Gavana Ballali: Nini kinaendelea?

Dotori

JF-Expert Member
Nov 3, 2007
544
24
Wadau kuna mtu mwenye taarifa yoyote kuhusu gavana wetu wa Benki Kuu? Hivi bado anaumwa? Bado yuko US au kesharudi Dar? Ni muda mrefu, kumekuwa na umkimya sana kuhusu Mhe. Gavana ambaye ni mtu muhimu katika masuala ya fedha TZ.
Wadau ninaomba taarifa.
 
Mafisadi wote wanajulikana sehemu walipo,mmoja yupo Kenya,anaomba hifadhi,wengi waliobakia wapo hapa hapa Tanzania yetu,wengine walipotelea Marekani kwenda kusomea digrii ya ufisadi na wamerudi kusubiri zamu yao,wamekuwa kama Tai walioona mzoga hawachezi mbali na Tanzania yetu,maana haina mwenyewe.

Lakini huyu D BALLALI ambaye hatujui ukubwa wake kimadaraka mpaka hata Serikali ya CCM haiwezi kumrejesha kwa kuwa hajulikani alipo! Mimi nadhani tuwaulize wale wote ambao leo wanarudisha pesa kwa mlango wa nyuma na Serikali inakubali bila hata kuwaweka magereza, ili kupata ukweli namna walivyozipata hizo pesa. Kwanini tunakubali kuwa kimya kiasi hiki, tusimuulize huyu bwana sifa ni nini kinachosababisha Ballali kushindwa kumrejesha nchini kujibu kesi yake.

Watanzania wangapi wamekufa,wamerejeshwa na wengine hata kutolewa na kupelekwa nje ya nchi kushtakiwa, kwanini huyu Ballali mtanzania mwenzetu inakuwa ni kigeu geu kwa Serikali!.
Sasa naamini Ballali,Rais Mstaafu B W M na J M K NA C C M yao wana kesi ya kujibu, na shahidi namba moja ni Ballali.

Watanzania wa ndani na mliopo nje tushirikiane kumtafuta huyu Balali mwenye siri nzito tumrejeshe kwa njia ya umoja wa mataifa,la muhimu tujue yupo wapi, kama yupo Afghanistan tumuombe BUSH, KWA NI YEYE TU anayeweza kufika hapo,kweli nawaambia kama sisi wenyewe watanzania hatutakuwa tayari kuona umuhimu wa Balali kurejeshwa nchini ili aje kuwataja Mafisadi wenye kinga basi tumekwisha kwani ni kila baada ya miaka mitano wanazaliwa si chini ya watano na baada ya miaka kumi anazaliwa mmoja ambaye naye anakinga.


BALLALIIIIIII ole wako TUKIKUPATA


AHSANTE
SEFF
 
I think issue ya Balali nilishawahi kusema hapa kuwa inachezwa kitu inaitwa delaying tacktick. Na wakati huo wnampa nafasi ya kuweka mambo sawa. Je hamuoni munkari unapoa. Balali akirudi wataanguka wengi. Hivyo they want him a way. Hivi kweli kwa kasha nzito kama hiyo Bush alpokuja Kikwete angekua serious angemuambia Mr kichaka kuna jamaa kajichimbia kwako namhitaji, Within 24hrs Balali angekuwa Dsm. Lakini nothing is going on. TUMELIWA MCHANA KWEUPE!!
 
