Zinedine
JF-Expert Member
- Apr 9, 2011
- 1,187
- 694
Mkuu Zimmerman, mbona kwenye habari yako hakuna sehemu yoyote waliotajwa wakristo kama walengwa sasa hawa wenzio hizi comments zao zinatoka wapi? Mbona wasio waislamu ni zaidi ya wakristo, tena iliyolengwa ni Serikali, je nyie wakristo mnaepingana na ulichoposti kwa mujibu wa Annur ni Serikali au ndo mnaowazuilia waislamu hata wakaazimia kufanya hivyo? read btn the lines plz!Ah Mukandara, sidhani kama ni muhimu kwenda kwenye arguments za Ukristo vs Uislam au Makristo vs Waislam kwenye hii thread. Nahisi wewe ni muumini wa dini ya kiislam reasonable, na kama ni hivyo ni lazima utakuwa unakubaliana na mimi kwamba lile gazeti la an-nuur wanavuka mipaka ya uhuru wa maoni kikatiba. Kama huwezi kuliona hilo basi hakuna tumaini kabisa miongoni mwa jamii ya watanzania wenzetu waislam. Kila muislam yeyote sensible anapaswa kukataa ideologies za hawa watu wa an-nuur. Hawako realistic, hawako kiamani, hawako kiislam. Hawatetei maslahi ya waislamu bali wanataka kutumia jukwaa la dini ya kiislamu kujijengea cheap popularity kwa migongo ya waislamu wachache wanaopandikizwa hisia za kujihisi wanaonewa na serikali au wakristo. Jamani mbona hii serikali ni yenu nyie waislam? na mbona wakristo ni ndugu zenu, jirani zenu, wanapanga kwenye nyumba zenu, mnapanga kwenye nyumba zao, wananunua kwenye maduka yenu na mnanunu kwenye maduka yao? Hamuoni kwamba hawa an-nuur si watu wema kwa pande zote mbili?