Gazeti la Mwanahalisi na kichwa hiki cha habari litasalimika?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,011
144,371
Kichwa cha habari kinasomeka:

"Njaa kali yaja"

Chini yake kuna maandishi madogo yanayosomeka:

"Akiba ya chakula yakauka"

Kwa kifupi, gazeti hili la Agosti 15-21,2016, Toleo Na.352,limeandika habari ya serikali kutokuwa na akiba ya kutosha ya chakula na zaidi limenukuu maelezo ya Kafulila kuhusu kushuka kwa akiba ya chakula alipoongea katika kongamano liliokuwa limeandaliwa na Baraza la Vijana wa Chadema mwishoni mwa wiki iliyopita.

Ukisoma habari nzima ambayo inayohusisha pia sehemu ndogo ya taarifa/maelezo ya Waziri wa Kilimo wakati akisoma bajeti ya wizara yake Bungeni mwaka huu,utagundua hakuna habari yoyote ya nyongeza kwa lengo la kuongeza chumvi zaidi ya kutumia taarifa ya Kafulila na maelezo ya Wazi Nchemba Bungeni kama chanzo tu cha taarifa hii.

Sasa wadau, licha ya habari yenyewe kutokuwa na kitu kipya, lakini kwa kutumia hiyo heading,gazeti hili litasalimika?

Labda swali la msingi ni je, kinachogomba ni kichwa cha habari au ni habari yenyewe?
 
Kinachomata ni kichwa tuu!, ila gazeti la Mwananchi, ndilo linaloongoza kwa umakini nchini katika magazeti ya Kiswahili.

Tena sio kwenye habari tuu, kichwa ndio kila kitu!.

P.
Sawa.Sasa wwewe kama Mwandishi,nini maoni yako kuhusu hiyo heading?
 
Sawa,wewe kama Mwandishi,nini maoni yako kuhusu hiyo heading?
iko poa wala haina tatizo lolote!, kwa sababu huo ndio ukweli wenyewe!, tatizo kwangu ni mpayukaji fulani aliyesema hatoi chakula kwa wenye njaa, ikibidi watu wafe njaa, bora wafe kuliko kuwagawia chakula!, moja ya malengo ya hifadhi ya chakula, ni pamoja na kukigawa kwenye baa la njaa!, kitendo tuu cha kupayukwa, ikibidi watu wafe njaa lakini hatugawi chakula, ni taarifa tosha kuwa hicho chakula cha kugawiwa bure hakipo!. Itakuwa ni aibu ya mwaka kama WFP, na FAO ndio watatuletea chakula!.

Mimi nilikulaga yanga!, enzi zile watu wanavaa sandarusi na magunia!, unifomu za madurufu, nimevaa!.

Pasco
 
iko poa wala haina tatizo lolote!, kwa sababu huo ndio ukweli wenyewe!, tatizo kwangu ni mpayukaji fulani aliyesema hatoi chakula kwa wenye njaa, ikibidi watu wafe njaa, bora wafe kuliko kuwagawia chakula!, moja ya malengo ya hifadhi ya chakula, ni pamoja na kukigawa kwenye baa la njaa!, kitendo tuu cha kupayukwa, ikibidi watu wafe njaa lakini hatugawi chakula, ni taarifa tosha kuwa hicho chakula cha kugawiwa bure hakipo!. Itakuwa ni aibu ya mwaka kama WFP, na FAO ndio watatuletea chakula!.

Mimi nilikulaga yanga!, enzi zile watu wanavaa sandarusi na magunia!, unifomu za madurufu, nimevaa!.

Pasco
Mkuu chagua maneno ya kuandika
 
Kichwa cha habari kinasomeka:

"Njaa kali yaja"

Chini yake kuna maandishi madogo yanayosomeka:

"Akiba ya chakula yakauka"

Kwa kifupi, gazeti hili la Agosti 15-21,2016, Toleo Na.352,limeandika habari ya serikali kutokuwa na akiba ya kutosha ya chakula na zaidi limenukuu maelezo ya Kafulila kuhusu kushuka kwa akiba ya chakula alipoongea katika kongamano liliokuwa limeandaliwa na Baraza la Vijana wa Chadema mwishoni mwa wiki iliyopita.

Ukisoma habari nzima ambayo inayohusisha pia sehemu ndogo ya taarifa/maelezo ya Waziri wa Kilimo wakati akisoma bajeti ya wizara yake Bungeni mwaka huu,utagundua hakuna habari yoyote ya nyongeza kwa lengo la kuongeza chumvi zaidi ya kutumia taarifa ya Kafulila na maelezo ya Wazi Nchemba Bungeni kama chanzo tu cha taarifa hii.

Sasa wadau, licha ya habari yenyewe kutokuwa na kitu kipya, lakini kwa kutumia hiyo heading,gazeti hili litasalimika?

Labda swali la msingi ni je, kinachogomba ni kichwa cha habari au ni habari yenyewe?
Mkuu hilo si ndilo gazeti pendwa lenu? Gazeti la mheshimiwa wenu!! Kumbe linaokoteza vihabari? Au unatutega?
 
iko poa wala haina tatizo lolote!, kwa sababu huo ndio ukweli wenyewe!, tatizo kwangu ni mpayukaji fulani aliyesema hatoi chakula kwa wenye njaa, ikibidi watu wafe njaa, bora wafe kuliko kuwagawia chakula!, moja ya malengo ya hifadhi ya chakula, ni pamoja na kukigawa kwenye baa la njaa!, kitendo tuu cha kupayukwa, ikibidi watu wafe njaa lakini hatugawi chakula, ni taarifa tosha kuwa hicho chakula cha kugawiwa bure hakipo!. Itakuwa ni aibu ya mwaka kama WFP, na FAO ndio watatuletea chakula!.

Mimi nilikulaga yanga!, enzi zile watu wanavaa sandarusi na magunia!, unifomu za madurufu, nimevaa!.

Pasco
Duh!Umeua!
 
iko poa wala haina tatizo lolote!, kwa sababu huo ndio ukweli wenyewe!, tatizo kwangu ni mpayukaji fulani aliyesema hatoi chakula kwa wenye njaa, ikibidi watu wafe njaa, bora wafe kuliko kuwagawia chakula!, moja ya malengo ya hifadhi ya chakula, ni pamoja na kukigawa kwenye baa la njaa!, kitendo tuu cha kupayukwa, ikibidi watu wafe njaa lakini hatugawi chakula, ni taarifa tosha kuwa hicho chakula cha kugawiwa bure hakipo!. Itakuwa ni aibu ya mwaka kama WFP, na FAO ndio watatuletea chakula!.

Mimi nilikulaga yanga!, enzi zile watu wanavaa sandarusi na magunia!, unifomu za madurufu, nimevaa!.

Pasco
Kuhusu hiyo Yanga hawa vijana wa DotCom hawatakuelewa watadhani ulikuwa unakula club ya Yanga!! Nami niliila tena ya mgawo kupitia Shirika la Ugawaji la Taifa (Ugawaji) au RTC na Maduka ya Kaya!!
 
Na mkuu wa kaya aliwatahadharisha wasengerema kwamba serikali haina shamba. Wasitarajie kupata chakula cha msaada kutoka serikalini.
 
Njaa imekuja serikali imekauka. Unadhani baba jesca aliposema serikali yangu haina chakula cha kugawa unadhani alitania?? Alimaanisha kweli wamekauka.. Kudadeki ACHA wasome namba mimi naendelee na maandalizi ya mkesha wa ukuta
 
Mwaka huu kiukweli chakula hamna mi nililima mahindi ila nilichovuna siri yangu sijui tatizo lilikuwa hali ya hewa au mbolea tuliyotumia mwaka huu ndo tatizo au laah
 
Kwa taarifa tu nchi yetu ndio nchi pekew ambao INA hadhina kubwa zaidi kuliko nchi zote za EAST AFRICA
Kulikua na wasiwasi wa wilaya 46 kuishia chakula lakini serkali imekwisha sawazisha hilo
Na tayari serkali imeamua kuaruhusu wannchi kuuza mazao yao nje ya nchi
 
Kuhusu hiyo Yanga hawa vijana wa DotCom hawatakuelewa watadhani ulikuwa unakula club ya Yanga!! Nami niliila tena ya mgawo kupitia Shirika la Ugawaji la Taifa (Ugawaji) au RTC na Maduka ya Kaya!!
Tulikuwa tunakimbilia gari la ugawaji linapopeleka chakula kwenye duka la kaya. Tuombe Mungu hayo yasirudie tena....
 
Mhariri wa hili gazeti hua anajua namna gani ya kuahadaa ma mbweha wake kulinunua kwa kuandika kichwa cha habari
Unamnukuu tumbili kama kafulila hana jipya kabisa amebaki kulea motto wake mjinga yule
Kwa taarifa yako limenukuu na maneno ya Mkuu wa Kaya kuwa hatatoa chakula cha msaada.
 
Back
Top Bottom