Watanzania wenzangu,samahani sana kama haya maswali yangu yatawaudhi,na hasa nyie mnaotumia kijiwe hiki,naomba majibu mazuri ili mpate faida ninayotaka kuwapa,katika maoni yangu,kwani nipo makini na haya matukio yanayotia aibu kwa nchi yetu, na huku viongozi wetu wakiitana mashujaa kwa ufisadi wanaoufanyia rasimali zetu, na huku wakilindwa na katiba yao walioiweka kwa faida yao,na huku wapambe wao wakisherehekea na kuwaunga mkono na kuwapongeza,wasichokijua kwasababu viongozi wetu wamevaa ngozi ya kondoo kumbe ni chui wasiostahili hata kuwepo katika mbuga zetu za wanyama.Naomba kurudi ktk mada yangu ya maswali kama nilivyowaomba hapo juu.
maswali yangu ni haya-
1-Hii Tanzania ni nchi ya watanzania au shamba la viongozi.(wajanja,mafisadi)
2- Kama ni nchi,Nani anawajibika kuhakikisha rasilimali za nchi yetu hazipotei katika mikono ya hao tunaowaita viongozi.
3-Inawezekana watanzania hawana sababu ya kulinda mali na rasilimali za nchiyao .je Kwa kukosa uzalendo wa nchi yao?au...
4-Ina wezekana hali hii ya tulio nayo sisi wananchi kuwa kimya kiasi hiki,na huku mafisadi waliobakia madarakani wakiwapongeza wenzao waliobainika. je ni sababu tosha iliyotufanya kutawaliwa na kuwa watumwa katika enzi za wakoloni?
5-Uzuzu na ujinga tulionao sisi raia wema wa nchi hii ni kweli ndio sababu ya kuwepo viongozi wezi na mafisadi majasiri.
6-Kama Rais wa nchi tunayemtegemea kuwa mlinzi wa mali na Rasilimali anampongeza fisadi kwa kujiuzulu,yeye ataitwa nani?
7-Ni ngazi gani ya madaraka serikalini itawajibika ikiwa Ballali atafia nje ya nchi kabla hajatoa maelezo ya tuhuma zinazomkabili?
8-Wezi,Majambazi na Mafisadi. Ni nani aliye na afadhali kati ya hawa.
9-Je tunasababu ya kumuuliza Rais wa nchi hii ya Tanzania, anafahamu nini kuhusu Ballali? ili tupate maoni yake.
10-MR&Mrs BWM,mali zao zinatisha,wametumia majina ya watu wengine, mzee wetu kingunge usiseme,na kinjeketile wake wanatisha,Lowasa huko Arusha inatisha jamaa ana nyumba kama si chini ya 30, zote hazipo kwa jina lake zipo kwa majina ya watu wake wakaribu. Sumaye ndio usiseme na la kutisha zaidi amepata digrii ya kuja kutumaliza. swali- Kwasababu hatuna uwezo wa kuwashtaki kwa kuwa hawa jamaa wapo juu ya sheria na katiba
JE TUWASEMEHE AU TUSUBIRI mpaka hapo Upinzani utakapochukua madaraka?
11-Watanzania wenzangu BWM YUPO Kenya na Kibarua kimeisha. Maovu Lukuki,ya ufisadi yanamuandama, Anahaki ya kutumia KINGA ILI ASISHTAKIWE? ILI UKWELI NA UWAZI UWEPO.
12- WATANZANIA tunawezaaaaa! kutamka kuwa sasa basi kama alivyothubutu mama Ana Kilango alipokuwa Bungeni?
Kwa baraka zenu naomba majibu yenye kuleta matumaini
Ahsanteni
ni seff
 
Mafisadi wote wanajulikana sehemu walipo,mmoja yupo Kenya,anaomba hifadhi,wengi waliobakia wapo hapa hapa Tanzania yetu,wengine walipotelea Marekani kwenda kusomea digrii ya ufisadi na wamerudi kusubiri zamu yao,wamekuwa kama Tai walioona mzoga hawachezi mbali na Tanzania yetu,maana haina mwenyewe.

Lakini huyu D BALLALI ambaye hatujui ukubwa wake kimadaraka mpaka hata Serikali ya CCM haiwezi kumrejesha kwa kuwa hajulikani alipo! Mimi nadhani tuwaulize wale wote ambao leo wanarudisha pesa kwa mlango wa nyuma na Serikali inakubali bila hata kuwaweka magereza, ili kupata ukweli namna walivyozipata hizo pesa. Kwanini tunakubali kuwa kimya kiasi hiki, tusimuulize huyu bwana sifa ni nini kinachosababisha Ballali kushindwa kumrejesha nchini kujibu kesi yake.

Watanzania wangapi wamekufa,wamerejeshwa na wengine hata kutolewa na kupelekwa nje ya nchi kushtakiwa, kwanini huyu Ballali mtanzania mwenzetu inakuwa ni kigeu geu kwa Serikali!.
Sasa naamini Ballali,Rais Mstaafu B W M na J M K NA C C M yao wana kesi ya kujibu, na shahidi namba moja ni Ballali.

Watanzania wa ndani na mliopo nje tushirikiane kumtafuta huyu Balali mwenye siri nzito tumrejeshe kwa njia ya umoja wa mataifa,la muhimu tujue yupo wapi, kama yupo Afghanistan tumuombe BUSH, KWA NI YEYE TU anayeweza kufika hapo,kweli nawaambia kama sisi wenyewe watanzania hatutakuwa tayari kuona umuhimu wa Balali kurejeshwa nchini ili aje kuwataja Mafisadi wenye kinga basi tumekwisha kwani ni kila baada ya miaka mitano wanazaliwa si chini ya watano na baada ya miaka kumi anazaliwa mmoja ambaye naye anakinga.


BALLALIIIIIII ole wako TUKIKUPATA


AHSANTE
SEFF


Hili swali aulizwe JK na I'm sure anajua yuko wapi.
 
Kama hawa walipo hapa, hawa ambao kamati ya bunge imedhirisha bila shaka yeyote kuwa sio viogozi bora wapo hapa na hakuna cha maana wanachofanyiwa dhidi ya makosa yao itakuwa huyo Bw Balali asiyekuwa Tz?

Kama hawa waliopo Tz na kudhibitishwa rasmi wanaachwa wanaranda randa na kuvunja sheria za bunge kwa kulipinga na kulidhalilisha hadharani na kuitwa mashujaa itakuwa ni huyo Bw aliyeko mbali na nchi?

Kama hawa liopo nchni wanaitwa na kamati ya bunge alafu kwa ukaidi tu wanaikatalia na kujifanyia watakalo Bw Balali unamtakia nini?

Kama hawaliopa Tz wazi kabasia hadharani wamepata "ajali ya Kisisa tu .." Balali kapata ajali ya nini? Kibishara... ajali ya vitabu Kuto_Balance? sema chochote!!

Kunahaja ya kuedelea kujieleza?

Balali anakuwa Na nguvu ya kukaa "mafichoni" raha mstarehe kwa kuona kwani hao walikuwa huko nyumbani wamefanyiwa nini? Wanavinjari watakavyo kuanzia vyombo vya habari na mitaani kwa kila staili ya kutukuzwa kwa ushuja uliotukuka.
 
ballali yupo na naamini serikali inajua alipo na uwezo wa kumrudisha upo, ila sijui tuseme ni kiburi au viongozi wanaogopa vivuli vyao? hakuna atakayeamin eti ballali hawezekani kurudishwa nyumbani ahukumiwe kwa matendo yake, ila kinachoonekana ni uoga au self diffence ya baadhi ya viongozi wetu kwasababu hata ballali mwenyewealisema atakuja kutaja mafisadi wenzake, hapo unategemea atarudi kweli? labda tuwashinikize viongozi wetu arudishwe.
 
bf_fail.jpg
 
Jamani nauliza BALALI yuko wapi???. na serikari imechukua hatua gani?

Naunga na wewe kutaka kujua juu ya huyu jamaa, maana kimya kama vile hakuna kilichotokea. Among the possibilities are:
1. kafichwa au kajificha?? yeye ndiye alikuwa kiungo cha ufisadi wanaogopa atamwaga mchele kwenye kuku wengi.
2. Bado mgonjwa mahututi au kidogo afadhali?? kama ndio, yu na hali gani? yu hospitali au nyumbani? Tunaomba kuelezwa yuko wapi tukamjulie hali.
 
Wadau kuna mtu mwenye taarifa yoyote kuhusu gavana wetu wa Benki Kuu? Hivi bado anaumwa? Bado yuko US au kesharudi Dar? Ni muda mrefu, kumekuwa na umkimya sana kuhusu Mhe. Gavana ambaye ni mtu muhimu katika masuala ya fedha TZ.
Wadau ninaomba taarifa.
Cha kushangaza ni kwanini modes wameiweka hii kwenye vibweka vya wakubwa!
Binafsi nafikiri hili ni swali muhimu na sio simply "kibweka"
 
1. kafichwa au kajificha??

Uwezekano wa yeye kuwa amejificha sio mkubwa sana hivyo naamini kuwa amefichwa!

2. Bado mgonjwa mahututi au kidogo afadhali?? kama ndio, yu na hali gani? yu hospitali au nyumbani? Tunaomba kuelezwa yuko wapi tukamjulie hali.

Hii bado ni puzzle! Hali yake inaweza kuwa nzuri au bado mahututi lakini bado tusiweze kumfikia kwa vile amefichwa.
 
Inabidi tuandamane ili kuleta dhana halisi ya nguvu ya Umma na vyombo vyote vya habari vishikie bango hili suala la kuishinikiza serikali imlete Balali aje ajibu shutuma zake

Mnaonaje hilo wanaJF?
 
Inabidi tuandamane ili kuleta dhana halisi ya nguvu ya Umma na vyombo vyote vya habari vishikie bango hili suala la kuishinikiza serikali imlete Balali aje ajibu shutuma zake

Mmh, kushinikiza balali arudishwe peke yake ni kama kulilia mkia wakati ng'ombe mzima ni stahili yako! Tushinikize mafisadi wote wa EPA, RICHMOND na Import Support wawekwe ndani!
 
Ndugu zanguni mi nina imani kabisa hapa kuna kamchezo kachafu ka kuzugana ili mambo yapoe na wadanganyika ghadhabu zitulie. Balali anajulikana alipo ingekuwa JK ni mwenzetu kwenye kijiwe chetu angetutonya kidogo ingawa angejidai tusimwambie mtu...Si unajua mtu mzima akijamba huwezi kusema? utageuza lugha kuwa bomu limelia kumbe kachafua hali ya hewa. Siri ya urembo iko kwa balali na ndio maana wametulia iko siku atachomolewa huko aliko ndipo mchezo utakaponoga mwanawane!!!

Hata Big Ben nae huenda anazugazuga nadhani anatamani na Zimbabwe wafurushane ili ahamie huko kujifanya msuruhisi ili auwe sooo!!! lakini kitaeleweka tu. Tatizo Mzee wa Zengo la kupinda nae ameanza kutupotezea stimu za kazi anapodai kuwa mafisadi wana pesa sana kwa hiyo kuwashitaki inahitaji uangalifu sijui anawinda digidigi anaogopa atakurupuka au vipi anaturudisha enzi zile za kulala usingizi wa pono kuamshwa mpaka umwagiwe maji sikioni...Hatuko tayari kwa hilo.....Mi nawaambia historia itaandikwa mwaka huu eh!!
 
Ndugu zanguni mi nina imani kabisa hapa kuna kamchezo kachafu ka kuzugana ili mambo yapoe na wadanganyika ghadhabu zitulie. Balali anajulikana alipo ingekuwa JK ni mwenzetu kwenye kijiwe chetu angetutonya kidogo ingawa angejidai tusimwambie mtu...Si unajua mtu mzima akijamba huwezi kusema? utageuza lugha kuwa bomu limelia kumbe kachafua hali ya hewa. Siri ya urembo iko kwa balali na ndio maana wametulia iko siku atachomolewa huko aliko ndipo mchezo utakaponoga mwanawane!!!

Hata Big Ben nae huenda anazugazuga nadhani anatamani na Zimbabwe wafurushane ili ahamie huko kujifanya msuruhisi ili auwe sooo!!! lakini kitaeleweka tu. Tatizo Mzee wa Zengo la kupinda nae ameanza kutupotezea stimu za kazi anapodai kuwa mafisadi wana pesa sana kwa hiyo kuwashitaki inahitaji uangalifu sijui anawinda digidigi anaogopa atakurupuka au vipi anaturudisha enzi zile za kulala usingizi wa pono kuamshwa mpaka umwagiwe maji sikioni...Hatuko tayari kwa hilo.....Mi nawaambia historia itaandikwa mwaka huu eh!!

Ni kweli kwamba watanzania wengi sana wana uchungu na hayo mafisadi, na kama ni suala la kujichukulia sheria mkononi basi watu wangeweza hata kuwachoma moto.Tatizo jiulize kitu kimoja..kwamba akikamatwa kibaka wa kawaida basi watu watamzingira, watampiga, mwenye jiwe, tofali petroli wote watarushia hapo kutengeneza roast..?Ila hawa mafisadi, ambao wizi wao ndio una athari kubwa sana katika maisha yetu, basi ndio tunawakumbatia, kiasi cha kuwapa hata majukumu makubwa katika taasisi mbalimbali za umma na kijamii..hawa ndio watu ambao walitakiwa kuchukuliwa sheria kali mkononi, na wananchi wenye hasira, kuliko mhalifu wa aina yoyote ile.. Sasa tukirudi kwenye suala la kuwachukulia hatua za kisheria hawa jamaa, kwa kweli hapo ningependa niungane na bwana MIZEnguo iliyoPINDA, katika kubainisha ukweli kwamba hawa watu wana nguvu sana, either ya ushawishi, ama kifedha pia. Hii inapelekea kwenye uelekeo wa kutumia busara sana na utafiti wa hali ya juu wa vigezo sahihi vya kuwafikisha watu hawa mahakamani.. kwani ni mara ngapi watanzania tumeshuhudia kwamba serikali yetu tukufu inapoteza kesi katika hali ya uzembe usioelezeka? Hivyo basi ni muhimu vitafutwe vigezo sahihi ambavyo once tunawaingiza humo basi hatoki mtu..Hapa nguvu na technique za kisheria zitahitajika zaidi...Kawaida waswahili husema kwamba "mwenye nguvu mpishe", lakini hivi sasa itakuwa kumwekea kisiki huyu mwenye nguvu na alieshiba ili ajikwae hadi kudondoka ...kabsaaa..
 
Ni wakati sasa Rais Kikwete atuambie Balali yuko wapi, ni wajibu wetu kujua kwani ni amechangia sana katika kuifanya Tanzania imeng'enywe na mafisadi na anajua mbinu zote zilizotumika kuifilisi nchi. RAIS KIKWETE TUNAKUULIZA BALALI YUKO WAPI, KWA MAMLAKA TULIYOKUPA UNA UWEZO WA KUJUA/UNAPASWA KUJUA NA UNAJUA BALALI YUKO WAPI, TUELEZE!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom