Gazeti la Mwananchi na hongo toka Mgodi wa Barrick

Taifa linapoteza pato kubwa kutoka katika ukwepaji wa kodi wa mgodi huu,
kuna manyanyaso kwa wafanyakazi wazalendo kwani wanachukuliwa kama mbwa ndani ya migodi, kuna tofauti kubwa na ubaguzi wa wazi wazi kati ka ngozi nyeupe na sisi weusi.

Kuna uharibifu mkubwa wa mazingira na umwagwaji wa sumu unaoingia kwenye vyanzo vya maji na mazingira.

Na namna ya kuyaziba mdomo yote haya ni hongo kwa magazeti yetu likiwemo Mwananchi linalojinadi kama liko mstari wa mbele katika kuweka wazi mambo yanayoendelea.

Yaani wewe unajiita mzalendo halafu unafumbia macho uozo huo mkubwa kazi yako ni kuja kulaumu gazeti tu? Kama wewe umeshafanya nini kuexpose mambo hayo ukiwa na ushahidi?
 
Tena yale matangazo ya kazi ya barrick usipoteze muda kuomba , hautajibiwa yale ni geresha tuu. money laundering mwananchi style. njia rahisis ya kusafishia pesa haramu za barrick.
 
Mwananchi bado ni gazeti zuri, labda utuambie hizo nafasi za kazi zinazo tangazwa zina watu au hakuna kama ulikuwa mmoja wapo wa waliomba! Nitamtafuta mtu wangu WAKUCHORONGA ambae anafanya huko atuambie za uhakika
 
Ndugu yangu kama unadhani unajua nusu ya siri za migodi kwa taarifa yako hujui hata robo.
Hutakiwi kutumia 10% ya ubongo wako kugundua kwa nini barick wanatangaza page tatu kwenye gazeti la mwananchi,kila siku,post hizo hizo kwa miaka mitatu??!!
Hapa ndio utaelewa wanakwepa kutoa hela cash,wanajifanya wamewauzia kurasa.

Hivi mnapolituhumu gazeti la mwananchi kwamba limechukua rushwa ya matangazo toka Barrick ili wasiandike kitu gani ambacho ni kipya..? Habari zote za migodi ya hapa nchini hakuna asieijua na Mwananchi ni miongoni mwa vyombo vichache vya habari ambavyo vilisaidia kueneza habari hizi mbovu za migodi yetu ikiwamo ya Barrick.. Acheni kugeuza JF kama kijiwe cha kahawa jamani.. Kuna serious issues za kujadili hapa..
 
This circumstancial evidence is not conclusive. It has to be corroborated before incriminating the newspaper.
 
Mwananchi, mnakalia kutangaza nafasi za kazi kwenye migodi ya hawa wezi barrick,je, mnajua wanavyoinyonya nchi? Kuna ukwepaji mkubwa wa kodi,kiwango cha dhahabu wanayozalisha hakuna anayejua si TRA wala wakala wa madini, mnakumbuka wakala wa madini na TRA walivyojiumauma kuhusu thamani ya dhahabu katika helikopta iliyotekwa ikiwa imesheheni dhahabu na WAZALENDO mwaka jana kule Geita! Bila aibu wakasema eti serikali ilikuwa ipate billion 1 kama kodi toka mzigo wenye thamani ya billion 43. Ukweli ni kuwa mzigo ulikuwa wa thamani kubwa kuliko hiyo. Sasa tujiulize ni mara ngapi helikopta inafuta dhahabu kwa mwezi kwa mgodi mmoja. Mimi ni mkazi wa Kahama jirani na Mgodi wa Buzwagi,hakika ni zaidi ya mara 3 kwa mwezi, sasa chukua hesabu hiyo ya TRA kwa mwezi ni bill 129 na kwa mwaka ni billion 1548 hapo serikali inaambulia kodi ya billion 36.Unaweza jikuta unalia kwa sauti na watu kudhani chizi kumbe uchungu wa dhuluma hii.
Utapeli wa maeneo ya watu katika vijiji vinavyozunguka mgodi,uchafuzi wa mazingira, dhuluma kwa wafanyakazi wazalendo ni kati ya mambo yanafanywa na wezi hawa wanaojiita wawekezaji. Mulikeni hayo ninyi wa gazeti la mwananchi. Njooni Kahama muone utajiri tulionao chini ya ardhi vs umaskini wa wananchi wa Kahama.
 
Ndugu yangu kama unadhani unajua nusu ya siri za migodi kwa taarifa yako hujui hata robo.
Hutakiwi kutumia 10% ya ubongo wako kugundua kwa nini barick wanatangaza page tatu kwenye gazeti la mwananchi,kila siku,post hizo hizo kwa miaka mitatu??!!
Hapa ndio utaelewa wanakwepa kutoa hela cash,wanajifanya wamewauzia kurasa.

Huyu mtoa hoja ana lake na Gazeti la Mwananchi. Nadhani anaudanganya umma kwa kuwa haupati magazeti yote. Tangazo analosema pia liko The Guardian leo kwenye pull out ya Sports & Entertainment Pg iii; Nipashe pg 22; Majira pg 18; Mtanzania pg 15; (kwa hapa sina daily news na habari leo). Anataka kusema na hayo yote yamehongwa? Mbona habari za barrick kunyanyasa wananchi zinatoka kila wakati? Ni zipi amezipeleka kwenye magazeti hayo na hazikutoka? Tupime tuone wenyewe.
 
Usikute mtoa mada amenyimwa tangazo la nafasi za kazi kwenye gazeti lake/analofanyia kazi.
Ebu funguka pls ili tujue kilichotokea.
Ila frankly speaking Barrick kwa kuhonga ili maovu yasiwekwe hadharani wako fiti nadhani kuna provision kwenye bajeti yao kwa ajili ya kunyamazisha watu
 
Uamuzi wa Kutangaza au kutotangaza na Chombo fulani cha Habari upo kwa Mtangazaji (Advertiser).

Hakuna sheria au sera yoyote ile inayomlazimisha mtangazaji (Advertiser) kutumia au kutotumia chombo fulani cha habari bali ni makubaliano tu baina ya chombo na mtangazaji mwenyewe
Mbona Emirates wanatangaza na Mwananchi na The Citizen peke yake? Je na wao wanaufisadi?

kuna matangazo yanaweza kujirudia hasa ya kibiashara lakini tangazo la nafasi za kazi hizo hizo zirudiwe kwenye gazeti hilo hilo kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu?. Na kama wewe ni mfuatiliaji wa gazeti la mwananchi tazama nakala zake kabla ya mwanzo wa Tangazo hili huone jinsi walivyokuwa wakiripoti masuala ya wizi katika migodi yetu na sasa gazeti hili limeshindwa kabisa kuandika chochote kuhusu wizi unaoendelea kwani wao wamekuwa ni sehemu ya wagawiwa wa masalio ya wizi unaotokana na kampuni ya Barick...kuna mengi yanaendelea na posho za wanahabari wa magazeti yetu kutoka kwa mgodi wa barick huku wananchi na wafanyakazi wa mgodi huu wakiteseka na kubaguliwa vilivyo...

nadhani biashara ya gazeti la mwananchi na mgodi wa barick ifike wakati basi iwekwe wazi, kama wanahisa ndani ya mgodi huu pia waweke wazi interest zao
 
Hii nimeiona kitambo si Mwananchi tu kumbuka hata Ippmedia nayo ilihongwa kuna kipindi magazeti yake yalikuwa yanaandika sana hali ya unyanyasaji wa wananchi lakini ghafla Mengi akakaribishwa huko kama mgeni rasmi na kimya hatusikii cha Muazini wala nini!
 
quote_icon.png
By ARV Ndugu yangu kama unadhani unajua nusu ya siri za migodi kwa taarifa yako hujui hata robo.
Hutakiwi kutumia 10% ya ubongo wako kugundua kwa nini barick wanatangaza page tatu kwenye gazeti la mwananchi,kila siku,post hizo hizo kwa miaka mitatu??!!

Hapa ndio utaelewa wanakwepa kutoa hela cash,wanajifanya wamewauzia kurasa.

Huyu mtoa hoja ana lake na Gazeti la Mwananchi. Nadhani anaudanganya umma kwa kuwa haupati magazeti yote. Tangazo analosema pia liko The Guardian leo kwenye pull out ya Sports & Entertainment Pg iii; Nipashe pg 22; Majira pg 18; Mtanzania pg 15; (kwa hapa sina daily news na habari leo). Anataka kusema na hayo yote yamehongwa? Mbona habari za barrick kunyanyasa wananchi zinatoka kila wakati? Ni zipi amezipeleka kwenye magazeti hayo na hazikutoka? Tupime tuone wenyewe.

Nadhani ARV atakuelewa hapa.. Na mpaka kwenye Daily News la jana nako kuna page nzima ya tangazo la Barrick ukurasa wa 31.. Kwa hiyo waseme ina maana wamehonga magazeti yote..?
 
