Gazeti la The Economist la nchini Uingereza, lamchafua Rais Magufuli

Kakke

JF-Expert Member
Dec 4, 2010
1,883
1,482
Gazeti la The Economist la nchini Uingereza, limeandika makala kuhusu utawala wa Rais JPM likimtaja kama dikteta hatari anayebukia barani Afrika, asiyejali utu, kiongozi asiye na dira (dystopian), na anayesikia fahari kutimiza matakwa yake kwa kuumiza wengine (rogue leader). Gazeti hilo maarufu duniani, hasa katika nchi za Ulaya limetumia vielelezo vya matukio ya watu kupotea, viongozi wa kisiasa kufungwa na kupigwa risasi hadharani, kuminywa kwa uhuru wa vyombo vya habari, watu kuuawa na kutupwa baharini, kama hoja za kukosoa utawala wa JPM.

Sehemu ya makala hiyo inaeleza "Magufuli had banned all political rallies, MPs are allowed to campaign only in their own constituencies (and several have been arrested), Several newspapers have been temporarily closed by the government. A journalist and opposition party members have disappeared, and mutilated bodies have washed up on the shores of Coco Beach in Dar es Salaam, the commercial capital. In September last year Tundu Lissu, a prominent opposition MP, was shot and injured outside his house in Dodoma"

"Dozen police officers have been killed in Kibiti, a coastal town about 70km south of Dar es Salaam. Yet little news leaks out from the region. Foreign journalists are turned back long before they reach Kibiti; a Tanzanian journalist investigating the killings has been missing for three months."

Kwa tafsiri isiyo rasmi gazeti hilo linasema "Magufuli amezuia shughuli za kisiasa kwa vyama vya upinzani (huku chama chake kikiendelea kufanya siasa), wabunge wa upinzani hawaruhusiwi kufanya mikutano nje ya majimbo yao, na baadhi yao wamekamatwa na kufungwa. Magazeti (yanayoikosoa serikali) yamefungiwa, mwandishi mmoja na baadhi ya wanasiasa wamepotea, huku miili ya watu waliouawa ikiokotwa baharini hasa ufukwe wa Coco. Mwezi September mwaka jana Tundu Lissu, mmoja wa wanasiasa wenye nguvu nchini Tanzania alipigwa risasi nje ya nyumba yake mjini Dodoma.

Gazeti hilo limeongeza "Askari Polisi wengi wameuawa mjini Kibiti, lakini hakuna taarifa za kutosha juu ya matukio hayo zilizowekwa wazi. Waandishi wa kigeni waliojaribu kuchunguza matukio hayo wamekuwa wakizuiwa na serikali kufika Kibiti, huku mwandishi wa Tanzania aliyekuwa akifuatilia sakata hilo (Azory Gwanda) akipotea kwa zaidi ya miezi mitatu sasa."

Gazeti hilo limefanya mahojiano na mbunge mmoja wa CCM ambaye amesema ni watu wachache sana ndani ya chama hicho wenye uthubutu wa kumkosoa Rais Magufuli. Wengi wanamuogopa na kumnyeyekea. Mbunge huyo amesema ni watu wachache wenye uthubutu wa kumkosoa Rais Magufuli waziwazi. Wengi wao hata kama wanaona amekosea watamkosoa pembeni lakini kwenye hadhara watamsifia.

Gazeti hilo limeeleza kuwa udhaifu wa Katiba ya nchi ndio unampa mwanya Rais Magufuli kuwa dikteta. Limemnukuu Mwalimu Nyerere aliposema Katiba inampa mdaraka makubwa anayoweza kuyatumia kuwa dikteta. "Katiba ya Tanzania inahitaji kufanyiwa marekebisho ili kumpunguzia Rais madaraka kwa sababu Magufuli anayatumia vibaya" limeongeza.

"Tanzania’s politics have never been truly open, but what is different now is that even CCM, which is by far the country’s most stable institution, is cowed" likimaanisha kwamba Siasa za Tanzania hazijawahi kuwa huru lakini ni jambo la ajabu kwamba hata CCM ambayo inaonekana kuwa taasisi imara inamuogopa Magufuli. (Hili ni jambo la hatari mtu mmoja kuogopwa na taasisi).

Baadhi ya watanzania wamekuwa na maoni tofauti kuhusu makala hiyo. Mwandishi na mchambuzi wa masuala ya siasa Yericko Nyerere amesema gazeti hilo limemdhalilisha "Rais wetu mpendwa" kwenye wigo wa kimataifa. Yericko ameshangazwa na ukimya wa UVCCM kutokusema jambo lolote hadi sasa. Amesema huenda kwa kuwa makala hiyo imeandikwa kwa kiingereza pengine ndio sababu ya ukimya wao. Amewataka kutafuta mkalimani wa kutafsiri ili kama taifa tuungane kukemea Rais wetu kudhalilishwa. Amesema makala hiyo ingeandikwa kwa Kiswahili UVCCM pamoja na msemaji wa chama hicho (aliyepoteza umaarufu) Bw.Humphrey Poepole wangekuwa wameshajibu.
 
Gazeti la The Economist la nchini Uingereza, limeandika makala kuhusu utawala wa Rais JPM likimtaja kama dikteta hatari anayebukia barani Afrika, asiyejali utu, kiongozi asiye na dira (dystopian), na anayesikia fahari kutimiza matakwa yake kwa kuumiza wengine (rogue leader). Gazeti hilo maarufu duniani, hasa katika nchi za Ulaya limetumia vielelezo vya matukio ya watu kupotea, viongozi wa kisiasa kufungwa na kupigwa risasi hadharani, kuminywa kwa uhuru wa vyombo vya habari, watu kuuawa na kutupwa baharini, kama hoja za kukosoa utawala wa JPM.

Sehemu ya makala hiyo inaeleza "Magufuli had banned all political rallies, MPs are allowed to campaign only in their own constituencies (and several have been arrested), Several newspapers have been temporarily closed by the government. A journalist and opposition party members have disappeared, and mutilated bodies have washed up on the shores of Coco Beach in Dar es Salaam, the commercial capital. In September last year Tundu Lissu, a prominent opposition MP, was shot and injured outside his house in Dodoma"

"Dozen police officers have been killed in Kibiti, a coastal town about 70km south of Dar es Salaam. Yet little news leaks out from the region. Foreign journalists are turned back long before they reach Kibiti; a Tanzanian journalist investigating the killings has been missing for three months."

Kwa tafsiri isiyo rasmi gazeti hilo linasema "Magufuli amezuia shughuli za kisiasa kwa vyama vya upinzani (huku chama chake kikiendelea kufanya siasa), wabunge wa upinzani hawaruhusiwi kufanya mikutano nje ya majimbo yao, na baadhi yao wamekamatwa na kufungwa. Magazeti (yanayoikosoa serikali) yamefungiwa, mwandishi mmoja na baadhi ya wanasiasa wamepotea, huku miili ya watu waliouawa ikiokotwa baharini hasa ufukwe wa Coco. Mwezi September mwaka jana Tundu Lissu, mmoja wa wanasiasa wenye nguvu nchini Tanzania alipigwa risasi nje ya nyumba yake mjini Dodoma.

Gazeti hilo limeongeza "Askari Polisi wengi wameuawa mjini Kibiti, lakini hakuna taarifa za kutosha juu ya matukio hayo zilizowekwa wazi. Waandishi wa kigeni waliojaribu kuchunguza matukio hayo wamekuwa wakizuiwa na serikali kufika Kibiti, huku mwandishi wa Tanzania aliyekuwa akifuatilia sakata hilo (Azory Gwanda) akipotea kwa zaidi ya miezi mitatu sasa."

Gazeti hilo limefanya mahojiano na mbunge mmoja wa CCM ambaye amesema ni watu wachache sana ndani ya chama hicho wenye uthubutu wa kumkosoa Rais Magufuli. Wengi wanamuogopa na kumnyeyekea. Mbunge huyo amesema ni watu wachache wenye uthubutu wa kumkosoa Rais Magufuli waziwazi. Wengi wao hata kama wanaona amekosea watamkosoa pembeni lakini kwenye hadhara watamsifia.

Gazeti hilo limeeleza kuwa udhaifu wa Katiba ya nchi ndio unampa mwanya Rais Magufuli kuwa dikteta. Limemnukuu Mwalimu Nyerere aliposema Katiba inampa mdaraka makubwa anayoweza kuyatumia kuwa dikteta. "Katiba ya Tanzania inahitaji kufanyiwa marekebisho ili kumpunguzia Rais madaraka kwa sababu Magufuli anayatumia vibaya" limeongeza.

"Tanzania’s politics have never been truly open, but what is different now is that even CCM, which is by far the country’s most stable institution, is cowed" likimaanisha kwamba Siasa za Tanzania hazijawahi kuwa huru lakini ni jambo la ajabu kwamba hata CCM ambayo inaonekana kuwa taasisi imara inamuogopa Magufuli. (Hili ni jambo la hatari mtu mmoja kuogopwa na taasisi).

Baadhi ya watanzania wamekuwa na maoni tofauti kuhusu makala hiyo. Mwandishi na mchambuzi wa masuala ya siasa Yericko Nyerere amesema gazeti hilo limemdhalilisha "Rais wetu mpendwa" kwenye wigo wa kimataifa. Yericko ameshangazwa na ukimya wa UVCCM kutokusema jambo lolote hadi sasa. Amesema huenda kwa kuwa makala hiyo imeandikwa kwa kiingereza pengine ndio sababu ya ukimya wao. Amewataka kutafuta mkalimani wa kutafsiri ili kama taifa tuungane kukemea Rais wetu kudhalilishwa. Amesema makala hiyo ingeandikwa kwa Kiswahili UVCCM pamoja na msemaji wa chama hicho (aliyepoteza umaarufu) Bw.Humphrey Poepole wangekuwa wameshajibu.
Tupe picha ya hilo gazeti lenye maandishi ya kumchafua JPM!
 
Kusema "dictator hatari anayeibuka afrika' hii ndo inaogofya, ni hatari kwa watanzania!
Hivi ni kweli ccm kama taasisi imara imefyata mkia kwa JPM??
mwenye uhakika na hili anijuzee
Anipe na mfano wa mkongwe ndani ya ccm mwenye uwezo wa kumuonya jpm hadharani bila kupepepesa macho!
 
sio kweli Lissu alikua shot outside his house,nakumbuka alipigwa kwenye viwanja vya bunge au nimekosea..?? wameweka chumvi
 
Gazeti la The Economist la nchini Uingereza, limeandika makala kuhusu utawala wa Rais JPM likimtaja kama dikteta hatari anayebukia barani Afrika, asiyejali utu, kiongozi asiye na dira (dystopian), na anayesikia fahari kutimiza matakwa yake kwa kuumiza wengine (rogue leader). Gazeti hilo maarufu duniani, hasa katika nchi za Ulaya limetumia vielelezo vya matukio ya watu kupotea, viongozi wa kisiasa kufungwa na kupigwa risasi hadharani, kuminywa kwa uhuru wa vyombo vya habari, watu kuuawa na kutupwa baharini, kama hoja za kukosoa utawala wa JPM.

Sehemu ya makala hiyo inaeleza "Magufuli had banned all political rallies, MPs are allowed to campaign only in their own constituencies (and several have been arrested), Several newspapers have been temporarily closed by the government. A journalist and opposition party members have disappeared, and mutilated bodies have washed up on the shores of Coco Beach in Dar es Salaam, the commercial capital. In September last year Tundu Lissu, a prominent opposition MP, was shot and injured outside his house in Dodoma"

"Dozen police officers have been killed in Kibiti, a coastal town about 70km south of Dar es Salaam. Yet little news leaks out from the region. Foreign journalists are turned back long before they reach Kibiti; a Tanzanian journalist investigating the killings has been missing for three months."

Kwa tafsiri isiyo rasmi gazeti hilo linasema "Magufuli amezuia shughuli za kisiasa kwa vyama vya upinzani (huku chama chake kikiendelea kufanya siasa), wabunge wa upinzani hawaruhusiwi kufanya mikutano nje ya majimbo yao, na baadhi yao wamekamatwa na kufungwa. Magazeti (yanayoikosoa serikali) yamefungiwa, mwandishi mmoja na baadhi ya wanasiasa wamepotea, huku miili ya watu waliouawa ikiokotwa baharini hasa ufukwe wa Coco. Mwezi September mwaka jana Tundu Lissu, mmoja wa wanasiasa wenye nguvu nchini Tanzania alipigwa risasi nje ya nyumba yake mjini Dodoma.

Gazeti hilo limeongeza "Askari Polisi wengi wameuawa mjini Kibiti, lakini hakuna taarifa za kutosha juu ya matukio hayo zilizowekwa wazi. Waandishi wa kigeni waliojaribu kuchunguza matukio hayo wamekuwa wakizuiwa na serikali kufika Kibiti, huku mwandishi wa Tanzania aliyekuwa akifuatilia sakata hilo (Azory Gwanda) akipotea kwa zaidi ya miezi mitatu sasa."

Gazeti hilo limefanya mahojiano na mbunge mmoja wa CCM ambaye amesema ni watu wachache sana ndani ya chama hicho wenye uthubutu wa kumkosoa Rais Magufuli. Wengi wanamuogopa na kumnyeyekea. Mbunge huyo amesema ni watu wachache wenye uthubutu wa kumkosoa Rais Magufuli waziwazi. Wengi wao hata kama wanaona amekosea watamkosoa pembeni lakini kwenye hadhara watamsifia.

Gazeti hilo limeeleza kuwa udhaifu wa Katiba ya nchi ndio unampa mwanya Rais Magufuli kuwa dikteta. Limemnukuu Mwalimu Nyerere aliposema Katiba inampa mdaraka makubwa anayoweza kuyatumia kuwa dikteta. "Katiba ya Tanzania inahitaji kufanyiwa marekebisho ili kumpunguzia Rais madaraka kwa sababu Magufuli anayatumia vibaya" limeongeza.

"Tanzania’s politics have never been truly open, but what is different now is that even CCM, which is by far the country’s most stable institution, is cowed" likimaanisha kwamba Siasa za Tanzania hazijawahi kuwa huru lakini ni jambo la ajabu kwamba hata CCM ambayo inaonekana kuwa taasisi imara inamuogopa Magufuli. (Hili ni jambo la hatari mtu mmoja kuogopwa na taasisi).

Baadhi ya watanzania wamekuwa na maoni tofauti kuhusu makala hiyo. Mwandishi na mchambuzi wa masuala ya siasa Yericko Nyerere amesema gazeti hilo limemdhalilisha "Rais wetu mpendwa" kwenye wigo wa kimataifa. Yericko ameshangazwa na ukimya wa UVCCM kutokusema jambo lolote hadi sasa. Amesema huenda kwa kuwa makala hiyo imeandikwa kwa kiingereza pengine ndio sababu ya ukimya wao. Amewataka kutafuta mkalimani wa kutafsiri ili kama taifa tuungane kukemea Rais wetu kudhalilishwa. Amesema makala hiyo ingeandikwa kwa Kiswahili UVCCM pamoja na msemaji wa chama hicho (aliyepoteza umaarufu) Bw.Humphrey Poepole wangekuwa wameshajibu.

Jamani Watanzania tuache ujuha! Economist watasema nini zuri kwa Magufuli wakati Acacia ndio wanafungasha? Watu mnakazana kukariri propaganda za Waingereza wakati wao wenyewe wanajadili madili ya gesi Hyatt! Pascal Mayalla unaitwa huku.
 
Gazeti la The Economist la nchini Uingereza, limeandika makala kuhusu utawala wa Rais JPM likimtaja kama dikteta hatari anayebukia barani Afrika, asiyejali utu, kiongozi asiye na dira (dystopian), na anayesikia fahari kutimiza matakwa yake kwa kuumiza wengine (rogue leader). Gazeti hilo maarufu duniani, hasa katika nchi za Ulaya limetumia vielelezo vya matukio ya watu kupotea, viongozi wa kisiasa kufungwa na kupigwa risasi hadharani, kuminywa kwa uhuru wa vyombo vya habari, watu kuuawa na kutupwa baharini, kama hoja za kukosoa utawala wa JPM.

Sehemu ya makala hiyo inaeleza "Magufuli had banned all political rallies, MPs are allowed to campaign only in their own constituencies (and several have been arrested), Several newspapers have been temporarily closed by the government. A journalist and opposition party members have disappeared, and mutilated bodies have washed up on the shores of Coco Beach in Dar es Salaam, the commercial capital. In September last year Tundu Lissu, a prominent opposition MP, was shot and injured outside his house in Dodoma"

"Dozen police officers have been killed in Kibiti, a coastal town about 70km south of Dar es Salaam. Yet little news leaks out from the region. Foreign journalists are turned back long before they reach Kibiti; a Tanzanian journalist investigating the killings has been missing for three months."

