Gazeti la Daily Mail yauita Uwanja wa Taifa Dsm kama "Nairobi City Stadium"

View attachment 541491

Gazeti kubwa Uingereza la Daily Mail limetangaza mechi ya Gor Mahia VS Everton mubashara kupitia tovuti Yake .

Kitu cha kushangaza ni kuuita uwanja wa Taifa wa Tanzania kama "Nairobi City Stadium" ,na sio kimakosa kwani wameuita hivyo mara zote walipoutaja . Je , unadhani tatizo ni nini hasa hadi makosa haya yanatokea ? Nani wakulaumiwa ?? Sportpesa Tanzania?Au sisi wenyewe kama nchi hatajaitambulisha vyema nje ya mipaka yetu.

Hawa Waingereza ina maana wakati wote hawajui kama Everton ipo Dar Es Salaam na si Nairobi?Hivi timu za Tanzania ilikuwaje sikadharau michuano hii na kuiachia Gor Mahia toka Kenya kuubeba ubingwa kiwepesi?Tunajambo la kujifunza


Endeleeni kujifunza mkimaliza elimu sisi tayari tuko mbali
 
Kwa nini isiwe umbumbu wa Mwandishi, wame report kila sehemu kuwa Everton imewasili Dar es salaam, na kwamba watacheza mechi na Goal Mahia toka Kenya Dar es salaam....

Hata kama ange google kidogo tu angekutana na habari nyingi juu ya mechi kuchezwa Uwanja wa Taifa Dar es salaam..
Balozi atafanya nini katika hili?

Wazungu sio Malaika, wapo Mbumbumbu wa kiwango cha rami!!
Vitu vingi sana vya muhimu vya Tanzania huwezi kuvipata kwenye google, ma blog mengi sana waandishi wake elimu hakuna, blog nying za Tanzania zimejaa mapenzi, na siasa na udaku halafu taarifa nyingi zinazo ihusu Tanzania zime andikwa kiswahili, hao wazungu walikuwa hawana mda wa kutafuta google then wai translate..



Tanzania mlisha fail kitambo sana hamna mnalo liweza na hakuna mtakalo kuja kuliweza...

Usije ukashangaa Somalia imeizidi Tanzania kiuchumi...
 
Hili ndio tatizo la waandishi wa habari wasioenda field. Wao wanadokoa habari huku na kule wakiwa nyuma ya keyboard...
 
kitu nilochojifunza nikuwa waandishi wote duniani akili zao zinafanana wewe unawezaje ukariport taarifa wakati hauko sure na sehemu habari iloyopo? kwa maana hiyo wao walijilidhisha.kuwa everton wapo kenya

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
 
Sasa kama hatujitangazi kimataifa unadhani itakuaje, Vyombo vyetu vya habari vinaishia humuhumu ndani
 
Simba na Yanga nao ni wa kulaumiwa sana.

Walifanya uzembe sana kuwaachia hao Wakenya wakachukua ubingwa wa michuano ya sportpesa ndani ya ardhi yetu hayo ndio matokeo yake.
 
View attachment 541491

Gazeti kubwa Uingereza la Daily Mail limetangaza mechi ya Gor Mahia VS Everton mubashara kupitia tovuti Yake .

Kitu cha kushangaza ni kuuita uwanja wa Taifa wa Tanzania kama "Nairobi City Stadium" ,na sio kimakosa kwani wameuita hivyo mara zote walipoutaja . Je , unadhani tatizo ni nini hasa hadi makosa haya yanatokea ? Nani wakulaumiwa ?? Sportpesa Tanzania?Au sisi wenyewe kama nchi hatajaitambulisha vyema nje ya mipaka yetu.

Hawa Waingereza ina maana wakati wote hawajui kama Everton ipo Dar Es Salaam na si Nairobi?Hivi timu za Tanzania ilikuwaje sikadharau michuano hii na kuiachia Gor Mahia toka Kenya kuubeba ubingwa kiwepesi?Tunajambo la kujifunza
Hakuna wakulaumiwa ila hao waandishi waledi wao ni wa Chini hawajui KAZI yao ndio maana kuna MTU aliwahi kusema sikuhizi hakuna waandishi kuna mashirawadu. Mwandishi / Mwana habari kama Chars hilari wabobevu hawawezi kukurupuka hiyo. Jana nimeona kwenye mitandao nimeona pia wanaliita Jiji la DSM fishing Village na Baadae wakabadilisha.. Ni wakuwapuuza tu watarekebisha wenyewe.

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
Tunalaumiwa watanzania kwa uvivu wa kutafuta taarifa na maarifa...
Pia Tunalaumiwa kwa kuishi kama tuko kijijini katikati ya dunia iliyofungua milango wazi.

