijana huyo hadi kumuua na mwili wake kuchomwa moto,” amesema Kamanda Mwaibambe.

Kufuatia tukio hilo, Mwenyekiti wa mtaa huo Salum Maige anashikiliwa na Polisi kusaidia kufahamika kwa wote waliohusika kwenye mauji hayo.

“Marehemu alishazingirwa hatuoni sababu za kumuua zaidi ya kumfikisha kwenye vyombo vya sheria. Kwa kuwa mauaji yamefanywa na wananchi wa eneo hilo tunamshikilia mwenyekiti ili asaidie polisi kuwapata wahusika,” ameongeza.

Mwananchi
 
Sasa kama alishazingirwa na hakuwa na iwezekano wa kukimbia, wamemuua wa nini? Inabidi mwenyekiti awataje wananchi wake waliofanya hayo mauaji.

Anyway, Tubuni na mkamilishe bwawa la Nyerere kama redemption
 
Mwanaume anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 18 hadi 22 ameuawa na mwili wake kuchomwa moto na wananchi wakidai kuwa alijaribu kutaka kumbaka mwanafunzi wa kidato cha pili katika Sekondari iliyopo Kata ya Bombambili mjini Geita.

Tukio hilo limetokea leo Alhamisi Februari 24, 2022 saa 12.30 asubuhi wakati mwanafunzi huyo akiwa njiani kwenda shule.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Henry Mwaibambe amethibitisha kutokea tukio hilo na kueleza kuwa mwanafunzi huyo alitoka nyumbani alfajiri kuwahi shuleni na akiwa njiani ndipo alipokamatwa na kijana huyo akimvutia kichakani kwa lengo la kumbaka.

“Alipomkamata mwanafunzi alipiga kelele na wananchi walikusanyika na kumzingira. Walianza kumuokoa mwanafunzi na kumpeleka shule kisha kumshambulia kijana huyo hadi kumuua na mwili wake kuchomwa moto,” amesema Kamanda Mwaibambe.

Kufuatia tukio hilo, Mwenyekiti wa mtaa huo Salum Maige anashikiliwa na Polisi kusaidia kufahamika kwa wote waliohusika kwenye mauji hayo.

“Marehemu alishazingirwa hatuoni sababu za kumuua zaidi ya kumfikisha kwenye vyombo vya sheria. Kwa kuwa mauaji yamefanywa na wananchi wa eneo hilo tunamshikilia mwenyekiti ili asaidie polisi kuwapata wahusika,” ameongeza.




Mwananchi
Hawa polisi wetu liniwataanza kutumia akili na sio mabavu kwenye utendaji wao?why wamshikilie Chairman kama hawajamlink na crime scene?tuelewe Kuna Ile sheria ya kumshikilia suspect only for 48hrs na baada ya hapo ni mahakamani au aachiwe, police walitakiwa ndio wapeleleze na sio kumtwisha mzigo huu chairman.Nikiupata urais wa 24 hrs wizara hii nitaiweka Sawa within 4hrs ikiwa ni pamoja na kuivunja na kutengeneza wizara mbili,police na home affairs, na uajiri mpya kwa all homicide detectives na training zao ndani ya Botswana na equipments zote from US.
 
Back
Top Bottom