Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,906
- 30,248
GAZETI LA TAZAMA MRABA - NYUNDO YA WIKI
''MSEKWA AMECHANGANYA HISTORIA YA TANU''
''MSEKWA AMECHANGANYA HISTORIA YA TANU''
Juma lililopita Naibu Mhariri wa JAMHURI Manyerere Jackton aliona mahali makala yangu ambayo nilikuwa nimefanya masahihisho kuhusu historia ya TANU kumweleza Mzee Pius Msekwa kuwa fikra ya kuunda TANU ilikuwa ni mazungumzo ya miaka mingi na ya kila siku kati ya Abdulwahid Kleist Sykes na Hamza Kibwana Mwapachu na si kweli kuwa ni Julius Kambarage Nyerere ndiye aliyeleta fikra ya kuunda chama cha siasa katika TAA pale alipoingia ndani ya uongozi wa TAA mwaka wa 1953.
Manyerere akaniandikia ujumbe mfupi kuniomba achape makala hii na nikamjibu afanye hivyo.
Toleo la TAZAMA la juma hili limechapa makala hiyo.