GATUSSO: mnipange ama niondoke

Gang Chomba

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
20,301
4,681
Aliyepata kuwa dikteta wa kiungo barani europa kwa Miaka ya hivi karibuni Ivan Rhino Genarro Gatusso amefungua kinywa chake na kusema kuwa anataka kujua mustakabali wa kupata namba katika kikosi cha kwanza hapa Milan ama la basi atatimka klabuni hapa.
kauli hiyo imetolewa kwa masikitiko makubwa na kiungo huyo nguli mwenye amsha amsha za kutosha awapo dimbani kufuatia kitendo cha kocha Leonaldo kuendelea kutomtumia kamanda huyo aliyepata kuwa pia kipenzi cha washabiki wa rossonelli.
Hakuna taarifa rasmi zilizobainisha kuwa ni sababu gani haswa imepelekea Gattuso kuwa benchi kwa mechi nyingi.
Lakini kuna habari zisizo za uhakika sinadokeza kuwa kocha Leonardo ameamua kutokumtumia kiungo huyo kutokana na kitendo chake cha utovu wa nidhamu alichokionyesha ktk mechi ya wapinzani wa jadi maarufu kama dela madoninna kati ya Rosonelli na Nerazurri ambapo Milan walifungwa goli 4-0 nyumbani kwake na Inter.
Lakini pia duru za soka zinadokeza kuwa mfumo unaotumika sasa wa kuwasimamisha washambuliaji wawili mbele ndo kikwazo cha kupata namba kwa Rhino. Wachambuzi wa soka pia wametanabaisha kuwa tangu kocha Leo alipoanza kuutumia mfumo huu Milan imekuwa na mfululizo wa ushindi ama droo kitu ambacho ndio milan wanachokitaka kwa sasa.
Najihisi kama ni kiongozi muasi kwa jinsi ninavyofanyiwa hapa Milan...hakika naumia sana pale ninapoona mashuka makuubwa yaliyoandikwa maneno ya kunisifu na kunitukuza toka kwa washabiki wenye imani nami lakini nayasoma hayo nikiwa nimekaa benchi...alikaririwa Gattuso kwa uchungu.
Lakini kwa sisi tunaoijua Milan tunaona wazi kuwa Leonaldo atakutana na upinzani mkali toka kwa washabiki wa Milan kufuatia kitendo chake cha kumuweka benchi mshambuliaji anayeaminika kuwa ni hatari Suppa Pippo Fillipo Inzaghi.
Hakuna uthibitisho mpk sasa unaoonyesha ni lini ama ni wapi Pippo aliwahi kumpiga chenga, ama tobo, ama kisigino beki kisha akafunga, lakini inaaminika kuwa Pippo ndiye mshambuliaji hatari na mabeki huwa makini kwa kipindi chote awapo uwanjani.
Leonaldo ameonyesha imani kwa washambuliaji Alesandro Pato na marco Boriello na amekuwa akimtumia kwa nadra sana mshambuliaji huyo kipenzi cha watu wa milan aliyejiunga na klabu hiyo mwaka 2000 akitokea Bianconelli ama Juve.
Akiongelea matukio haya hivi karibuni makamo wa rais wa klabu hiyo muheshimiwa Adriano Galliani amesema kuwa mambo yote haya yanatokea ni kwa sababu tu ya swala zima la wakati...
Milan ilianzishwa tarehe 16/dec/1898 na tangu hapo imebeba kombe la ulaya mara 7 na ndio klabu iliyobeba vikombe vingi vya kimataifa kuliko klabu yoyote hapa ulimwenguni.
'SFORZA MILAN'.
 
uhasama na makocha una spoil sana viwango vya wachezaji.

si mnakumbuka kilichomkumba rivaldo akiwa ac milan?
kiwango alikuwa nacho kilikuwa ni cha juu sana,
lakini kocha akasema hakumpeleka hapo klabuni,
ila alikuwa amepelekwa na rais wa klabu,
kwa hiyo rais wa club ndio ampange...
dogo akakaa benchi,
mwisho wa siku kiwango kikaporomoka na leo sijui hata aliko.
 
lakini jamaa anaonekana kweli mbabe sana uwanjani, rafu nyingi sana.
 
Hivi na flamini nae vipi kama mtu mzima Gattuso hachezi yeye inakuwaje? Au ndo anacheza badala ya Gattusso?
 
