Gazeti la Jamhuri lalipoteza gazeti la Kubenea la Mwanahalisi

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,367
Wadau, amani iwe kwenu.

Hapo zama za kale kulikuwa na kijigazeti kimoja ambacho kilijiita Mwanahalisi. Kigazeti hicho kilibobea kwa udaku huku kikijificha kwenye chaka la kufanya uchunguzi. Kwa vile baadhi ya watu walikuwa wanashabikia sana udaku, kigazeti hicho kikajipatia umaarufu. Umaarufu huo ukawalewesha wamiliki wa kigazeti hicho.

Baada ya miaka kadhaa kupita, Bonge la Gazeti likaanzishwa kwenye kaya. Gazeti hilo ambalo lilipewa jina la Jamhuri likaanza kuwafumbua macho wana kaya na kuwabainisha zipi habari za uchunguzi na upi udaku. Kilichowafumbua macho wanakaya ni jinsi gazeti hilo la Jamhuri lilivyofichua njama zinazotumika bandarini kuiba mafuta huku wakitumia mchoro unaoelezea kila pahala ambapo mafuta yanachepushwa.

Kuona hivyo ndivyo wana kaya wakany'amua. Wakabaini zipi habari za uchunguzi na upi ni udaku. Kuanzia wakati huo, Mwanahalisi limepotezwa kabisa na Jamhuri linaendelea kupaa. Mwanahalisi limepotezwa na mmiliki wake Saed Kubenea hana ujanja tena. Amebaki anatweta twe twe twe tweeeee!
 
Siku zote wenye akili tulijua kuwa Mwanahalisi walikuwa wanaandika udaku. Kikwete aliwalea sana. Sidhani kama zama hizi za Hapa Kazi Tu wataendelea kutamba. Heko Jamhuri
 
Mwanahalisi halikuwa gazeti la kuandika habari za uchunguzi, Kubenea alikuwa anatafuta kuingia kwenye siasa,wananchi wetu siasa za uongo ndizo wanazipenda na kuzishabikia, Kubenea alibaini hilo mapema.
 
Siku zote wenye akili tulijua kuwa Mwanahalisi walikuwa wanaandika udaku. Kikwete aliwalea sana. Sidhani kama zama hizi za Hapa Kazi Tu wataendelea kutamba. Heko Jamhuri
Ni kama mtoa habari wa Mwanahalisi aliwa Dr. Slaa vile! Maana baada ya Slaa kuondoka Chadema, nalo limekwisha.
 
poleni kwa umbumbumbu wenu
tanzania kuna magazeti mawili tu.
mwanahalisi na mawio ingawa moja mmelifuta
na lazima myachukie kwa sababu ya kuandika ukweli hayo yaliyobaki ni kusfia tu
 
nimesoma aya ya kwanza nikaona una chuki na mwanahalisi.
Kwa ushauri sio lazima ulisome au kulitizama, tafuta gazeti unalolipenda ndio usome.
 
Si umeambiwa kuwa limepotezwa na Jamhuri! Yaani hakuna anayelinunua kabisa. Limebaki kuwa gazeti la kuzolea kinyesi mtoto anapojisaidia haja kubwa ama wengine wanatumia kufungia maandazi
Lilipofunguliwa, Kubenea akaongea kwa mbwembwe kwelikweli, kumbe makapi tupu.
 
Pmoja na yote hivi udaku hauko uhuru na habarleo ?

Mnajitekenya wenyewe Na kucheka wenyewe !
Magamba mnaangaika. Na maigizo! Mpaka kwenye taaluma za watuu?
 
nimesoma aya ya kwanza nikaona una chuki na mwanahalisi.
Kwa ushauri sio lazima ulisome au kulitizama, tafuta gazeti unalolipenda ndio usome.
Mbona wengi tuliosma hii mada, inaonekana kuongelea uhalisia? Au wewe ndo unachuki binafsi na mleta mada? Binafsi naungana na mleta mada kuwa Mwanahalisi sasa ni gazeti la kufungja mandazi.
 
Mbona wengi tuliosma hii mada, inaonekana kuongelea uhalisia? Au wewe ndo unachuki binafsi na mleta mada? Binafsi naungana na mleta mada kuwa Mwanahalisi sasa ni gazeti la kufungja mandazi.
kila mtu ana upeo wake wakuelewa na kuchambua jambo.
 
ngojeni niajiriwe na kubenea,mtaisoma namba. KUbenea i am very seriaous naitaji kazi hapo ofisni kwako,tafadhali maombi yangu kwako naomba uyapokee. niliwai kufanya mafunzo kwa vitendo hapo, niuipokelewa na alfred Lukasi, hakika, nilliva kiuandishi, kilichoi nipoteza ni baada kufungiwa nilipotea ila KUBENEA NIPE KAZI MAANA NAJUA WEWEupo busy na ubunge.
 
Chiki binafsi: taka habari yoyote iliyoandikwa na mwanahalisi ambayo ni udaku. Usiandike ki ushabiki. Mwanahalisi limeibua mambo mengi yenye tija kwa nchi mpaka kuhatarisha maisha ya waandishi. Rejea mgomo Wa madaktari name dokta ulimboka au rudi nyuma kidogo juu ya a list of shame. Hii ni mifano michache turn.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom