The Informer
Senior Member
- Jun 14, 2010
- 119
- 29
Mimi mwenyewe nikiwa ni mwandishi wa habari, nimeshtushwa, nimeshangaa na kupigwa butwaa na kitendo cha gazeti la Tanzania Daima, ambalo linamilikiwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, kutumika kumsafisha Edward Lowassa.
Pamoja ni kweli kuwa Mbowe anasifika kwa kutoa uhuru kwa wahariri wake na huwa haingilii editorial independence ya newsroom, naona sasa gazeti hili limekwenda too far.
Tanzania Daima la leo Jumamosi Novemba 27, 2010, kina habari kwenye ukurasa wa mbele yenye kichwa cha habari: "Lowassa: Nimechoka kuzushiwa. * Mwanaye ajipanga kuchukua hatua za kisheria kujisafisha."
Kwenye habari hiyo, gazeti la Tanzania Daima kwa makusudi kabisa linamuita Lowassa Waziri Mkuu "mstaafu."
Huu ni upotoshaji wa makusudi kwani taifa zima linajua Lowassa kamwe hakustaafu, alilazimika kujiuzulu mwaka 2008 baada ya kuhusishwa na kashfa ya ufisadi ya Richmond.
Kitendo cha Tanzania Daima kumuita Lowassa kimakosa kwa makusudi kuwa ni Waziri Mkuu "mstaafu" kina lengo maalum ya kumuweka mwanasiasa huyu aliyechafuka kwenye kundi moja kama mawaziri wakuu wa zamani waliostaafu kiheshima kama Cleopa David Msuya, Salim Ahmed Salim, Joseph Warioba, John Malecela na Frederick Sumaye.
Ukweli utabaki palepale kuwa Lowassa ni waziri mkuu "aliyejiuzulu" kwa kashfa ya ufisadi na si "mstaafu."
Kwenye habari hiyo inayombeba waziwazi Lowassa, hakuna sehemu popote ambapo kashfa ya Richmond inatajwa wala mazingira ya Lowassa kutoka serikalini kuelezwa.
Badala yake, gazeti hili limetoa platform prominently kwenye ukurasa wa kwanza kwa Lowassa kueleza kuchoshwa kwake "kuzushiwa" mambo na kusisitiza kuwa yeye hajatoswa na Kikwete na wala alikuwa hataki nafasi yoyote ya uwaziri.
Pia, gazeti hilo limetumika kama mouthpiece kwa kutoa fursa ndefu kwa Lowassa kumtetea mtoto wake Frederick, ambaye aliripotiwa na gazeti la RAIA MWEMA la wiki hii kuwa anachunguzwa na polisi Uingereza kwa tuhuma za money laundering baada ya kununua nyumba huko UK yenye thamani ya shilingi bilioni 1/-.
Inaeleweka kuwa Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, Absalom Kibanda, ni rafiki wa karibu wa Lowassa na pia anafanya kazi kwenye magazine ya Lowassa inayoitwa UMOJA.
Hivi mmiliki wa Tanzania Daima, Freeman Mbowe, anaelewa kuwa gazeti lake limekuwa likitumika mara kwa mara kumsafisha Lowassa na swahiba wake Rostam Aziz?
Kama jibu ndiyo, kwa nini anaachia hali hii na kuendelea kuwa na Mhariri Mkuu Kibanda mwenye conflict of interest kwa kuwa pia ameajiriwa na Lowassa?
Pamoja ni kweli kuwa Mbowe anasifika kwa kutoa uhuru kwa wahariri wake na huwa haingilii editorial independence ya newsroom, naona sasa gazeti hili limekwenda too far.
Tanzania Daima la leo Jumamosi Novemba 27, 2010, kina habari kwenye ukurasa wa mbele yenye kichwa cha habari: "Lowassa: Nimechoka kuzushiwa. * Mwanaye ajipanga kuchukua hatua za kisheria kujisafisha."
Kwenye habari hiyo, gazeti la Tanzania Daima kwa makusudi kabisa linamuita Lowassa Waziri Mkuu "mstaafu."
Huu ni upotoshaji wa makusudi kwani taifa zima linajua Lowassa kamwe hakustaafu, alilazimika kujiuzulu mwaka 2008 baada ya kuhusishwa na kashfa ya ufisadi ya Richmond.
Kitendo cha Tanzania Daima kumuita Lowassa kimakosa kwa makusudi kuwa ni Waziri Mkuu "mstaafu" kina lengo maalum ya kumuweka mwanasiasa huyu aliyechafuka kwenye kundi moja kama mawaziri wakuu wa zamani waliostaafu kiheshima kama Cleopa David Msuya, Salim Ahmed Salim, Joseph Warioba, John Malecela na Frederick Sumaye.
Ukweli utabaki palepale kuwa Lowassa ni waziri mkuu "aliyejiuzulu" kwa kashfa ya ufisadi na si "mstaafu."
Kwenye habari hiyo inayombeba waziwazi Lowassa, hakuna sehemu popote ambapo kashfa ya Richmond inatajwa wala mazingira ya Lowassa kutoka serikalini kuelezwa.
Badala yake, gazeti hili limetoa platform prominently kwenye ukurasa wa kwanza kwa Lowassa kueleza kuchoshwa kwake "kuzushiwa" mambo na kusisitiza kuwa yeye hajatoswa na Kikwete na wala alikuwa hataki nafasi yoyote ya uwaziri.
Pia, gazeti hilo limetumika kama mouthpiece kwa kutoa fursa ndefu kwa Lowassa kumtetea mtoto wake Frederick, ambaye aliripotiwa na gazeti la RAIA MWEMA la wiki hii kuwa anachunguzwa na polisi Uingereza kwa tuhuma za money laundering baada ya kununua nyumba huko UK yenye thamani ya shilingi bilioni 1/-.
Inaeleweka kuwa Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, Absalom Kibanda, ni rafiki wa karibu wa Lowassa na pia anafanya kazi kwenye magazine ya Lowassa inayoitwa UMOJA.
Hivi mmiliki wa Tanzania Daima, Freeman Mbowe, anaelewa kuwa gazeti lake limekuwa likitumika mara kwa mara kumsafisha Lowassa na swahiba wake Rostam Aziz?
Kama jibu ndiyo, kwa nini anaachia hali hii na kuendelea kuwa na Mhariri Mkuu Kibanda mwenye conflict of interest kwa kuwa pia ameajiriwa na Lowassa?