Hivi na flamini nae vipi kama mtu mzima Gattuso hachezi yeye inakuwaje? Au ndo anacheza badala ya Gattusso?

Nimeifuatilia timu hii kwa muda sasa na ninachojaribu kukwambia ni kuwa Flamini nae hana namba ingawa mara kadhaa amekuwa anaingia kama sub.
Gattuso alivimba sana kichwa, acha ashikishwe adabu.
Kama timu inaweza kwenda el santiago bernabeu bila yeye na kupata ushindi ni wazi kuwa hana msaada kama yeye anaofikiria
 
Ili Gattuso apangwe basi ni wazi mmoja kati ya Boriello ana Pato anatakiwa akae benchi. Na hili haliwezekani kwa sababu wote hawa kwa sasa wako kwe fomu.
jamaa alikosea ktk mechi waliyofungwa 4 dhidi ya Inter kwani alipewa kadi nyekundu ya kizembe kisha akaenda kumfokea leonardo na kuvua jezi na kuitupa chini.
Kitendo hiki kilitafsiliwa tofauti na waandishi wa soka
 
Teh teh teh halafu mkuu gang chomba nahisi sasa watu watakuwa wamefahamu timu unayoishabikia.
Teh teh tutaanza kuifuatilia sasa ili tuwe tunakupa maneno machafu kama unayoyatoaga kwa wenzako
 
Ili Gattuso apangwe basi ni wazi mmoja kati ya Boriello ana Pato anatakiwa akae benchi. Na hili haliwezekani kwa sababu wote hawa kwa sasa wako kwe fomu.
jamaa alikosea ktk mechi waliyofungwa 4 dhidi ya Inter kwani alipewa kadi nyekundu ya kizembe kisha akaenda kumfokea leonardo na kuvua jezi na kuitupa chini.
Kitendo hiki kilitafsiliwa tofauti na waandishi wa soka

Na wakati ligi ilipokuwa inaanza milan walikuwa na matokeo mabaya kutokana na kumsimamisha mshambuliaji mmoja mbele.
Lakini toka alipoanza kusimamisha watu wawili timu imekuwa na matokeo mazuri mpk rrraha yani.
Pirlo ni mtu muhimu sana ktk kikosi hivyo hawezi kukaa nje, na pia mtu kama Clarence nae
Ni mtu hatari sana.
So mtu anayetakiwa akae nje kwa ajili ya Gattuso ni Massimo ama tunaomjua tunamwita Ambro ambaye ndiye Nahodha wetu na pia ana uwezo mkubwa wa kunyang'anya mipira pasipo rafu. Pia ambro ana kipaji cha kupiga mipira mirefu na kumdondokea mshambuliaji nae akafunga...
So Kaka Gattuso itakuwaje?
 
Nimeifuatilia timu hii kwa muda sasa na ninachojaribu kukwambia ni kuwa Flamini nae hana namba ingawa mara kadhaa amekuwa anaingia kama sub.

Maskini Flamini, anasubiri wazee wastaafu then aanze kucheza.
 
Maskini Flamini, anasubiri wazee wastaafu then aanze kucheza.

Kwa kwa kwaaaaa
Wakuzeheka ni nani?
Seeldorf?
Au Pirlo?
Yaani hawa hawazeheki.
Juzi seedorf kawajibu waandishi wa habari kuwa ni rahisi kwa waandishi kustaafu kuliko yeye kutundika daruga...so kama Flamini anasubiri atasubiri mpk kunakucha
 
Aliyepata kuwa dikteta wa kiungo barani europa kwa Miaka ya hivi karibuni Ivan Rhino Genarro Gatusso amefungua kinywa chake na kusema kuwa anataka kujua mustakabali wa kupata namba katika kikosi cha kwanza hapa Milan ama la basi atatimka klabuni hapa.
kauli hiyo imetolewa kwa masikitiko makubwa na kiungo huyo nguli mwenye amsha amsha za kutosha awapo dimbani kufuatia kitendo cha kocha Leonaldo kuendelea kutomtumia kamanda huyo aliyepata kuwa pia kipenzi cha washabiki wa rossonelli.
Hakuna taarifa rasmi zilizobainisha kuwa ni sababu gani haswa imepelekea Gattuso kuwa benchi kwa mechi nyingi.
Lakini kuna habari zisizo za uhakika sinadokeza kuwa kocha Leonardo ameamua kutokumtumia kiungo huyo kutokana na kitendo chake cha utovu wa nidhamu alichokionyesha ktk mechi ya wapinzani wa jadi maarufu kama dela madoninna kati ya Rosonelli na Nerazurri ambapo Milan walifungwa goli 4-0 nyumbani kwake na Inter.
Lakini pia duru za soka zinadokeza kuwa mfumo unaotumika sasa wa kuwasimamisha washambuliaji wawili mbele ndo kikwazo cha kupata namba kwa Rhino. Wachambuzi wa soka pia wametanabaisha kuwa tangu kocha Leo alipoanza kuutumia mfumo huu Milan imekuwa na mfululizo wa ushindi ama droo kitu ambacho ndio milan wanachokitaka kwa sasa.
Najihisi kama ni kiongozi muasi kwa jinsi ninavyofanyiwa hapa Milan...hakika naumia sana pale ninapoona mashuka makuubwa yaliyoandikwa maneno ya kunisifu na kunitukuza toka kwa washabiki wenye imani nami lakini nayasoma hayo nikiwa nimekaa benchi...alikaririwa Gattuso kwa uchungu.
Lakini kwa sisi tunaoijua Milan tunaona wazi kuwa Leonaldo atakutana na upinzani mkali toka kwa washabiki wa Milan kufuatia kitendo chake cha kumuweka benchi mshambuliaji anayeaminika kuwa ni hatari Suppa Pippo Fillipo Inzaghi.
Hakuna uthibitisho mpk sasa unaoonyesha ni lini ama ni wapi Pippo aliwahi kumpiga chenga, ama tobo, ama kisigino beki kisha akafunga, lakini inaaminika kuwa Pippo ndiye mshambuliaji hatari na mabeki huwa makini kwa kipindi chote awapo uwanjani.
Leonaldo ameonyesha imani kwa washambuliaji Alesandro Pato na marco Boriello na amekuwa akimtumia kwa nadra sana mshambuliaji huyo kipenzi cha watu wa milan aliyejiunga na klabu hiyo mwaka 2000 akitokea Bianconelli ama Juve.
Akiongelea matukio haya hivi karibuni makamo wa rais wa klabu hiyo muheshimiwa Adriano Galliani amesema kuwa mambo yote haya yanatokea ni kwa sababu tu ya swala zima la wakati...
Milan ilianzishwa tarehe 16/dec/1898 na tangu hapo imebeba kombe la ulaya mara 7 na ndio klabu iliyobeba vikombe vingi vya kimataifa kuliko klabu yoyote hapa ulimwenguni.
'SFORZA MILAN'.

Dah hili swala la Inzaghi hata mimi limeanza kunitia hofu.
Ila mmmmh mie chimo.
 
OFFICIAL NEWZ:
Makamo mwenyekiti wa AC Milan msema hovyo Adriano Galianni muda wowote atakuwa na kikao cha faragha na Gattuso.

Source: le gazzetto dello sport
 
Kwa kwa kwaaaaa
Wakuzeheka ni nani?
Seeldorf?
Au Pirlo?
Yaani hawa hawazeheki.
Juzi seedorf kawajibu waandishi wa habari kuwa ni rahisi kwa waandishi kustaafu kuliko yeye kutundika daruga...so kama Flamini anasubiri atasubiri mpk kunakucha
Flamini siku hizi anacheza beki wa kulia/kushoto na anaanzia bench
 
Flamini siku hizi anacheza beki wa kulia/kushoto na anaanzia bench

flamini kafulia vibaya mno.
We fikilia anacheza mtu kama Abate yeye amejikunyata tu nje.
ana wakati mgumu kwa kweli. Wale jamaa wana tradition zao ktk soka
 
Kocha wa Milan Leonardo kawatoa hofu wana Milan kwa kuwaambia kuwa kibaba chao kikiwa fit 100% atakipanga tu hivyo msihofu
 
Halafu huyo gatuso mwenyewe anayezungumziwa basi utafikiri labda ni fabregas ama gerald ama lampard. Kumbe zee limeshachoka.
 
Flamini siku hizi anacheza beki wa kulia/kushoto na anaanzia bench

Flamini jana kaanza dimba la chini kuchukua nafasi ya Pirlo aliepumzishwa...final result catania 0-2 milan.
Thanx to Hunter
 
Back
Top Bottom