Gazeti la mtanzania la tarehe 29/06/2012 - SOMA TAFADHALI

samirnasri

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
1,388
213
Leo tarehe 29/06/2012 asubuhi mishale ya saa moja na nusu asubuhi nilikuwa naangalia mapitio ya magazeti katika televisheni ya ATN ambapo kelvin moto alikuwa akisoma mapitio ya magazeti. Alianza na gazeti la mtanzania na habari iliyokuwa kwenye ukurasa wa mbele ilisomeka siri ya kutekwa dk. ulimboka...........akisoma habari hiyo kwa masikitiko makubwa kelvin motto alisema dokta ulimboka alimtambua mmoja wa wanajopo wanaounda timu ya uchunguzi iliyoundwa na jeshi la polisi kuwa ni mmoja kati ya watu waliomteka na hivyo kumwambia amrudishie simu yake na waleti yake. Pia alisema afande huyo ambaye hakutajwa jina kwenye gazeti alimuuliza dk ulimboka kama chadema wanahusika na utekwaji wake. Habari hiyo ambayo iliripotiwa na gazeti hilo kutoka chanzo cha uhakika iliendelea kusema mara baada ya kuona ametambulika afande huyo alitoka wodini kimya huku ameinamisha kichwa chini.

Nilipatwa na shauku kubwa sana ya kusoma gazeti hilo ili nipate undani wa mkasa huo. Kitu cha ajabu nilipoenda kununua gazeti la mtanzania nikakuta ukurasa wa mbele kuna habari inayosomeka hivi "madaktari waanza kusimamishwa kazi" nilishangaa ikabidi nifungue kurasa za ndani kuitafuta habari niliyoitaka bila mafanikio. Nilijiuliza maswali mengi bila majibu. Kwanza nikawaza inawezekana mtanzania wametoa version mbili za gazeti lao leo, pili nikasema inawezekana nilisikia vibaya labda lilikuwa ni gazeti la tanzania daima lakini hailkuwa hivyo, tatu nikasema kuna mazingara yamefanyika au, nne nikawaza au nilikuwa naota lakini nikasema hapana. Nauliza kama kuna mwanajamvi yeyote aliye angalia ATN na kusikia wakati kelvin motto akisoma mapitio ya magazeti ili anisaidie kunipa majibu. Maana kelvini aliisoma kwa msisitizo na kuwataka wananchi wanunue nakala ili waone nchi yetu ilipofika. Natamani ningekuwa na namba ya simu ya kelvin motto nimuulize huenda angenipa jibu.
 
Leo tarehe 29/06/2012 asubuhi mishale ya saa moja na nusu asubuhi nilikuwa naangalia mapitio ya magazeti katika televisheni ya ATN ambapo kelvin moto alikuwa akisoma mapitio ya magazeti. Alianza na gazeti la mtanzania na habari iliyokuwa kwenye ukurasa wa mbele ilisomeka siri ya kutekwa dk. ulimboka...........akisoma habari hiyo kwa masikitiko makubwa kelvin motto alisema dokta ulimboka alimtambua mmoja wa wanajopo wanaounda timu ya uchunguzi iliyoundwa na jeshi la polisi kuwa ni mmoja kati ya watu waliomteka na hivyo kumwambia amrudishie simu yake na waleti yake. Pia alisema afande huyo ambaye hakutajwa jina kwenye gazeti alimuuliza dk ulimboka kama chadema wanahusika na utekwaji wake. Habari hiyo ambayo iliripotiwa na gazeti hilo kutoka chanzo cha uhakika iliendelea kusema mara baada ya kuona ametambulika afande huyo alitoka wodini kimya huku ameinamisha kichwa chini.

Nilipatwa na shauku kubwa sana ya kusoma gazeti hilo ili nipate undani wa mkasa huo. Kitu cha ajabu nilipoenda kununua gazeti la mtanzania nikakuta ukurasa wa mbele kuna habari inayosomeka hivi "madaktari waanza kusimamishwa kazi" nilishangaa ikabidi nifungue kurasa za ndani kuitafuta habari niliyoitaka bila mafanikio. Nilijiuliza maswali mengi bila majibu. Kwanza nikawaza inawezekana mtanzania wametoa version mbili za gazeti lao leo, pili nikasema inawezekana nilisikia vibaya labda lilikuwa ni gazeti la tanzania daima lakini hailkuwa hivyo, tatu nikasema kuna mazingara yamefanyika au, nne nikawaza au nilikuwa naota lakini nikasema hapana. Nauliza kama kuna mwanajamvi yeyote aliye angalia ATN na kusikia wakati kelvin motto akisoma mapitio ya magazeti ili anisaidie kunipa majibu. Maana kelvini aliisoma kwa msisitizo na kuwataka wananchi wanunue nakala ili waone nchi yetu ilipofika. Natamani ningekuwa na namba ya simu ya kelvin motto nimuulize huenda angenipa jibu.

Hujakosea kabisa. Ni kweli kwamba leo gazeti la Mtanzania lina habari 2 zinazochanganya kwenye front page.Ukiingia kwenye gazeti la mtanzania online unapata habari tofauti na iliyojitokeza kwenye gazeti hilo asubuhi. Ukiangalia kwenye millard ayo blogspot,gazeti la mtanzania linaonyesha kwamba Dr. Ulimboka amemtambua mtuhumiwa na kumwomba wallet na simu yake. Angalia hata sasa kwenye millard ayo blogspot kwenye sehemu ya magazeti ya leo.

2115-450x600.jpg



Source: Millard Ayo blogspot,29.06.2012
 
Inawezekana wametoa version mbili leo ila mimi nimenunua lenye habari iliyosomwa ATN. Kuna jina moja la askari limehifadhiwa ila ametajwa mtu anayeitwa Ayoub kuwa ndie aliyempigia simu dr. Ulibomka kabla ya kutekwa.
 
Inawezekana
wametoa version mbili leo ila mimi nimenunua lenye habari iliyosomwa ATN. Kuna jina moja
la askari limehifadhiwa ila ametajwa mtu anayeitwa Ayoub kuwa ndie aliyempigia simu dr. Ulibomka kabla ya kutekwa.

inategemea habari hiyo wameipata muda gani. habari moto zikifika wakati gazeti liko mitamboni kuna kitu kinaitwa stop press ambapo uchapaji
husimama na gazeti kupangwa upya. sasa nakala za awali hutumwa mikoani hivyo magazeti hayo yataikosa hiyo habari moto.
 
Nikweli inachanganya lakini ukiangalia vizuri habari hiyo ipo imelezea kisa kizima ya jinsi ilivyotokea ukiangalia vizuri kurasa kama sikakosea ya tatu utaiona hata mimi ilinichukuwamuda kuiona.
 
Back
Top Bottom