Oohh? Wapi tido mhando na kurugenzi yako mpya jibu mashtaka haya najua nawe uko huku
 
Kazi hipo sasa kumbe ndio namna ya kuyafumba magazeti yetu mdomo? nadhani wakishindwa kwa njia hii basi watayanunua kabisa na kuyazima kama enzi za rai ikauzwa na kuchinjwa kabisa
 
profile_mask2.png

nevilletz@gmail.com

15:56 (7 minutes ago)
cleardot.gif



cleardot.gif

cleardot.gif

to fkatulanda, mabadilikotanz.
cleardot.gif


Mwananchi ni taasisi kubwa, policy iko very crear, markerting na editorial ni idara tofauti na wala hazihusiani. Anyway kama ushahidi kwamba wahariri zaidi ya 20 wa MCL wamehongwa na Barrick basi auweke hadharani. Vinginevyo zinaweza kuwa ni tuhuma zenye malengo ya kuchafuana tu. Credibility ya Mwananchi kila mmoja wetu anaifahamu, tuhukumiwe kwa haki . Hata serikali inaongoza kwa matangazo yake MCL lakini siyo hongo!
 
Makampuni huangalia ni gazeti lipi linaloweza kuwafikia watu wengi na ndio huwa kipaombele katika kupeleka matangazo yao, unless kama tangazo hilo ni maalumu kwa watu wa eneo fulani au watu wa aina fulani, ndipo vyombo vya habari vinavyosikilizwa ama kusomwa kwa wingi maeneo/watu husika hutumiwa.

Acha majungu wewe kijana,

Umeelewa?
 
profile_mask2.png

nevilletz@gmail.com
15:56 (7 minutes ago)
cleardot.gif


cleardot.gif

cleardot.gif
to fkatulanda, mabadilikotanz.
cleardot.gif

Mwananchi ni taasisi kubwa, policy iko very crear, markerting na editorial ni idara tofauti na wala hazihusiani. Anyway kama ushahidi kwamba wahariri zaidi ya 20 wa MCL wamehongwa na Barrick basi auweke hadharani. Vinginevyo zinaweza kuwa ni tuhuma zenye malengo ya kuchafuana tu. Credibility ya Mwananchi kila mmoja wetu anaifahamu, tuhukumiwe kwa haki . Hata serikali inaongoza kwa matangazo yake MCL lakini siyo hongo![/QUOTE

Tambua mfumo wa habari ni sawa na Auditing kama Mwananchi au gazeti lingine linapoweza kuvuna mamilioni ya fedha toka katika kampuni fulani au mtu fulani kuna udugu na urafiki unajengeka. Inawezekanaje kwa tangazo la nafasi za kazi linalolipiwa mamilioni ya shilingi kila siku liwe kwenye gazeti la mwananchi pasipo kuathiri utendaji na uhuru wa gazeti?

Tungeshangaa kama mwananchi mbali na kupokea mabilioni hayo toka kwa kampuni ya barick wangeweza kuandika unyanyasaji na ukandamizaji wanaofanyiwa watumishi wa mgodi huu na kama ingeweza kuandika chochote juu ya ukwepaji mkubwa wa kodi wa rafiki yao barick anayewawezesha kupata gawio la mamilioni kila siku kutokana na majadiliano yao ya kupeana pesa kupitia mfumo wa matangazo na posho kwa waandishi wa habari wake.

Tambua kampuni ya barick ni jabali la kunyamazisha taasisi na watu wanaoweza kuwa na namna ya kuweka wazi maslahi yao katika umma. wanahistoria ya kufadhili safari na semina ya kamati za Bunge na kuhonga wabunge na watu wanaodhani wangeweza kukwamisha mipango yao ya kutetea wanyonge.Tulidhani wato waliopotea tungebaki na mwanaharakati wetu wa gazeti la Mwananchi lakini nalo limetumbukia katika mfumo hule hule wa Hongo za kufungwa mdomo.
 
profile_mask2.png

nevilletz@gmail.com
15:56 (7 minutes ago)
cleardot.gif

cleardot.gif

cleardot.gif
to fkatulanda, mabadilikotanz.
cleardot.gif

Mwananchi ni taasisi kubwa, policy iko very crear, markerting na editorial ni idara tofauti na wala hazihusiani. Anyway kama ushahidi kwamba wahariri zaidi ya 20 wa MCL wamehongwa na Barrick basi auweke hadharani. Vinginevyo zinaweza kuwa ni tuhuma zenye malengo ya kuchafuana tu. Credibility ya Mwananchi kila mmoja wetu anaifahamu, tuhukumiwe kwa haki . Hata serikali inaongoza kwa matangazo yake MCL lakini siyo hongo![/QUOTE

Tambua mfumo wa habari ni sawa na Auditing kama Mwananchi au gazeti lingine linapoweza kuvuna mamilioni ya fedha toka katika kampuni fulani au mtu fulani kuna udugu na urafiki unajengeka. Inawezekanaje kwa tangazo la nafasi za kazi linalolipiwa mamilioni ya shilingi kila siku liwe kwenye gazeti la mwananchi pasipo kuathiri utendaji na uhuru wa gazeti?

Tungeshangaa kama mwananchi mbali na kupokea mabilioni hayo toka kwa kampuni ya barick wangeweza kuandika unyanyasaji na ukandamizaji wanaofanyiwa watumishi wa mgodi huu na kama ingeweza kuandika chochote juu ya ukwepaji mkubwa wa kodi wa rafiki yao barick anayewawezesha kupata gawio la mamilioni kila siku kutokana na majadiliano yao ya kupeana pesa kupitia mfumo wa matangazo na posho kwa waandishi wa habari wake.

Tambua kampuni ya barick ni jabali la kunyamazisha taasisi na watu wanaoweza kuwa na namna ya kuweka wazi maslahi yao katika umma. wanahistoria ya kufadhili safari na semina ya kamati za Bunge na kuhonga wabunge na watu wanaodhani wangeweza kukwamisha mipango yao ya kutetea wanyonge.Tulidhani wato waliopotea tungebaki na mwanaharakati wetu wa gazeti la Mwananchi lakini nalo limetumbukia katika mfumo hule hule wa Hongo za kufungwa mdomo.

gm26may@gmail.com
15:51 (1 hour ago)
cleardot.gif


cleardot.gif

to mabadilikotanz.
cleardot.gif


Hata mimi ilibidi kuangalia magazeti mengine na kweli inaonekana matangazo hayo yanatoka magazeti mengi tu

Ni Nadra sana kumaliza wiki bila kuona nafasi za kazi za Barrick kwenye magazeti kadhaa

Sasa labda aseme yote hayo huwa yanahongwa

Ingawa nashindwa kuelewa utahongaje kwa kuweka tangazo la kazi

Nategemea watu watahongwa ili waandike mazur kuhusu kampuni fulan na kufumbia macho maovu/ mapungufu ya kampuni hiyo

Au wangehongwa wasiandike chochote about Barrick

Nadhani mwandishi aliamua kuwa mvivu wa kufikiri
 
Mwananchi, mnakalia kutangaza nafasi za kazi kwenye migodi ya hawa wezi barrick,je, mnajua wanavyoinyonya nchi? Kuna ukwepaji mkubwa wa kodi,kiwango cha dhahabu wanayozalisha hakuna anayejua si TRA wala wakala wa madini, mnakumbuka wakala wa madini na TRA walivyojiumauma kuhusu thamani ya dhahabu katika helikopta iliyotekwa ikiwa Buzwagi,hakika ni zaidi ya mara 3 kwa mwezi, sasa chukua hesabu hiyo ya TRA kwa mwezi ni bill 129 na kwa mwaka ni billion 1548 hapo serikali inaambulia kodi ya billion 36.Wakala wa Madini wanafanya kazi nzuri sana mzee. Usiwasingizie kwa hilo. Aliyejichanganya alikuwa afisa madini, wall TRA hawakusema kitu. Ukitaka kujua kazi nzuri ya Wakala wa Madini, tembelea tovuti yao Tanzania Minerals Audit Agency.
 
Gazeti la mwananchi limekubali kuwa miongoni mwa magazeti yaliyokubali kufumba mdomo kwa ajili ya kupata nafasi ya kupewa matangazo ya baric kila wakati.

Unajiuliza tangazo la kazi la mgodi huu linalotolewa kila siku kwa takribani miaka miwili sasa na linalochokua kurasa tatu na zaidi ni sababu gani?

Huu ni mpango wa hongo kwa gazeti la mwananchi kwani na gazeti la mwananchi limekubali kuhongeka na kufungwa mdomo toka kwa mgodi huu na kuacha kuandika mambo ya dhuruma yanayofanywa na mgodi huu.

Upuuzi mtupu! Siyo Barrick tu peke yao wanaotangaza Mwananchi. Serikali pamoja na makampuni yote makubwa binafsi yanatangaza Mwananchi. This is purely a business decision. Mwananchi ndio gazeti linaloongoza Tanzania kwa sasa, hivyo watangazaji wa biashara, huduma na fursa wanakimbilia huko. Kama Barrick kweli ina hizo kashfa, kwa nini basi magazeti mengine yasiyopata hayo matangazo (hongo kwa mujibu wa mtoa mada) wasiandike hizo habari?! Kama kweli kuna kashfa za Barrick, basi magazeti mengine yasio hongwa eti kwa kupewa matangazo wanashindwa nini kufichua hizo kashfa?

My take: Mtoa mada hii aidha ni mkurupukaji na mwenye akili finyu au ni gazeti mshindani wa Mwananchi anayeona wivu wa kike kwa gazeti la Mwananchi kutokana na matangazo wanayoendelea kuyapata. Au all the above!
 
Back
Top Bottom