Makosa mawili yaliyofanywa na gazeti hili la Kiingereza kwa Mujibu wa vyanzo nilivyoviona jf.
1:Dar es Salaam kuitwa kijiji cha wavuvi badala ya Jiji la Dar es Salaam.
Ikumbukwe Dar es Salaam iko mbele ya Nairobi na ni ya kwanza Afrika nzima kwa majiji yote Afrika kwa kukua. Hao waingereza ilikuwa ni heshima kwetu kuwakosoa.
Top 20 Fastest Growing African Cities | Africa Strictly Business

2:Mechi Kati ya Gol Mahia V/S Everton ilichezewa uwanja wa Nairobi wakati dunia nzima akiwemo na kocha wa Everton Ronald Komando akihojiwa hukohuko England alisema anaenda tanzania na anaenda kushindana ili ashinde.

Nilitegemea hiki kifanyike...
Badala ya kulalamikia JF tungejiorganize tunaenda kufungua accounts kwenye gazeti lao na kucomment chini ya ile habr makosa waliofanya.
Ikiwezekana kuwatumia emails kama watanzania aggressive tuliomakini.

Utauliza kwa nini mimi sikufanya hivyo. Kwa sababu mimi ni mtanzania huyohuyo anaelalamikiwa ktk hrkt za kajitoa huko kwenye team malalamiko.
 
Vitu vingi sana vya muhimu vya Tanzania huwezi kuvipata kwenye google, ma blog mengi sana waandishi wake elimu hakuna, blog nying za Tanzania zimejaa mapenzi, na siasa na udaku halafu taarifa nyingi zinazo ihusu Tanzania zime andikwa kiswahili, hao wazungu walikuwa hawana mda wa kutafuta google then wai translate..



Tanzania mlisha fail kitambo sana hamna mnalo liweza na hakuna mtakalo kuja kuliweza...

Usije ukashangaa Somalia imeizidi Tanzania kiuchumi...
Kuhusu ujio wa Everton sio kweli Mkuu, hata ukienda website ya BBC (sio ya kiswahili) walikua wana report habari ya Everton toka wanapanda ndege kwao mpaka wanashuka Dar!
Media moja ika report Everton tayari imewasiri kijiji cha Uvuvi cha Dar es salaam!

Na kwa taarifa yako hawa waandishi wanao report hizo habari Wamekuja na Team hapa Bongo, na wengine walitangulia Dar es salaam.

Umesahau Samatta anachukua Tuzo ya Africa walim report kama Raia wa Congo, na wengine kama Angola.....sasa mwandishi kama huyu angetumia Dakika 5 tu kwa google, angejua Samatta ni RAIA wa nchi gani, lakini yeye aliandika kama alivyofikiri kichwani, sasa mwandishi wa kizungu kama huyu na wale waloutaja uwanja wa Taifa kama wa Nairobi, ni Mambumbumbu tu, Wazungu sio Malaika!
Wapo Vilaza wa kutupwa wanaoamini Africa ni nchi moja.
 
Tanzania haijulikan ni nchi ya wap. ...sasa ili kutowapa shida wasomaji wake ndo maana wanatafuta nchi angalau inajulikana kama Kenya, ndo maana vitu vingi vizuri vinatajwa vipo kenya ili kutoshusha thamani ya ivyo vitu

Sent from my TECNO-L8Plus using JamiiForums mobile app
Waache upuuzi, mbona boss wa ACACIA hakutua Nairobi?
 
Hili gazeti lingeshtakiwa kwa kutokuwa makini na kazi yao. Kwanza linachochea chuki
 
Hawaijui Africa
Wakenya ni mda mrefu walikuwa wanatembelea nyota ya Tanzania.ikumbukukwe kuwa kwa mda mrefu sasa kenya inajulikana ndiyo nchi pekee ya afrika mashariki na tz wanaitambulisha kama mkoa.
 
kumbe waandishi wa habari wa ovyo ovyo hawapo clouds na efm tuu, hata uingereza kumbe shazi. hii tasnia ya habari inahitaji nyongeza ya kitu ili kuimprove
Na wale waliotangaza trump kampongeza magu nadhani pia wapo clouds!ni vilaza Namba moja

Sent from my TECNO-Y6 using JamiiForums mobile app
 
Swali zuri kwa great thinkers....Tatizo vituo vya taifa vya utangazaji vyenyewe vipo busy kuonyesha matukio kama chereko chereko na mambo mengine yasiyo na faida.

sent from my Makinikia 7 using jamiiForums mobile app

Hivi tbc walionyesha pambano hilo??
Ni tukio/shindano la kibinafsi hivyo television ya taifa haihusiki mpaka labda ambapo wangelipwa

Sportspesa ndo kila kitu
 
Hilo gazeti hovyo kabisa jana wameliita Dar kuwa ni FISHING VILLAGE , kumbe waandishi wavivu siyo tu akina Salva ata huku wapo wengi tu . Aya bana wazee wa fishing village endeleeni kuvua makenikia.
Unajua kwenye map mwananyamala yote ni bwawa kubwa..
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom