Nimepitia taarifa za kidogo cha mh. Mbunge Mtema, katika gazeti la habari leo si taarifa iliyopewa kipaumbele jambo ambalo nadhani si Sawa na hasa nikilinganisha na taarifa iliyopewa kipaumbele, taarifa ambayo haikuwa na uharaka wowote Kwani
1. Ni habari ya kawaida pamoja na yaliyoandikwa kuipa uzito. hapa nawakumbuka wastaafu wote hata walio vijijini.
2. Ni ya uchunguzi, so ingeelea kutafitiwa japo kwa leo, na ikaambatanishiwa na nyaraka kadhaa za utumishi wa umma zinazopelekea hali ngumu ya maisha kwa watumishi wasifanya ufisadi.
Kwa maoni yangu nashauri
1. Habari leo wajisahishe katika hili Kwani pamoja na mwelekeo wao kisiasi wakumbuke like ni gazeti la umma wa tz, linaendeshwa kwa kodi zetu, Kwani hata wasipouza litaendelea kuchapwa tu.
2. R. Mtema, marehemu sasa, Alikuwa mtanzania, Lakini mbunge wa JMT, hivyo ni msiba kitaifa, ni uungwana tukalia wote,
3. Ajali ile imechukua maisha ya watz wengine, Kama mlivyowahi jurist kipaumbele katika taarifa nyingine za aina hii, basi mngefanya vivyohivyo
4. Kofi zetu zinauma pamoja na madhira mnayotutendea nyie mlokabidhiwa dhamana ya utumishi wa umma.
Inasikitisha, mnaimba uzalendo, kuipenda nchi, kuwa wamoja ilihali ninyi mmejitenga na jamii ya watz. Naomba kwa hili tuwakumbushe Habari leo kwamba wamechemka.
Mkuu kuna gazeti lingine nalo la Majira limeamua kuandika wanachoita vita ya madaraka ndani ya chadema