Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 17,378
- 21,070
Kwa hakika nchi yetu kwa sasa imekuwa feki kwa 100%.
Kitu pekee kilichobaki ni kumsifia Rais Magufuli hata kama anachokifanya si sahihi ili mradi tu na wewe upate tonge la ugali.
Kwa hakika nimesikitika sana kuhusu gazeti la Jamvi la habari kuandika habari ambazo ni uongo uliopitiliza kwa nia ya kumfanya Rais Magufuli aonekane anafanya mambo makubwa makubwa hapa nchini hususani kwenye suala zima la jeshi.
Kuna habari imeandika mambo haya kuhusu makomandoo wa Tanzania waliopatikana kipindi Rais Magufuli yupo madarakani, waliainisha sifa zao kama ifuatavyo;
1)Hawawezi kudhurika hata kidogo wakipigwa panga au kitu chochote chenye ncha kali, huwa kinadunda tu na wakati mwingine kinapinda kabisa bila kumdhuru huyo Komando wala kumpa maumivu au alama ya aina yoyote ile.
2)Hawa makomando wakikupiga teke moja unakufa hapo hapo ila kama mtu mwenye mafunzo unazimia siku tatu.
3)Wanapiga mateke futi kumi na mbili.
4)Wanaweza kupiga teke moja watu kumi kwa mkupuo.
5)Wanaweza kukaa bila kula chochote kwa miezi mitatu bila kudhurika.
NB: Bora hili gazeti lifungiwe tu kama wanavyofungia magazeti mengine kwa kuandika taarifa za uongo.
Kitu pekee kilichobaki ni kumsifia Rais Magufuli hata kama anachokifanya si sahihi ili mradi tu na wewe upate tonge la ugali.
Kwa hakika nimesikitika sana kuhusu gazeti la Jamvi la habari kuandika habari ambazo ni uongo uliopitiliza kwa nia ya kumfanya Rais Magufuli aonekane anafanya mambo makubwa makubwa hapa nchini hususani kwenye suala zima la jeshi.
Kuna habari imeandika mambo haya kuhusu makomandoo wa Tanzania waliopatikana kipindi Rais Magufuli yupo madarakani, waliainisha sifa zao kama ifuatavyo;
1)Hawawezi kudhurika hata kidogo wakipigwa panga au kitu chochote chenye ncha kali, huwa kinadunda tu na wakati mwingine kinapinda kabisa bila kumdhuru huyo Komando wala kumpa maumivu au alama ya aina yoyote ile.
2)Hawa makomando wakikupiga teke moja unakufa hapo hapo ila kama mtu mwenye mafunzo unazimia siku tatu.
3)Wanapiga mateke futi kumi na mbili.
4)Wanaweza kupiga teke moja watu kumi kwa mkupuo.
5)Wanaweza kukaa bila kula chochote kwa miezi mitatu bila kudhurika.
NB: Bora hili gazeti lifungiwe tu kama wanavyofungia magazeti mengine kwa kuandika taarifa za uongo.