Yaliyojiri Kuapishwa kwa Donald Trump, rais wa 45 wa Marekani

Satuuuu

JF-Expert Member
Dec 3, 2015
1,849
1,993
Wakuu habari yenu

Huu ni ukurasa huru kwa yeyote mwenye kufwatilia kinachoendelea USA ktk kuapishwa kwa Trump ili sisi tulio mbali na TV zetu tujue nini kinaendelea.

Rais mteule Donald J. Trump anatarajiwa kuapishwa rasmi kuwa rais wa 45 wa Marekani majira ya saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

=====

Inaugural address: Trump's full speech


As prepared for delivery

Chief Justice Roberts, President Carter, President Clinton, President Bush, President Obama, fellow Americans, and people of the world: Thank you.

We, the citizens of America, are now joined in a great national effort to rebuild our country and to restore its promise for all of our people.
Together, we will determine the course of America and the world for years to come.

We will face challenges. We will confront hardships. But we will get the job done.

Every four years, we gather on these steps to carry out the orderly and peaceful transfer of power, and we are grateful to President Obama and First Lady Michelle Obama for their gracious aid throughout this transition. They have been magnificent.

Today's ceremony, however, has very special meaning. Because today we are not merely transferring power from one administration to another, or from one party to another -- but we are transferring power from Washington, D.C. and giving it back to you, the American People.
Words from the past: Inauguration speech library

For too long, a small group in our nation's Capital has reaped the rewards of government while the people have borne the cost. Washington flourished -- but the people did not share in its wealth. Politicians prospered -- but the jobs left, and the factories closed.

The establishment protected itself, but not the citizens of our country. Their victories have not been your victories; their triumphs have not been your triumphs; and while they celebrated in our nation's capital, there was little to celebrate for struggling families all across our land.

That all changes -- starting right here, and right now, because this moment is your moment: it belongs to you.
It belongs to everyone gathered here today and everyone watching all across America. This is your day. This is your celebration. And this, the United States of America, is your country.

What truly matters is not which party controls our government, but whether our government is controlled by the people. January 20th 2017, will be remembered as the day the people became the rulers of this nation again. The forgotten men and women of our country will be forgotten no longer.

Everyone is listening to you now.

You came by the tens of millions to become part of a historic movement the likes of which the world has never seen before. At the center of this movement is a crucial conviction: that a nation exists to serve its citizens.

Americans want great schools for their children, safe neighborhoods for their families, and good jobs for themselves. These are the just and reasonable demands of a righteous public.

But for too many of our citizens, a different reality exists: Mothers and children trapped in poverty in our inner cities; rusted-out factories scattered like tombstones across the landscape of our nation; an education system flush with cash, but which leaves our young and beautiful students deprived of knowledge; and the crime and gangs and drugs that have stolen too many lives and robbed our country of so much unrealized potential.

This American carnage stops right here and stops right now.
We are one nation -- and their pain is our pain. Their dreams are our dreams; and their success will be our success. We share one heart, one home, and one glorious destiny.

The oath of office I take today is an oath of allegiance to all Americans.

For many decades, we've enriched foreign industry at the expense of American industry; subsidized the armies of other countries while allowing for the very sad depletion of our military; we've defended other nation's borders while refusing to defend our own; and spent trillions of dollars overseas while America's infrastructure has fallen into disrepair and decay.

We've made other countries rich while the wealth, strength, and confidence of our country has disappeared over the horizon.
One by one, the factories shuttered and left our shores, with not even a thought about the millions upon millions of American workers left behind.

The wealth of our middle class has been ripped from their homes and then redistributed across the entire world.
But that is the past. And now we are looking only to the future. We assembled here today are issuing a new decree to be heard in every city, in every foreign capital, and in every hall of power.

From this day forward, a new vision will govern our land.

From this moment on, it's going to be America First.

Every decision on trade, on taxes, on immigration, on foreign affairs, will be made to benefit American workers and American families. We must protect our borders from the ravages of other countries making our products, stealing our companies, and destroying our jobs. Protection will lead to great prosperity and strength.

I will fight for you with every breath in my body -- and I will never, ever let you down.
America will start winning again, winning like never before.

We will bring back our jobs. We will bring back our borders. We will bring back our wealth. And we will bring back our dreams.

We will build new roads, and highways, and bridges, and airports, and tunnels, and railways all across our wonderful nation.

We will get our people off of welfare and back to work -- rebuilding our country with American hands and American labor.
We will follow two simple rules: Buy American and hire American.

We will seek friendship and goodwill with the nations of the world -- but we do so with the understanding that it is the right of all nations to put their own interests first.

We do not seek to impose our way of life on anyone, but rather to let it shine as an example for everyone to follow.
We will reinforce old alliances and form new ones -- and unite the civilized world against radical Islamic terrorism, which we will eradicate completely from the face of the Earth.

At the bedrock of our politics will be a total allegiance to the United States of America, and through our loyalty to our country, we will rediscover our loyalty to each other.

When you open your heart to patriotism, there is no room for prejudice. The Bible tells us, "How good and pleasant it is when God's people live together in unity."

We must speak our minds openly, debate our disagreements honestly, but always pursue solidarity.
When America is united, America is totally unstoppable.
There should be no fear -- we are protected, and we will always be protected.
We will be protected by the great men and women of our military and law enforcement and, most importantly, we are protected by God.
Finally, we must think big and dream even bigger.

In America, we understand that a nation is only living as long as it is striving.
We will no longer accept politicians who are all talk and no action -- constantly complaining but never doing anything about it.
The time for empty talk is over. Now arrives the hour of action.

Do not let anyone tell you it cannot be done. No challenge can match the heart and fight and spirit of America.
We will not fail. Our country will thrive and prosper again.

We stand at the birth of a new millennium, ready to unlock the mysteries of space, to free the Earth from the miseries of disease, and to harness the energies, industries and technologies of tomorrow.

A new national pride will stir our souls, lift our sights, and heal our divisions.

It is time to remember that old wisdom our soldiers will never forget: that whether we are black or brown or white, we all bleed the same red blood of patriots, we all enjoy the same glorious freedoms, and we all salute the same great American Flag.

And whether a child is born in the urban sprawl of Detroit or the windswept plains of Nebraska, they look up at the same night sky, they fill their heart with the same dreams, and they are infused with the breath of life by the same almighty Creator.

So to all Americans, in every city near and far, small and large, from mountain to mountain, and from ocean to ocean, hear these words:
You will never be ignored again.

Your voice, your hopes, and your dreams will define our American destiny. And your courage and goodness and love will forever guide us along the way.

Together, We will make America strong again.

We will make wealthy again.

We will make America proud again.

We will make America safe again.

And yes, together, we will make America great again. Thank you. God bless you. And God bless America.

======

Kiswahili;

TRUMP: Jaji Mkuu Roberts, Rais Carter, Rais Clinton, Rais Bush, Rais Obama, Wamarekani wenzangu na watu wote duniani, asanteni sana. (MAKOFI)

Sisi, Wananchi wa Marekani, tunaungana katika juhudi za pamoja kitaifa kujenga nchi yetu na kutunza ahadi zake kwa watu wetu wote. (MAKOFI)

Pamoja, tutaamua hatima ya Marekani na dunia kwa ajili ya watu wote (na tutafanya hivyo) kwa miaka mingi ijayo. Tutakutana na changamoto, tutakutana na vikwazo, lakini tutahakikisha kazi inafanyika.

Kila miaka minne, tunakusanyika hapa kubadilishana madaraka kwa njia ya amani, na tunamshukuru sana Rais Obama na mke wa Rais Bi. Michele Obama kwa msaada wao mkubwa muda wote tulipokuwa tunafanya mchakato huo. Wamekuwa watu muhimu. Asanteni sana. (MAKOFI)

Pamoja na hayo, sherehe ya leo, ina maana kubwa, hatuko hapa kwa ajili tu ya kuhamisha madaraka kutoka utawala mmoja kwenda mwingine au kutoka chama kimoja kwenda chama kingine, lakini tuko hapa kuhamisha madaraka kutoka Washington D.C na kuyakabidhi kwenu, watu. (MAKOFI).

Kwa muda mrefu, kikundi kidogo kwenye mji mkuu wa nchi yetu kimekuwa kikivuna matunda ya serikali wakati watu wakibeba gharama. Washington iliendelea kuneemeka lakini watu hawakupata mgao wa utajiri wake. Wanasiasa walifaidika lakini kazi ziliondoka na viwanda vikafungwa. Mfumo wa Waanzilishi (The Establishments) ulijilinda na siyo kuwalinda wananchi wa nchi yetu. Ushindi (wa Waanzilishi) haukuwa ushindi wenu. Mafanikio yao hayakuwahi kuwa mafanikio yenu. Na wakati walikuwa wakisheherekea kwenye mji mkuu wa nchi yetu, familia zinazohangaika nchi nzima hazikuwa na cha kusheherekea. (MAKOFI)

Mabadiliko yote hayo yanaanzia hapa na yanaanza sasa hivi kwa sababu wakati huu ni wakati wenu na ni wakati unaomilikiwa na nyinyi. (MAKOFI)

TRUMP: Wakati huu unamilikiwa na kila mmoja aliyekusanyika hapa leo na kila mmoja anayetufuatilia akiwa sehemu yoyote hapa Marekani. Hii ni siku yenu. Hii ni sherehe yenu. Na hii, Marekani, ni nchi yenu. (MAKOFI).

Cha msingi siyo chama gani kinaongoza serikali yetu, cha msingi ni ikiwa serikali yetu inadhibitiwa na nyinyi, watu. (MAKOFI).

Tarehe 20 Januari 2017 itakumbukwa kama siku ambayo watu (Wa Marekani) walikuwa watawala wa taifa hili tena. (MAKOFI).

Wanaume na Wanawake wa nchi yetu hawatasahaulika tena. (MAKOFI).

Kila mmoja anawasikiliza hivi sasa. Mmekuja kwa wingi mno kwa makumi na mamilioni kuwa sehemu ya vuguvugu, mfano ambao dunia haikuwahi kuuona kabla. (MAKOFI).

Katikati ya vuguvugu hili kuna ahadi muhimu, kwamba taifa lipo kwa ajili ya kuwatumikia raia wake. Wamarekani wanahitaji shule bora kwa ajili ya watoto wao, majirani salama kwa ajili ya familia zao, kazi nzuri kwa ajili yao. Haya ni mahitaji halali na ya msingi ya watu sahihi na jamii sahihi.

Lakini sehemu kubwa ya watu wetu, wanakumbana na halisia tofauti: akina mama na watoto wameshikiliwa na umasikini ndani ya miji yetu; viwanda vilivyochakaa vimetapakaa kama makaburi kila kona ya nchi yetu; elimu yetu inatolewa kwa wenye pesa, jambo linaloacha wanafunzi wetu wadogo na wazuri wakinyimwa maarifa; na uhalifu na makundi ya kihalifu na madawa ya kulevya ambavyo vimeshachukua maisha ya watu wengi na kuiondolea nchi yetu nguvu kazi muhimu. Mabalaa hayo kwa Wamarekani yanasimamishwa mahali hapa na yanasimama sasa hivi. (MAKOFI)

Sisi ni taifa moja na maumivu yao ni maumivu yetu. Ndoto zao ni ndoto zetu. Na mafanikio yao yatakuwa mafanikio yetu. Tunashirikishana moyo mmoja, nyumba moja na matarajio ya aina moja. Kiapo cha Urais nilichokula leo ni kiapo cha utii kwa Wamarekani wote. (MAKOFI).

Kwa miongo mingi, tumekuwa tukitajirisha viwanda vya nje ya Marekani kwa gharama za viwanda vya Marekani; tumekuwa tukitoa ruzuku na kuyapa majeshi ya nchi nyingine, wakati tukiruhusu hali mbaya na ya kusikitisha kwa majeshi yetu. Tumekuwa tukilinda mipaka ya nchi nyingine na tukikataa kulinda mipaka yetu wenyewe. (MAKOFI).

Tumekuwa tukitumia trilioni na trilioni za dola za Marekani nje ya nchi yetu wakati miundombinu ya Marekani ikiwa imeanguka, kuharibika na kuoza. Tumekuwa tukizifanya nchi nyingine kuwa tajiri, wakati utajiri, uimara na kujiamini kwa nchi yetu kukipungua kwa kila namna.