Kwa tafsiri isiyo rasmi gazeti hilo linasema "Magufuli amezuia shughuli za kisiasa kwa vyama vya upinzani (huku chama chake kikiendelea kufanya siasa), wabunge wa upinzani hawaruhusiwi kufanya mikutano nje ya majimbo yao, na baadhi yao wamekamatwa na kufungwa. Magazeti (yanayoikosoa serikali) yamefungiwa, mwandishi mmoja na baadhi ya wanasiasa wamepotea, huku miili ya watu waliouawa ikiokotwa baharini hasa ufukwe wa Coco. Mwezi September mwaka jana Tundu Lissu, mmoja wa wanasiasa wenye nguvu nchini Tanzania alipigwa risasi nje ya nyumba yake mjini Dodoma.

Gazeti hilo limeongeza "Askari Polisi wengi wameuawa mjini Kibiti, lakini hakuna taarifa za kutosha juu ya matukio hayo zilizowekwa wazi. Waandishi wa kigeni waliojaribu kuchunguza matukio hayo wamekuwa wakizuiwa na serikali kufika Kibiti, huku mwandishi wa Tanzania aliyekuwa akifuatilia sakata hilo (Azory Gwanda) akipotea kwa zaidi ya miezi mitatu sasa."

Gazeti hilo limefanya mahojiano na mbunge mmoja wa CCM ambaye amesema ni watu wachache sana ndani ya chama hicho wenye uthubutu wa kumkosoa Rais Magufuli. Wengi wanamuogopa na kumnyeyekea. Mbunge huyo amesema ni watu wachache wenye uthubutu wa kumkosoa Rais Magufuli waziwazi. Wengi wao hata kama wanaona amekosea watamkosoa pembeni lakini kwenye hadhara watamsifia.

Gazeti hilo limeeleza kuwa udhaifu wa Katiba ya nchi ndio unampa mwanya Rais Magufuli kuwa dikteta. Limemnukuu Mwalimu Nyerere aliposema Katiba inampa mdaraka makubwa anayoweza kuyatumia kuwa dikteta. "Katiba ya Tanzania inahitaji kufanyiwa marekebisho ili kumpunguzia Rais madaraka kwa sababu Magufuli anayatumia vibaya" limeongeza.

"Tanzania’s politics have never been truly open, but what is different now is that even CCM, which is by far the country’s most stable institution, is cowed" likimaanisha kwamba Siasa za Tanzania hazijawahi kuwa huru lakini ni jambo la ajabu kwamba hata CCM ambayo inaonekana kuwa taasisi imara inamuogopa Magufuli. (Hili ni jambo la hatari mtu mmoja kuogopwa na taasisi).

Baadhi ya watanzania wamekuwa na maoni tofauti kuhusu makala hiyo. Mwandishi na mchambuzi wa masuala ya siasa Yericko Nyerere amesema gazeti hilo limemdhalilisha "Rais wetu mpendwa" kwenye wigo wa kimataifa. Yericko ameshangazwa na ukimya wa UVCCM kutokusema jambo lolote hadi sasa. Amesema huenda kwa kuwa makala hiyo imeandikwa kwa kiingereza pengine ndio sababu ya ukimya wao. Amewataka kutafuta mkalimani wa kutafsiri ili kama taifa tuungane kukemea Rais wetu kudhalilishwa. Amesema makala hiyo ingeandikwa kwa Kiswahili UVCCM pamoja na msemaji wa chama hicho (aliyepoteza umaarufu) Bw.Humphrey Poepole wangekuwa wameshajibu.

Ni kawaida yao siku zote Wazungu ' Kumchafua ' kwa ' Propaganda ' wao yule Kiongozi imara / mahiri wa Afrika hasa pale ambapo anasimamia vizuri rasilimali za Watanzania wote. Na naamini bado kuna ' Mapopoma ' fulani wataiamini hii taarifa na si ajabu hata wakaanza kuifanya ndiyo ' Agenda ' yao Kuu kuanzia hata Kesho.
 
66 Reactions
Reply
Back
Top Bottom