Gari yangu asubuhi/ikiwa imepoa. Nikitoa gear kutoka R kwenda D/2/L inashtuka khu! Hii imekaaje?

Mlolongo

JF-Expert Member
Jul 4, 2019
3,271
5,892
Namiliki babywoka jamii ya IST, Swift, Honda Fit au Passo.

Asubuhi napowasha gari au mfano gari nimepaki mahali muda mrefu, nipokuja kuwasha gari si inakuaga P?
Okey, sasa nashika gear lever naweka Reverse kutoa parking/getini. Kisha nikipeleka D au L au 2 ili niondoke, gari inafanya kama kushituka hivi Khuu, then gia inaingia fresh naondoka zangu.

Sema nini, baada ya hapo (yaani gari ikiwa imechanganya) haishituki tena. Hii inatokea tu asubuhi napoiwasha, au nikiwa nimeipaki mahali muda mrefu (imepoa weeee) halafu nikaiwasha sasa nikataka kutoa R kwenda D.

Naomba nieleweke:
Asubuhi napowasha gari nikiweka Reverse nikapeleka Drive (D/2/L) gari inashtuka hivi. Lakin baada ya hapo (hata nikirudia tena mara ya pili) haishituki tena. Mpaka ipoe tena weeeee halafu nifanye tena kutoa R kwenda D/2/L ndio mshituko utatokea.

Hii itakua imekaaje mazee. Tatizo ni ile gear lever, gearbox, oil, fuel, engine au nini?

Babywoka yangu naipenda.
 
Shida ni moja kati ya haya mambo mawili.

1. Gearbox oil imechoka hivyo inakuwa na nzito kuflow(viscosity kubwa) ikiwa ya baridi.

2. Oil unayotumia siyo sahihi/incompatible kwa gearbox yako.

N.B. Oil huwa nzito kuflow ikiwa ya baridi na huwa nyepesi ikiwa ya moto.
 
Sasa bro mbona naporudia mara ya pili haishituki tena. Tatizo ni pale mwanzo tu gari inapotoka kupoa.
Acha uvivu mkuu,gari ikishatembea kuna kuongezeka kwa joto kwenye baadhi ya components hivyo inaweza kuwa ni sababu ikishatembea hiyo hali inapotea...
 
Shida ni moja kati ya haya mambo mawili.

1. Gearbox oil imechoka hivyo inakuwa na nzito kuflow(viscosity kubwa) ikiwa ya baridi.

2. Oil unayotumia siyo sahihi/incompatible kwa gearbox yako.

N.B. Oil huwa nzito kuflow ikiwa ya baridi na huwa nyepesi ikiwa ya moto.
Blaza Gearbox Oil unamaanisha ATF/Hydraulic?
 
Hi ndg nisaidie ushauri nina carina yangu 7A inasumbua kupanda mlima inachemsha. Nakkukosa nguvu hasa kwenye mlima
Pili hydraulic inaisha haraka yaan wiki 1 niliweka lita 4 leo iko low kabisa
.nikiweka d kuondoka gear inachelewa kuingia na kutoka na kuna sauti inatoka kama mshutuko then inaondoka hapo
 
Hi ndg nisaidie ushauri nina carina yangu 7A inasumbua kupanda mlima inachemsha. Nakkukosa nguvu hasa kwenye mlima
Pili hydraulic inaisha haraka yaan wiki 1 niliweka lita 4 leo iko low kabisa
.nikiweka d kuondoka gear inachelewa kuingia na kutoka na kuna sauti inatoka kama mshutuko then inaondoka hapo
Angalia hydraulic inavujia wapi
 
Back
Top Bottom