Gang Chomba
JF-Expert Member
- Feb 29, 2008
- 20,301
- 4,681
Aliyepata kuwa dikteta wa kiungo barani europa kwa Miaka ya hivi karibuni Ivan Rhino Genarro Gatusso amefungua kinywa chake na kusema kuwa anataka kujua mustakabali wa kupata namba katika kikosi cha kwanza hapa Milan ama la basi atatimka klabuni hapa.
kauli hiyo imetolewa kwa masikitiko makubwa na kiungo huyo nguli mwenye amsha amsha za kutosha awapo dimbani kufuatia kitendo cha kocha Leonaldo kuendelea kutomtumia kamanda huyo aliyepata kuwa pia kipenzi cha washabiki wa rossonelli.
Hakuna taarifa rasmi zilizobainisha kuwa ni sababu gani haswa imepelekea Gattuso kuwa benchi kwa mechi nyingi.
Lakini kuna habari zisizo za uhakika sinadokeza kuwa kocha Leonardo ameamua kutokumtumia kiungo huyo kutokana na kitendo chake cha utovu wa nidhamu alichokionyesha ktk mechi ya wapinzani wa jadi maarufu kama dela madoninna kati ya Rosonelli na Nerazurri ambapo Milan walifungwa goli 4-0 nyumbani kwake na Inter.
Lakini pia duru za soka zinadokeza kuwa mfumo unaotumika sasa wa kuwasimamisha washambuliaji wawili mbele ndo kikwazo cha kupata namba kwa Rhino. Wachambuzi wa soka pia wametanabaisha kuwa tangu kocha Leo alipoanza kuutumia mfumo huu Milan imekuwa na mfululizo wa ushindi ama droo kitu ambacho ndio milan wanachokitaka kwa sasa.
Najihisi kama ni kiongozi muasi kwa jinsi ninavyofanyiwa hapa Milan...hakika naumia sana pale ninapoona mashuka makuubwa yaliyoandikwa maneno ya kunisifu na kunitukuza toka kwa washabiki wenye imani nami lakini nayasoma hayo nikiwa nimekaa benchi...alikaririwa Gattuso kwa uchungu.
Lakini kwa sisi tunaoijua Milan tunaona wazi kuwa Leonaldo atakutana na upinzani mkali toka kwa washabiki wa Milan kufuatia kitendo chake cha kumuweka benchi mshambuliaji anayeaminika kuwa ni hatari Suppa Pippo Fillipo Inzaghi.
Hakuna uthibitisho mpk sasa unaoonyesha ni lini ama ni wapi Pippo aliwahi kumpiga chenga, ama tobo, ama kisigino beki kisha akafunga, lakini inaaminika kuwa Pippo ndiye mshambuliaji hatari na mabeki huwa makini kwa kipindi chote awapo uwanjani.
Leonaldo ameonyesha imani kwa washambuliaji Alesandro Pato na marco Boriello na amekuwa akimtumia kwa nadra sana mshambuliaji huyo kipenzi cha watu wa milan aliyejiunga na klabu hiyo mwaka 2000 akitokea Bianconelli ama Juve.
Akiongelea matukio haya hivi karibuni makamo wa rais wa klabu hiyo muheshimiwa Adriano Galliani amesema kuwa mambo yote haya yanatokea ni kwa sababu tu ya swala zima la wakati...
Milan ilianzishwa tarehe 16/dec/1898 na tangu hapo imebeba kombe la ulaya mara 7 na ndio klabu iliyobeba vikombe vingi vya kimataifa kuliko klabu yoyote hapa ulimwenguni.
'SFORZA MILAN'.
kauli hiyo imetolewa kwa masikitiko makubwa na kiungo huyo nguli mwenye amsha amsha za kutosha awapo dimbani kufuatia kitendo cha kocha Leonaldo kuendelea kutomtumia kamanda huyo aliyepata kuwa pia kipenzi cha washabiki wa rossonelli.
Hakuna taarifa rasmi zilizobainisha kuwa ni sababu gani haswa imepelekea Gattuso kuwa benchi kwa mechi nyingi.
Lakini kuna habari zisizo za uhakika sinadokeza kuwa kocha Leonardo ameamua kutokumtumia kiungo huyo kutokana na kitendo chake cha utovu wa nidhamu alichokionyesha ktk mechi ya wapinzani wa jadi maarufu kama dela madoninna kati ya Rosonelli na Nerazurri ambapo Milan walifungwa goli 4-0 nyumbani kwake na Inter.
Lakini pia duru za soka zinadokeza kuwa mfumo unaotumika sasa wa kuwasimamisha washambuliaji wawili mbele ndo kikwazo cha kupata namba kwa Rhino. Wachambuzi wa soka pia wametanabaisha kuwa tangu kocha Leo alipoanza kuutumia mfumo huu Milan imekuwa na mfululizo wa ushindi ama droo kitu ambacho ndio milan wanachokitaka kwa sasa.
Najihisi kama ni kiongozi muasi kwa jinsi ninavyofanyiwa hapa Milan...hakika naumia sana pale ninapoona mashuka makuubwa yaliyoandikwa maneno ya kunisifu na kunitukuza toka kwa washabiki wenye imani nami lakini nayasoma hayo nikiwa nimekaa benchi...alikaririwa Gattuso kwa uchungu.
Lakini kwa sisi tunaoijua Milan tunaona wazi kuwa Leonaldo atakutana na upinzani mkali toka kwa washabiki wa Milan kufuatia kitendo chake cha kumuweka benchi mshambuliaji anayeaminika kuwa ni hatari Suppa Pippo Fillipo Inzaghi.
Hakuna uthibitisho mpk sasa unaoonyesha ni lini ama ni wapi Pippo aliwahi kumpiga chenga, ama tobo, ama kisigino beki kisha akafunga, lakini inaaminika kuwa Pippo ndiye mshambuliaji hatari na mabeki huwa makini kwa kipindi chote awapo uwanjani.
Leonaldo ameonyesha imani kwa washambuliaji Alesandro Pato na marco Boriello na amekuwa akimtumia kwa nadra sana mshambuliaji huyo kipenzi cha watu wa milan aliyejiunga na klabu hiyo mwaka 2000 akitokea Bianconelli ama Juve.
Akiongelea matukio haya hivi karibuni makamo wa rais wa klabu hiyo muheshimiwa Adriano Galliani amesema kuwa mambo yote haya yanatokea ni kwa sababu tu ya swala zima la wakati...
Milan ilianzishwa tarehe 16/dec/1898 na tangu hapo imebeba kombe la ulaya mara 7 na ndio klabu iliyobeba vikombe vingi vya kimataifa kuliko klabu yoyote hapa ulimwenguni.
'SFORZA MILAN'.