MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,172
- 23,974
INTELLIGENCE UNIT ni sehemu ya kitengo ndani ya Gazeti la The Economist ambacho hufanya uchunguzi na utafiti wa kisiasa na kiuchumi kwa nchi mbali mbali duniani na kutoa matokeo au matarajio.
Kitengo hiki cha kiuchunguzi kina wafanyakazi wabobezi zaidi ya 100 duniani ambao hutoa tafiti na utabiri baada ya uchunguzi kuhusu masuala ya kiuchumi kwa nchi mbali mbali kila mwanzo wa mwaka kulingana na mazingira halisi.
Ikumbukwe kuwa gazeti la The Economist limekuwa mwiba mkali hasa kwa Rais Magufuli kwa sababu linaamini sera za kisiasa na kiuchumi za Rais Magufuli zinaenda kinyume na mtazamo/msimamo wa kisiasa na kiuchumi wa gazeti hili.
Kwenye suala la kiuchumi, The Economist linaamini katika Ubinafsishaji na kuachia uchumi huru bila ya serikali kuingilia kati. Kwenye suala la kijamii, The Economist linaamini katika ndoa za jinsia moja na kuhalalisha utumiaji wa baadhi ya madawa ya kulevya kama bangi.
Ukitaka kujua msimamo wa Gazeti la The Economist kuhusu masuala ya kisiasa na kiuchumi;
GONGA LINK HII>>>Is The Economist Left or Right Wing
Hata hivyo linapofika suala la uchambuzi na utafiti, gazeti la The Economist hutoa matokeo ya tafiti na utabiri kama ambavyo jopo la wachunguzi wake limeona na kufikia hitimisho.
Kwenye masuala ya kisiasa nchini, jopo la wachunguzi wa INTELLIGENCE UNIT limesema baada ya Uchaguzi Mkuu, Rais Magufuli na CCM wataendelea sio kutawala tu bali pia watahodhi kwa kiwango kikubwa madaraka ya nchi. Kutakuwa na utulivu wa kisiasa kuanzia 2020-2023 huku CCM ikiendelea kujiimarisha zaidi kutokana na udhaifu na kudhoofika kwa vyama vya upinzani.
Kwenye masuala ya kiuchumi limesema pamoja na kwamba serikali ya Rais Magufuli imeonesha mipango na nia ya kuboresha uwajibikaji katika sekta za umma na kuboresha maisha ya wananchi lakini itakabiliwa na uwezo mdogo kifedha.
INTELLIGENCE UNIT imebainisha kuwa, kutokuwa na utungaji sera ulioeleweka nchini kutawafanya wawekezaji kuogopa kuwekeza nchini, hata hivyo matarajio kwa nusu ya mwaka yanaonekana kuwa imara kutokana na kukua kwa sekta ya utoaji huduma nchini na uwekezaji kwenye miundombinu kitaifa.
Ukitaka kusoma repoti yote;
GONGA LINK HII>>>ENTELLIGENCE UNIT: Tanzania political and economic forecast
Kitengo hiki cha kiuchunguzi kina wafanyakazi wabobezi zaidi ya 100 duniani ambao hutoa tafiti na utabiri baada ya uchunguzi kuhusu masuala ya kiuchumi kwa nchi mbali mbali kila mwanzo wa mwaka kulingana na mazingira halisi.
Ikumbukwe kuwa gazeti la The Economist limekuwa mwiba mkali hasa kwa Rais Magufuli kwa sababu linaamini sera za kisiasa na kiuchumi za Rais Magufuli zinaenda kinyume na mtazamo/msimamo wa kisiasa na kiuchumi wa gazeti hili.
Kwenye suala la kiuchumi, The Economist linaamini katika Ubinafsishaji na kuachia uchumi huru bila ya serikali kuingilia kati. Kwenye suala la kijamii, The Economist linaamini katika ndoa za jinsia moja na kuhalalisha utumiaji wa baadhi ya madawa ya kulevya kama bangi.
Ukitaka kujua msimamo wa Gazeti la The Economist kuhusu masuala ya kisiasa na kiuchumi;
GONGA LINK HII>>>Is The Economist Left or Right Wing
Hata hivyo linapofika suala la uchambuzi na utafiti, gazeti la The Economist hutoa matokeo ya tafiti na utabiri kama ambavyo jopo la wachunguzi wake limeona na kufikia hitimisho.
Kwenye masuala ya kisiasa nchini, jopo la wachunguzi wa INTELLIGENCE UNIT limesema baada ya Uchaguzi Mkuu, Rais Magufuli na CCM wataendelea sio kutawala tu bali pia watahodhi kwa kiwango kikubwa madaraka ya nchi. Kutakuwa na utulivu wa kisiasa kuanzia 2020-2023 huku CCM ikiendelea kujiimarisha zaidi kutokana na udhaifu na kudhoofika kwa vyama vya upinzani.
Kwenye masuala ya kiuchumi limesema pamoja na kwamba serikali ya Rais Magufuli imeonesha mipango na nia ya kuboresha uwajibikaji katika sekta za umma na kuboresha maisha ya wananchi lakini itakabiliwa na uwezo mdogo kifedha.
INTELLIGENCE UNIT imebainisha kuwa, kutokuwa na utungaji sera ulioeleweka nchini kutawafanya wawekezaji kuogopa kuwekeza nchini, hata hivyo matarajio kwa nusu ya mwaka yanaonekana kuwa imara kutokana na kukua kwa sekta ya utoaji huduma nchini na uwekezaji kwenye miundombinu kitaifa.
Ukitaka kusoma repoti yote;
GONGA LINK HII>>>ENTELLIGENCE UNIT: Tanzania political and economic forecast