Una uhakika mwaka 2025 mazingira na mambo mengine yatakuwa sawasawa na mwaka 2015?
CCM ya 1977, ndo ile ile ya 1984, ndo ile ile ya 1994, ndo ile ile ya 2012, na ndo hiyo hiyo ya 2025!!

Hivi kwa mawazo yenu, mnaamini kabisa hao akina Ndugai wana ubavu wa kufurukuta mbele ya akina JK, Kinana, akina Mzee Makamba, Pius Msekwa, akina Mzee Pius Mangula, akina Mzee Karume, and the like?!!

Ukisikia CCM ina wenyewe, hao ndo wenye CCM yao na sio akina Dotto au akina Kabudi!!!

Hata huyo Kassim Majaliwa hayumo kwenye kundi la "wenye CCM yao"

Hakuna hata mmoja miongoni mwao mwenye sauti mbele ya Baraza la Usalama wa Taifa!!

Hebu chukua timu mzima ya akina Ndugai kisha ipimie na Timu ya akina Lowassa!!

Hao akina Ndugai wakitaka wawe na huo ubavu basi waishike TISS... sasa sijui wataanzia wapi!! NI nani miongoni mwao mwenye ubavu wa kuishika TISS?!

TISS yenyewe inaripoti kwa SSH! Na asikudanganye mtu.. President nchi hii ndo kila kitu!!!

Juzi hapa niliwapa mfano wa Magu!! Magu aliyeonekana mshamba fulani hivi mchunga ng'ombe wa Kisukuma ambae hata accent yake inaboa!!

Pamoja na yote hayo, bado aliweza kumzima Membe aliyekulia TISS!! Aliweza kumzima Membe ambae anaweza kukaa siti moja na "Wenye CCM Yao" na wakapiga stori na kugonga cheers kama zote but still, aliyeonekana "Mshamba mmoja hivi wa Kisukuma" akamzima Membe!!

Huyo ndo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambae pia ndie Mwenyekiti wa Chama ambae watu wanaota eti wanaweza kumtoa kirahisi rahisi tu!! Wa kumtoa wenyewe ni akina nani? "Eti akina Ndugai..."
 
Waswahili wanasema ukiishi nyumba ya vioo usitake ugomvi wa mawe. Kwa kua umetangaza waziwazi na mapema vita na unaowatuhumu kutaka uraisi 2025 sasa kaa mguu sawa. Wenzio hua wanapigana kimya kimya sasa wewe ugomvi wa chumbani umeuleta sebuleni. Jiandae kupigwa vita nje nje na waziwazi kama ulivyoanza mwenyewe. Hili goma umelipiga mapema mnoooo.
Umevurugwa, pole sana! Utasubiri sana!
 
Ndugai and the company wana - muscles za kumtunishia m/kiti ccm!!!? Kweli!!?
Mi najua kwa hakika, kwa katiba iliyopo labda samia afe (God have mercy) lakn vinginevyo, atakuwa rais hadi 2030.
Ahsante kwa kuliona hilo, na ni mjinga asiyezijua siasa za Tanzania tu ndie anaweza kukupinga!
 
Yaani ukitaka kuona uchanga wa mtu kwenye siasa za Tanzania basi msikilize anaongea nini kuhusu Samia na 2025!!

Guys, moja ya sababu ambazo ma-CCM huwa wanatupiga sana bao ni namna wanavyo-handle mambo yao!!!

Huku nje unaweza kuona huko CCM kuna mtimbwalanyiko kweli kweli lakini haya majamaa yakishakutana tu Chimwaga, yanakuwa kitu kimoja!!

Hizi simulizi za CCM kuparaganyika, CCM kufa kibudu zilienea sana wakati wa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa CCM mwaka 2012!!!

Tena wakati ule kulikuwa na vigogo kweli kweli waliokuwa wanaonekana ndo wanaenda kuichinja CCM... hawa ni pamoja na Lowassa, Chenge, na Rostam Azizi!!

Kuna wengine wakafikia hadi kusema JK anapigwa chini uenyekiti... sie wengine tukawa tunacheka tu!!!

Pamoja na rabsha zote hizo, wafuatiliaji wa siasa watakumbuka kilitokea nini!!

The Main Villain Himself, Edward Ngoyai Lowassa wakaja kumchinja na kumzika kabisa 2015!!!

Hayo ndo ma-CCM!!

Hivi mwaka huu CCM si wanafanya Uchaguzi wake mkuu?!

Subirini basi kama hamajasikia Samia huyo huyo akichaguliwa tena uenyekiti kwa 100%!!
Ccm ni chama dola kweli kweli.... mwenyekiti wa chama ambaye pia ni Rais ndiye mwenye kauli ya mwisho.
 
Waswahili wanasema ukiishi nyumba ya vioo usitake ugomvi wa mawe. Kwa kua umetangaza waziwazi na mapema vita na unaowatuhumu kutaka uraisi 2025 sasa kaa mguu sawa. Wenzio hua wanapigana kimya kimya sasa wewe ugomvi wa chumbani umeuleta sebuleni. Jiandae kupigwa vita nje nje na waziwazi kama ulivyoanza mwenyewe. Hili goma umelipiga mapema mnoooo.
2025
Ni
Mbali
Sana
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom