William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,588
- 10,375
- Gazeti la Mawio jana liliandika habari ya KUTUNGA na ya UONGO likiwa na nia ya kumdhalilisha Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Makonda kwamba alipewa Ukuu wa Wilaya kwa sababu aliwahi kumfunga kamba za viatu Mtoto wa Rais wa zamani Dr. JK huku likionyesha picha ambayo Mtoto huyo wa Rais wa zamani na Mbunge wa Chalinze (CCM) Mh. Ridhiwani Kikwete akifungwa kamba viatu na mtu ambaye sio Mkuu huyo wa Wilaya ya Kinondoni.
- Ukweli ni kwamba picha hiyo ni ya Mh. Ridhiwani akifungwa kamba za viatu na Msaidizi wa Mwanamitindo maarufu hapa nchini Sheria Ngowi na kitendo hicho kilifanyika Dukani kwa Mwanamitindo huyo Masaki. Gazeti la Mawio linaonekana kuzibeba habari hizo kwenye mtandao wa kijamii hasa wa Instagram bila kufanyia UTAFITI na UKWELI wa habari hii.
- Sijui sheria inasema nini unapotokea udhalilishaji kama huu, tabia ya kubeba habari za Instagram bila kuzifanyia utafiti inaonekana kuwatesa mpaka baadhi ya Watendaji wa Serikali, mimi nafikiri ni muhimu sana Gazeti la Mawio likaomba radhi hasa kwa sisi wasomaji wake kwa kutulisha habari ya uongo.
Le Mutuz Nation
- Ukweli ni kwamba picha hiyo ni ya Mh. Ridhiwani akifungwa kamba za viatu na Msaidizi wa Mwanamitindo maarufu hapa nchini Sheria Ngowi na kitendo hicho kilifanyika Dukani kwa Mwanamitindo huyo Masaki. Gazeti la Mawio linaonekana kuzibeba habari hizo kwenye mtandao wa kijamii hasa wa Instagram bila kufanyia UTAFITI na UKWELI wa habari hii.
- Sijui sheria inasema nini unapotokea udhalilishaji kama huu, tabia ya kubeba habari za Instagram bila kuzifanyia utafiti inaonekana kuwatesa mpaka baadhi ya Watendaji wa Serikali, mimi nafikiri ni muhimu sana Gazeti la Mawio likaomba radhi hasa kwa sisi wasomaji wake kwa kutulisha habari ya uongo.
Le Mutuz Nation