Kimoja baada ya kingine, viwanda vikafungwa na vikaiacha ardhi yetu, bila hata kufikiria kuhusu mamilioni na mamilioni ya Wamarekani ambao walikuwa wanapotezewa kazi. Utajiri wa watu wa kati umeondolewa kutoka kwenye familia zao na kisha ukagawanywa katika nchi zote duniani. Lakini hayo yamepita. Na sasa, tunaangalia mbele tu. (MAKOFI).

TRUMP: Tumekusanyika hapa leo kutoa AMRI MPYA itakayosikika katika kila mji, katika kila mji mkuu wa nchi za Dunia yote, na katika kila sehemu yenye madaraka. Kuanzia leo kwenda mbele, dira mpya ndiyo itaongoza taifa letu. Kuanzia leo kwenda mbele, itakuwa ni Marekani kwanza, Marekani kwanza. (MAKOFI).

Kila maamuzi kuhusu biashara, kuhusu kodi, kuhusu uhamiaji, kuhusu mambo ya nje yatafanywa kuwanufaisha wafanyakazi wa Marekani na familia za Marekani. Lazima tulinde mipaka yetu dhidi ya mipango ya nchi nyingine kutengeneza bidhaa zetu, kuiba makampuni yetu na kuharibu kazi zetu. (MAKOFI).

Kujilinda kutapelekea tupate uimara na mafanikio makubwa. Nitawapigania kwa kila pumzi iliyomo kwenye mwili wangu. Na kamwe sitaawangusha. (MAKOFI).

Marekani itaanza kushinda tena, kushinda kuliko ilivyowahi kutokea. (MAKOFI).

Tutarudisha kazi zetu. Tutarudisha mipaka yetu. Tutarudisha utajiri wetu. Tutarudisha ndoto zetu. (MAKOFI).

Tutajenga njia mpya, na njia kuu na madaraja na viwanja vya ndege na mitaro na reli kila mahali katika nchi yetu kuu. Tutawatoa watu wetu kwenye matatizo na kuwarudisha wafanye kazi, kuijenga upya nchi yetu kwa mikono ya Wamarekani na Wafanyakazi wa Marekani. (MAKOFI).

Tutafuata kanuni mbili za kawaida; nunua Mmarekani na ajiri Mmarekani (Nunua bidhaa ya Marekani na toa ajira kwa Raia wa Marekani). (MAKOFI).

Tutatafuta marafiki na kuonesha nia njema kwa mataifa ya dunia, lakini tutafanya hivyo kwa kuelewa kwamba ni haki ya kila taifa kuweka mbele maslahi yake.

Hatutatafuta kuanzisha aina yetu ya maisha kwa taifa lolote, lakini badala yake kufanya maisha yetu yangare na kuwa mfano. Tutangara ili kila taifa lifuate mfano wetu. (MAKOFI).

Tutarejesha marafiki wa zamani na kukaribisha wapya na kuunganisha dunia iliyostaarabika dhidi ya Ugaidi wa Uislamu wa siasa kali, ambao tutauondoa katika uso wa dunia. (MAKOFI).

Katika kitovu cha siasa zetu kutakuwa na utii mkubwa kwa Marekani, na kupitia heshima kwa nchi yetu tutavumbua heshima kwa kila mmoja. Unapofungua moyo wako kwa ajili ya uzalendo, hakutakuwa na nafasi ya kuhujumiwa. (MAKOFI).

Biblia inatueleza namna ilivyo jambo jema pale watu wa Mungu wanapoishi pamoja katika muunganiko/muungano. Lazima tuseme yaliyomo katika fikra zetu kwa uwazi, tujadiliane mambo ambayo hatukubaliani kwa uaminifu, lakini muda wote tukilinda umoja wetu. Wakati Marekani inapoungana, hakuna awezaye kuisimamisha. (MAKOFI).

Hakupaswi kuwa na woga. Tunalindwa na siku zote tutalindwa. Tutalindwa na wanaume na wanawake wasio na mfano ambao wako kwenye majeshi yetu na vyombo vya dola. Na muhimu kuliko yote, tutalindwa na Mungu. (MAKOFI).

TRUMP: Mwisho, lazima tufikiri mbali na kuota ndoto kubwa zaidi. Marekani, tunafahamu kwamba taifa linaishi ikiwa tu linapambana kupata matokeo bora. Hatutaendelea kukubali wanasiasa ambao wanaongea bila vitendo, muda wote wanalalamika, lakini hawajawahi kufanya chochote ili kubadilisha kile wanachokilalamikia. (MAKOFI)

Muda wa mazungumzo hewa umekwisha. Sasa imefika saa ya vitendo. (MAKOFI).

Usiruhusu mtu yeyote akwambie kwamba haiwezi kufanyika. Hakuna changamoto inayoweza kuendana na jitihada na ari ya Marekani. Hatutashindwa. Nchi yetu itavuka na kushamiri tena.

Tunasimama wakati wa kuzaliwa kwa milennia mpya, tukiwa tayari kufungua majaribu ya anga, kuifanya dunia kuwa huru dhidi ya majanga ya magonjwa, na kujenga nishati, viwanda na teknolojia kwa ajili ya kesho. Tunu mpya za taifa zitakuwa ndani yetu, zitainua maono yetu na kuponya migawanyiko yetu.

Ni muda wa kukumbuka busara za zamani ambazo wanajeshi wetu hawawezi kusahau, kwamba hata kama sisi ni weusi au kijivu au weupe, sote tunavuja damu moja nyekundu ya wazalendo. (MAKOFI).

Sote tunafurahia uhuru wa kipekee na sote tunaipiga saluti, bendera moja kuu ya Marekani. (MAKOFI).

Na ikiwa mtoto amezaliwa katika eneo la Mjini la Detroit au maeneo yenye upepo mwingi huko Nebraska, wote wanaangalia anga moja ya usiku, wote wana ndoto moja, na wote wamepewa pumzi ya maisha na Muumbaji mmoja. (MAKOFI).

Kwa hiyo, kwa Wamarekani wote katika kila mji karibu na mbali, mdogo na mkubwa, mlima kwa mlima, bahari kwa bahari, sikilizeni maneno haya. Hamtadharauliwa tena. (MAKOFI).

Sauti zenu, matumaini yenu na ndoto zenu, zitaeleza ukuu wa Marekani yetu. Na ujasiri wenu na uzuri wenu na mapenzi yenu vitatuongoza siku zote katika njia tunayopita. (MAKOFI).

Pamoja, tutaifanya Marekani kuwa imara tena. Tutaifanya Marekani kuwa tajiri tena. Tutaifanya Amerika kujivuna tena. Tutaifanya Marekani kuwa salama tena. Na ndiyo, pamoja tutaifanya Marekani kuwa Kuu tena. (MAKOFI).

Asanteni sana. Mungu awabariki. Na Mungu aibariki Marekani. (MAKOFI).

[HASHTAG]#Note[/HASHTAG]: Nimeifasiri baada ya maombi mengi. Nawatakia mjadala mwema.

Baruapepe: juliusmtatiro@yahoo.com, Whatsup: +255 787 536759.
 
Kwa Picha: Sherehe ya kuapishwa kwa Donald Trump
Mamia ya maelfu ya raia wahudhuria kuonyesha umoja wao na wengine wakipinga huku Donald Trump akiapishwa kuwa rais wa Marekani.

_93722273_obama.jpg

Aliyekuwa rais wa Marekani Barrack Obama akipunga mkono kusema kwaheri wakati alipoingia katika ndege na kuondoka, huku Donald Trump na mkewe wakirudi katika jengo la Capitol Hill

_93722038_mediaitem93722037.jpg

Rais Donald Trump kushoto na rais wa zamani Barrack Obama wakiwa na wake zao nyuma yao, wakati wa kuimbwa kwa wimbo wa taifa

_93721915_mediaitem93721914.jpg

Jackie Evancho, mshiriki wa shindano la Got Talent ndiye aliyeimba wimbo wa taifa wa Marekani katika sherehe hizo

_93720821_mediaitem93720820.jpg

Raia wa Marekani waliofurahia kuapishwa kwa Donald Trump wakiwa wamevalia nguo za bendera ya Marekani

_93720159_mediaitem93720158.jpg

Rais Trump akipongezwa na familia yake baada ya kula kiapo huku aliyekuwa rais Obama na mkewe wakitazama

_93720078_mediaitem93720076.jpg

Donald Trump baada ya kuapishwa kuwa rais wa 45 wa Marekani

_93688000_mediaitem93687999.jpg

Makamu wa rais Mike Pence akiapishwa huku mkewe Karen Pence akimuangalia

_93721746_8cbc066c-e987-4f59-a53d-86bb388250ab.jpg

Hillary Clinton, ambaye alishindwa na Donald Trump, akimnong;onezea kwa masikio yake aliyekuwa rais wa zamani George Bush kabla ya kuapishwa kwa Trump

_93721981_mediaitem93721980.jpg
Vyombo vya habari vyajianda kabla ya kuanza kwa sherehe ya kumuapisha Donald Trump katika mvua

_93722075_mediaitem93722074.jpg

Waandamanji wanaompiga Donald Trump wakongamana karibu na eneo linalokaribia lango la kuingia eneo la capitol hill

_93722232_mediaitem93722231.jpg

Msafara uliombeba Barrack Obama na Donald Trump waingia katika barabara ya Pennsylvania kuelekea Capitol hill kwa sherehe ya kuapishwa kwa Trump

_93689792_mediaitem93685688.jpg

Ni tabasamu kwa wapiga picha wakati ambapo Barrack Obama na Michelle wanamkaribisha Donald Trump na Melania Trump katika ikulu ya Whitehouse kwa chai asubuhi ya siku yakuapishwa.

_93689793_mediaitem93685685.jpg

Watazamaji wakongaman karibu na Capitol hill licha ya baridi na mvua ili kushuhudia kuapishwa kwa rais Trump

_93690446_oval_getty.jpg

Barack Obama akiondoka katika ikulu ya Whitehouse kwa mara ya mwisho akikamilisha utawala wake wa kipindi cha miaka minane kama rais wa Marekani.

_93690448_getty_nohillary.jpg

Kwa wengine ilikuwa furaha isio kifani na ukumbusho wa ushindi wa Donald Trump katika uchaguzi uliopita dhidi ya Hillary Clinton

_93690450_trump_nose_getty.jpg

Lakini maelfu ya waandamani walihudhuria kuonyesha hasira zao wakisema ''sio rais wangu''

_93690452_getty_dragged.jpg

Waandamanji walijaribu kufunga njia kuingia katika eneo la Capitol ambapo rais Trump aliapishwa raasmi kuwa rais wa 45 wa Marekani
 
Tendo la kuapishwa kwa rais huyu mteule wa marekani linaendelea muda huu live Azam two
Ngoja tuone leo ataieleza nini dunia,Najua Mange yupo na joto la juu kabisa muda huu.
 
Donald Trump Singers Fear Blackballing If They Perform at Inauguration.jpg


Hakika siku iliyokuwa inasubiriwa dunia nzima imewadia, ni leo Rais mteule wa marekani anaapishwa kuwa Rais wa Taifa hilo kubwa duniani. Trump atakuwa Rais wa 45 wa taifa hilo kubwa duniani.

Trump anachukua hatamu kutoka kwa Rais Barack Obama saa mbili usiku Afrika Mashariki. Atakula kiapo muda mfupi kabla ya saa mbili
Atatoa hotuba na kisha aongoze msafara kuelekea White House
Wafuasi wake wanatarajiwa kukusanyika kwa wingi barabara za Washington.

Tuwe pamoja katika tukio hili kubwa, karibu.
wp_ss_20170120_0001.png



Sherehe ya kuapisha itaanza saa 17:30 kwa saa za afrika mashariki.

UPDATE 17:15
Trump na Obama watakunywa kahawa pamoja WH wakisubiri wasaa uwadie.

UPDATE 18:00
Trump akaribishwa WH na Obama, wameingia ndani kunywa kahawa

UPDATE 18:08
RAIS George Bush Jr na mkewe tayari wameshawasili US capitol kuhudhuria sherehe ya kuapishwa Trump

UPDATE 18:18
Hillary Clinton na Bill Clintol wamewasili US capitol
 
Back
Top Bottom