GAZETI LA UHURU; 8 Dec 2010:Mbunge ahamasisha machinga kuchoma mali za halmashauri

AmaniKatoshi

Senior Member
Mar 31, 2009
158
14
WanaJF nimestushwa na habari iliyoandikwa na gazeti la UHURU toleo la leo jumatano tarehe 8 Dec, 2010. Nimeangalia magazeti mengine, hakuna hata moja lilioandika walichoandika GAZETI HILI LA SEREKALI. TAfadhali soma habari hii hapa chini

Mbunge ahamasisha machinga kuchoma mali za halmashauri

Wednesday, 08 December 2010 07:55 newsroom



* Pia, ataka viwanda, hoteli za wana-CCM zichomwe
* Ni iwapo CHADEMA itashindwa kiti cha umeya wa Jiji

NA PETER KATULANDA, MWANZA

MBUNGE wa Nyamagana kupitia CHADEMA, Ezekia Wenje, anadaiwa kuanza siasa chafu kwa kuhamasisha wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga wachome mali za Halmashauri ya Jiji la Mwanza kama chama hicho hakitatwaa kiti cha umeya. Wenje pia anadaiwa kuwahamasisha wafuasi wa CHADEMA kuchoma viwanda na hoteli za baadhi ya matajiri ambao ni wanachama wa CCM kama watakikosa kiti hicho. Alitoa maelekezo hayo juzi saa 11.00 jioni, wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Sahara kata ya Pamba, wilayani Nyamagana. Akizungumza kwenye umati uliojitokeza kumsikiliza, alisema wananchi wasikubali maeneo yao yapimwe na maofisa ardhi wa jiji
watakaokwenda kupima kwa lengo la kuwalipa fidia ili wauze viwanja hivyo, wachome moto magari yao .​


ìTunasikia maofisa wa Jiji wanataka kuja kupima viwanja katika baadhi ya maeneo kwa lengo la kuwaondoa na kuwauzia matajiri, msikubaliane nao na waambieni waondoke, wakiwabishia basi mchome magari yao kuonyesha kuwa hamkubaliani nao kupora ardhi yenu,î alisema. Alidai kwamba baadhi ya wana-CCM wanawashawishi madiwani wa CHADEMA wamchague Meya wa Jiji kutoka CCM, hivyo wananchi wasikubaliane na matokeo yatakayotangazwa Desemba 17, mwaka huu, iwapo Meya hatatoka CHADEMA.

Tumewaeleza madiwani wetu kuwa siku hiyo tutapiga kura za wazi kumchagua Meya wa Jiji la Mwanza, atakayetusaliti tunaanza naye kisha tunawafuata matajiri wa CCM na kutatahakikisha mali zao tunaziharibu au kuzichoma ili wajue hatuko tayari kuibiwa,î alisisitiza Wenje.​


Aliwataka wafanyabiashara ndogo ndogo waendelee kufanya biashara zao popote bila kubugudhiwa na mgambo wa jiji. Wenje pia alikaririwa akiwaonya walimu wa sekondari na shule za msingi kutowatoza wanafunzi michango yoyote, huku akisema anamshukuru mfanyabiashara mmoja mzalendo kutoka Dar es Salaam kwa alichodai kumsaidia kuwa mbunge. Kutokana na kauli hizo, baadhi ya wananchi akiwemo Jumanne Magembe na wengine ambao hawakutaka kutajwa majina yao waliponda kauli za Mbunge huyo na kudai kwamba ni uchochezi wa kisiasa ambao utasababisha uvunjifu wa amani hapa.​

ìHuu ni uchochezi na siasa chafu, Wenje amezungumza maneno ya uchochezi anapaswa kukemewa na mamlaka husika kabla mambo hayajawa kama Kenya na kusababisha machafuko kwa manufaa ya wanasiasa wasiokuwa na uchungu na damu ya Watanzania,î alisema Magembe. ìNyie waandishi, hayo ndiyo maneno ya kuja kuwaeleza wananchi kama si kuleta uchochezi?" alihoji mkazi mwingine na kuongeza: "Hii ni hatari kwa wananchi na wafuasi wa vyama vya siasa, jiji lina sheria zake na pia kila jambo lina utaratibu wake wa kisheria."​

Mbunge ahamasisha machinga kuchoma mali za halmashauri

My take:

Linganisha habari hii na habari iliyoandikwa na gazeti la majira la leo www.majira.co.tz

Pia najiuliza kama ni kweli amesema hayo ni maneno ya uchochezi na ya kuvunja sheria. Sasa kama polisi walikuwepo mkutanoni hapo si wangemkamata?

Pia, ingewezekana hadi leo vyombo vingine vya habari au serekali isingetoa tamko?

Pia kwa nini hawajamquote Wenje na kuandika maneneo aliyotamka bila kuchakachua?

Huyu Jumanne Maghembe ndie waziri wa serekali yetu?

KAMA NI KWELI WENJE AHOJIWE NA KUCHUKULIWA HATUA< KAMA SIO KWELI >CHADEMA LAZIMA WAJIPANGE NA KUMUWAJIBISHA MWANDISHI HUYU NA GAZETI HILI LA UHURU ILI IWE FUNDISHO
 
WanaJF nimestushwa na habari iliyoandikwa na gazeti la UHURU toleo la leo jumatano tarehe 8 Dec, 2010. Nimeangalia magazeti mengine, hakuna hata moja lilioandika walichoandika GAZETI HILI LA SEREKALI. TAfadhali soma habari hii hapa chini
mkuu hili ni gazeti la chama cha mapinduzi!
 
wanajf nimestushwa na habari iliyoandikwa na gazeti la uhuru toleo la leo jumatano tarehe 8 dec, 2010. Nimeangalia magazeti mengine, hakuna hata moja lilioandika walichoandika gazeti hili la serekali. Tafadhali soma habari hii hapa chini

mbunge ahamasisha machinga kuchoma mali za halmashauri

wednesday, 08 december 2010 07:55 newsroom



* pia, ataka viwanda, hoteli za wana-ccm zichomwe
* ni iwapo chadema itashindwa kiti cha umeya wa jiji

na peter katulanda, mwanza

mbunge wa nyamagana kupitia chadema, ezekia wenje, anadaiwa kuanza siasa chafu kwa kuhamasisha wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga wachome mali za halmashauri ya jiji la mwanza kama chama hicho hakitatwaa kiti cha umeya. wenje pia anadaiwa kuwahamasisha wafuasi wa chadema kuchoma viwanda na hoteli za baadhi ya matajiri ambao ni wanachama wa ccm kama watakikosa kiti hicho. Alitoa maelekezo hayo juzi saa 11.00 jioni, wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa sahara kata ya pamba, wilayani nyamagana. Akizungumza kwenye umati uliojitokeza kumsikiliza, alisema wananchi wasikubali maeneo yao yapimwe na maofisa ardhi wa jiji
watakaokwenda kupima kwa lengo la kuwalipa fidia ili wauze viwanja hivyo, wachome moto magari yao .​


ìtunasikia maofisa wa jiji wanataka kuja kupima viwanja katika baadhi ya maeneo kwa lengo la kuwaondoa na kuwauzia matajiri, msikubaliane nao na waambieni waondoke, wakiwabishia basi mchome magari yao kuonyesha kuwa hamkubaliani nao kupora ardhi yenu,î alisema. Alidai kwamba baadhi ya wana-ccm wanawashawishi madiwani wa chadema wamchague meya wa jiji kutoka ccm, hivyo wananchi wasikubaliane na matokeo yatakayotangazwa desemba 17, mwaka huu, iwapo meya hatatoka chadema.

tumewaeleza madiwani wetu kuwa siku hiyo tutapiga kura za wazi kumchagua meya wa jiji la mwanza, atakayetusaliti tunaanza naye kisha tunawafuata matajiri wa ccm na kutatahakikisha mali zao tunaziharibu au kuzichoma ili wajue hatuko tayari kuibiwa,î alisisitiza wenje.​


aliwataka wafanyabiashara ndogo ndogo waendelee kufanya biashara zao popote bila kubugudhiwa na mgambo wa jiji. Wenje pia alikaririwa akiwaonya walimu wa sekondari na shule za msingi kutowatoza wanafunzi michango yoyote, huku akisema anamshukuru mfanyabiashara mmoja mzalendo kutoka dar es salaam kwa alichodai kumsaidia kuwa mbunge. Kutokana na kauli hizo, baadhi ya wananchi akiwemo jumanne magembe na wengine ambao hawakutaka kutajwa majina yao waliponda kauli za mbunge huyo na kudai kwamba ni uchochezi wa kisiasa ambao utasababisha uvunjifu wa amani hapa.​

ìhuu ni uchochezi na siasa chafu, wenje amezungumza maneno ya uchochezi anapaswa kukemewa na mamlaka husika kabla mambo hayajawa kama kenya na kusababisha machafuko kwa manufaa ya wanasiasa wasiokuwa na uchungu na damu ya watanzania,î alisema magembe. ìnyie waandishi, hayo ndiyo maneno ya kuja kuwaeleza wananchi kama si kuleta uchochezi?" alihoji mkazi mwingine na kuongeza: "hii ni hatari kwa wananchi na wafuasi wa vyama vya siasa, jiji lina sheria zake na pia kila jambo lina utaratibu wake wa kisheria."​

mbunge ahamasisha machinga kuchoma mali za halmashauri

my take:

Linganisha habari hii na habari iliyoandikwa na gazeti la majira la leo www.majira.co.tz

pia najiuliza kama ni kweli amesema hayo ni maneno ya uchochezi na ya kuvunja sheria. Sasa kama polisi walikuwepo mkutanoni hapo si wangemkamata?

Pia, ingewezekana hadi leo vyombo vingine vya habari au serekali isingetoa tamko?

Pia kwa nini hawajamquote wenje na kuandika maneneo aliyotamka bila kuchakachua?

Huyu jumanne maghembe ndie waziri wa serekali yetu?

kama ni kweli wenje ahojiwe na kuchukuliwa hatua< kama sio kweli >chadema lazima wajipange na kumuwajibisha mwandishi huyu na gazeti hili la uhuru ili iwe fundisho
sahihisho tu; uhuru sio gazeti la serikali ni gazeti la chama cha mapinduzi
 
Samahanini nilisahau kuwa uhuru ni gazeti la CCM. LAkini tutafute uhalisia wa habari waliyoandika...ni hatari sanaaa
 
NA PETER KATULANDA, MWANZA[/COLOR]
Nimeona habari hii imeandikwa na mwadishi wake hapo juu, swali kwa wanaofahamu tafadhari, hivi huyu Peter Katulanda ndiye yule mwandishi anayeandikia na gazeti la Mwananchi akitumia jina la Frederick Katulanda?

mkuu hili ni gazeti la chama cha mapinduzi!
Kwa hakika habari ikiandikwa na UHURU, Mtanzania, Jambo Leo, mie sishangai kabisa hata kidogo maana kazi yake ni Propaganda. UHURU ni mali ya CCM lakini Mtanzania na Jambo leo ni mali ya makada wa CCM unategemea nini?
 
Naona bado inawauma sana ccm kukosa ubunge nyamagana
siyo Nyamagana tuu! unajua ukombozi wowote huanzia kwenye miji mikubwa na CHADEMA imechukua miji na majiji, lazima iwaume tena sana. lakini huwa nasema muda woote hii nchi haina sheria!?? kwanini magazeti kama haya hayachukuliwi hatua?
 
Wajameni, kampeni za LAURENCE MARSHA zimehamia kwenye magazeti!!! Anamtumia Zidhiwani na Makamba kuwashawishi waandishi wao wa habari wa CCM kuandika habari za uongo ili CDM ionekane inaharibu amani!! Hawana sera....
 
WanaJF nimestushwa na habari iliyoandikwa na gazeti la UHURU toleo la leo jumatano tarehe 8 Dec, 2010. Nimeangalia magazeti mengine, hakuna hata moja lilioandika walichoandika GAZETI HILI LA SEREKALI. TAfadhali soma habari hii hapa chini

Mbunge ahamasisha machinga kuchoma mali za halmashauri

Wednesday, 08 December 2010 07:55 newsroom



* Pia, ataka viwanda, hoteli za wana-CCM zichomwe
* Ni iwapo CHADEMA itashindwa kiti cha umeya wa Jiji

NA PETER KATULANDA, MWANZA

MBUNGE wa Nyamagana kupitia CHADEMA, Ezekia Wenje, anadaiwa kuanza siasa chafu kwa kuhamasisha wafanyabiashara wadogo maarufu kama machinga wachome mali za Halmashauri ya Jiji la Mwanza kama chama hicho hakitatwaa kiti cha umeya. Wenje pia anadaiwa kuwahamasisha wafuasi wa CHADEMA kuchoma viwanda na hoteli za baadhi ya matajiri ambao ni wanachama wa CCM kama watakikosa kiti hicho. Alitoa maelekezo hayo juzi saa 11.00 jioni, wakati akihutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa Sahara kata ya Pamba, wilayani Nyamagana. Akizungumza kwenye umati uliojitokeza kumsikiliza, alisema wananchi wasikubali maeneo yao yapimwe na maofisa ardhi wa jiji
watakaokwenda kupima kwa lengo la kuwalipa fidia ili wauze viwanja hivyo, wachome moto magari yao .​


ìTunasikia maofisa wa Jiji wanataka kuja kupima viwanja katika baadhi ya maeneo kwa lengo la kuwaondoa na kuwauzia matajiri, msikubaliane nao na waambieni waondoke, wakiwabishia basi mchome magari yao kuonyesha kuwa hamkubaliani nao kupora ardhi yenu,î alisema. Alidai kwamba baadhi ya wana-CCM wanawashawishi madiwani wa CHADEMA wamchague Meya wa Jiji kutoka CCM, hivyo wananchi wasikubaliane na matokeo yatakayotangazwa Desemba 17, mwaka huu, iwapo Meya hatatoka CHADEMA.

Tumewaeleza madiwani wetu kuwa siku hiyo tutapiga kura za wazi kumchagua Meya wa Jiji la Mwanza, atakayetusaliti tunaanza naye kisha tunawafuata matajiri wa CCM na kutatahakikisha mali zao tunaziharibu au kuzichoma ili wajue hatuko tayari kuibiwa,î alisisitiza Wenje.​


Aliwataka wafanyabiashara ndogo ndogo waendelee kufanya biashara zao popote bila kubugudhiwa na mgambo wa jiji. Wenje pia alikaririwa akiwaonya walimu wa sekondari na shule za msingi kutowatoza wanafunzi michango yoyote, huku akisema anamshukuru mfanyabiashara mmoja mzalendo kutoka Dar es Salaam kwa alichodai kumsaidia kuwa mbunge. Kutokana na kauli hizo, baadhi ya wananchi akiwemo Jumanne Magembe na wengine ambao hawakutaka kutajwa majina yao waliponda kauli za Mbunge huyo na kudai kwamba ni uchochezi wa kisiasa ambao utasababisha uvunjifu wa amani hapa.​

ìHuu ni uchochezi na siasa chafu, Wenje amezungumza maneno ya uchochezi anapaswa kukemewa na mamlaka husika kabla mambo hayajawa kama Kenya na kusababisha machafuko kwa manufaa ya wanasiasa wasiokuwa na uchungu na damu ya Watanzania,î alisema Magembe. ìNyie waandishi, hayo ndiyo maneno ya kuja kuwaeleza wananchi kama si kuleta uchochezi?" alihoji mkazi mwingine na kuongeza: "Hii ni hatari kwa wananchi na wafuasi wa vyama vya siasa, jiji lina sheria zake na pia kila jambo lina utaratibu wake wa kisheria."​

Mbunge ahamasisha machinga kuchoma mali za halmashauri

My take:

Linganisha habari hii na habari iliyoandikwa na gazeti la majira la leo www.majira.co.tz

Pia najiuliza kama ni kweli amesema hayo ni maneno ya uchochezi na ya kuvunja sheria. Sasa kama polisi walikuwepo mkutanoni hapo si wangemkamata?

Pia, ingewezekana hadi leo vyombo vingine vya habari au serekali isingetoa tamko?

Pia kwa nini hawajamquote Wenje na kuandika maneneo aliyotamka bila kuchakachua?

Huyu Jumanne Maghembe ndie waziri wa serekali yetu?

KAMA NI KWELI WENJE AHOJIWE NA KUCHUKULIWA HATUA< KAMA SIO KWELI >CHADEMA LAZIMA WAJIPANGE NA KUMUWAJIBISHA MWANDISHI HUYU NA GAZETI HILI LA UHURU ILI IWE FUNDISHO


MWANDISHI MAKINI WA MAJIRA AMERIPOTI HIVI:-
Wenje achangiwa samani za ofisi
*Ni baada ya Masha kudaiwa kuzihamisha
*Zitto apuunza madai mgawanyiko Chadema

Na Wilhelm Mulinda, Mwanza

WANANCHI wa Jimbo la Nyamagana mkoani Mwanza juzi walichanga sh 179, 690 kwa ajili ya kununua samani za Ofisi ya Mbunge wa
Jimbo hilo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Ezekia Wenje.Fedha hizo zilichangwa wakati mbunge huyo alipokuwa akihutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Sahara jijini hapa kwa lengo la kuwashukuru wananchi kwa kumchagua.

Wananchi hao waliamua kuchanga fedha hizo baada ya mbunge huyo kueleza kuwa ofisi yake haina meza wala kiti na kwamba analazimika kuwahudumia wananchi akiwa amesimama kutokana na samani ambazo zikuwa katika ofisi hiyo kuchukuliwa na Mbunge wa zamani wa jimbo hilo, Bw. Lawrence Masha kwa madai kuwa alinunua samani hizo kwa fedha zake.

Siku chache baada ya Bw. Masha kuachia madaraka hayo, iliyokuwa ofisi yake ilikuwa haina samani muhimu, ikiwamo picha ya Rais Jakaya Kikwete, simu ya mezani ilikatwa waya na kichwa chake kubebwa; vitasa, zulia, mafaili yenye nyaraka za maendeleo ya jimbo na mapazia.

Kutokana na hali hiyo, Bw. Wenje alikaririwa akisema: Niliwabana viongozi ngazi ya wilaya na mkoa wanieleze vimeenda wapi hivi vituâ&#8364;¦ niliambiwa eti vilinunuliwa na mtu binafsi na havikuwa vya serikali.Akihutubia mkutano huo juzi Bw. Wenje alisema kuwa Bw. Masha hakuwa na sababu ya kuchukua samani hizo kwa vile serikali kila mwaka ilikuwa ikitoa fedha kwa ajili ya kuendesha ofisi hiyo na kuhoji kwamba kama alinunua kwa fedha zake, zile za serikali zilienda wapi kwa kipindi cha miaka mitano.

Akiwashukuru wananchi, Bw. Wenje alisema kuwa yeye amekuwa mbunge kwa sababu wananchi walikubali kupigwa mabomu na hata kupoteza maisha yao siku ya kutangaza matokeo, na si kwa sababu alipigiwa kura nyingi au nchi ni ya demokrasia.

Aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika Ofisi ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza siku ya kuwachagua Meya na Naibu Meya wa Jiji hilo ili washangilie ushindi, kwa vile chama chao kina wajumbe wengi wa kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi huo ambao wanakihakikishia ushindi wa kutwaa viti hivyo na kuongoza halmashauri hiyo.

"Sisi tuna wajumbe 17 ukiweka na diwani mmoja wa Chama cha Civic United Front (CUF) tunakuwa jumla 18 wakati Chama cha Mapinduzi (CCM) kina wajumbe 13 pekee, hivyo hatuna sababu ya kushindwa kupata kiti cha umeya na naibu meya," alisema Bw. Wenje.

Bw. Wenje alisema kuwa endapo Halmashauri ya Jiji la Mwanza itahitaji kuwaondoa wamachinga katika maeneo wanayofanyia biashara, inatakiwa kufanya nao mazungumzo badala ya kuwaondoa kwa nguvu, hali ambayo inaweza kusababisha kero kwa wafanyabiashara hao na wananchi wengine kwa ujumla.Alisema kuwa yeye amechaguliwa na maskini, hivyo ni lazima asimame mstari wa mbele kuwatetea wanyonge ambao ndio wapiga kura wake, ili wafanye shughuli zao za kujiletea maendeleo pamoja na familia zao bila usumbufu wowote.....

Sasa ukiangalia tu hapo unagundua kwamba huyo wa UHURU anawatumikia mabwana zake, anaendeleza mapambano dhidi ya CDM na anataka kuchochea amani jimboni hapo. CCM ni mufilisi wa siasa..
 
Hizi ni habari za uchochezi aliyetoa hizi habari athibitishe la sivyo akamatwe na ashitakiwe kwa uchochezi
 
Na wewe nawe umekosa ya kusoma hadi usome uhuru, huo mda si bora ungeutumia kukaa na mpenzi wako mkarelax kidogo!
 
Back
Top Bottom