samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
Leo tarehe 29/06/2012 asubuhi mishale ya saa moja na nusu asubuhi nilikuwa naangalia mapitio ya magazeti katika televisheni ya ATN ambapo kelvin moto alikuwa akisoma mapitio ya magazeti. Alianza na gazeti la mtanzania na habari iliyokuwa kwenye ukurasa wa mbele ilisomeka siri ya kutekwa dk. ulimboka...........akisoma habari hiyo kwa masikitiko makubwa kelvin motto alisema dokta ulimboka alimtambua mmoja wa wanajopo wanaounda timu ya uchunguzi iliyoundwa na jeshi la polisi kuwa ni mmoja kati ya watu waliomteka na hivyo kumwambia amrudishie simu yake na waleti yake. Pia alisema afande huyo ambaye hakutajwa jina kwenye gazeti alimuuliza dk ulimboka kama chadema wanahusika na utekwaji wake. Habari hiyo ambayo iliripotiwa na gazeti hilo kutoka chanzo cha uhakika iliendelea kusema mara baada ya kuona ametambulika afande huyo alitoka wodini kimya huku ameinamisha kichwa chini.
Nilipatwa na shauku kubwa sana ya kusoma gazeti hilo ili nipate undani wa mkasa huo. Kitu cha ajabu nilipoenda kununua gazeti la mtanzania nikakuta ukurasa wa mbele kuna habari inayosomeka hivi "madaktari waanza kusimamishwa kazi" nilishangaa ikabidi nifungue kurasa za ndani kuitafuta habari niliyoitaka bila mafanikio. Nilijiuliza maswali mengi bila majibu. Kwanza nikawaza inawezekana mtanzania wametoa version mbili za gazeti lao leo, pili nikasema inawezekana nilisikia vibaya labda lilikuwa ni gazeti la tanzania daima lakini hailkuwa hivyo, tatu nikasema kuna mazingara yamefanyika au, nne nikawaza au nilikuwa naota lakini nikasema hapana. Nauliza kama kuna mwanajamvi yeyote aliye angalia ATN na kusikia wakati kelvin motto akisoma mapitio ya magazeti ili anisaidie kunipa majibu. Maana kelvini aliisoma kwa msisitizo na kuwataka wananchi wanunue nakala ili waone nchi yetu ilipofika. Natamani ningekuwa na namba ya simu ya kelvin motto nimuulize huenda angenipa jibu.
Nilipatwa na shauku kubwa sana ya kusoma gazeti hilo ili nipate undani wa mkasa huo. Kitu cha ajabu nilipoenda kununua gazeti la mtanzania nikakuta ukurasa wa mbele kuna habari inayosomeka hivi "madaktari waanza kusimamishwa kazi" nilishangaa ikabidi nifungue kurasa za ndani kuitafuta habari niliyoitaka bila mafanikio. Nilijiuliza maswali mengi bila majibu. Kwanza nikawaza inawezekana mtanzania wametoa version mbili za gazeti lao leo, pili nikasema inawezekana nilisikia vibaya labda lilikuwa ni gazeti la tanzania daima lakini hailkuwa hivyo, tatu nikasema kuna mazingara yamefanyika au, nne nikawaza au nilikuwa naota lakini nikasema hapana. Nauliza kama kuna mwanajamvi yeyote aliye angalia ATN na kusikia wakati kelvin motto akisoma mapitio ya magazeti ili anisaidie kunipa majibu. Maana kelvini aliisoma kwa msisitizo na kuwataka wananchi wanunue nakala ili waone nchi yetu ilipofika. Natamani ningekuwa na namba ya simu ya kelvin motto nimuulize huenda angenipa jibu.