Fred Mwakitundu
JF-Expert Member
- Dec 31, 2018
- 227
- 383
Taarifa zilizozagaa mjini na kwingineko ni kwamba Gazeti la RAI Nguvu ya Hoja la leo Machi 14 limepigwa pini na wakubwa ndani ya chama cha mapinduzi lisiuzwe mitaani na kuna maagizo kuwa lichomwe moto mara moja ili habari hiyo 'chafu' isiendelee kutamalaki mitaani.
Kama hujabahatika kuliona Gazeti hilo leo pole yako lakini wale ambao tumeliona na kupata nakala limeandika habari kubwa isemayo LOWASA 'AMSEMA' POLE POLE,habari hiyo ina picha ya Lowassa mwenyewe na pembeni picha ya pole pole.
Mtu aliyezungumza nami amesema habari hiyo imewakera sana wakubwa ndani ya Chama kubwa na kuagiza memejimenti ya RAI kuhakikisha gazeti hilo lisiingie mitaani.
Wauza magazeti Jijjini Arusha na Moshi walipokonywa magazeti hayo leo Alfajiri wakielezwa kuna maelekezo kutoka Juu kwamba hakuna kuuza gazeti la RAI na sasa Gazeti hilo litachapishwa upya na kuuzwa wiki ijayo lakini bila habari ya Lowassa.
Kwenye habari hiyo Lowassa akiwa Monduli ameelezea jinsi Pole Pole alivyokuwa akimsema vibaya kwenye luninga baada ya kuwa nje ya chama hicho tangu mwaka 2015 baada ya kutupwa nje na CCM kwenye mbio za urais na baadaye kukimbilia Chadema kujaribu bahati yake ambako nako aliangukia pua.
Sasa tusubiri kitakachotokea huko RAI,je Rostam atakinukisha kwa walioruhusu habari hiyo ichapishwe ama itakuwaje?,ni suala la muda
Kama hujabahatika kuliona Gazeti hilo leo pole yako lakini wale ambao tumeliona na kupata nakala limeandika habari kubwa isemayo LOWASA 'AMSEMA' POLE POLE,habari hiyo ina picha ya Lowassa mwenyewe na pembeni picha ya pole pole.
Mtu aliyezungumza nami amesema habari hiyo imewakera sana wakubwa ndani ya Chama kubwa na kuagiza memejimenti ya RAI kuhakikisha gazeti hilo lisiingie mitaani.
Wauza magazeti Jijjini Arusha na Moshi walipokonywa magazeti hayo leo Alfajiri wakielezwa kuna maelekezo kutoka Juu kwamba hakuna kuuza gazeti la RAI na sasa Gazeti hilo litachapishwa upya na kuuzwa wiki ijayo lakini bila habari ya Lowassa.
Kwenye habari hiyo Lowassa akiwa Monduli ameelezea jinsi Pole Pole alivyokuwa akimsema vibaya kwenye luninga baada ya kuwa nje ya chama hicho tangu mwaka 2015 baada ya kutupwa nje na CCM kwenye mbio za urais na baadaye kukimbilia Chadema kujaribu bahati yake ambako nako aliangukia pua.
Sasa tusubiri kitakachotokea huko RAI,je Rostam atakinukisha kwa walioruhusu habari hiyo ichapishwe ama itakuwaje?,ni suala la muda