Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,813
- 4,547
Gari nne likiwemo lori la mafuta zimegongana na kusababisha ajali katika eneo la Mlandizi mkoani Pwani usiku wa kuamkia leo Julai 2, na kupelekea kifo cha mtu mmoja na majeruhi watatu, abiria wanaotokea Dar es Salaam wameshauriwa kutumia barabara ya Bagamoyo.
Akifafanua zaidi kuhusu tukio hili Kamanda Polisi mkoani Pwani, Bw. Wankyo Nyigesa amesema "Majeruhi wapo katika hospitali ya Tumbi pamoja na mwili wa marehemu lakini ninawashauri wasafiri wanaotokea Dar es Salaam watumie barabara ya Bagamoyo ili tuweze kuifungua hii barabara kwa sababu foleni ni kubwa sana" -
Akifafanua zaidi kuhusu tukio hili Kamanda Polisi mkoani Pwani, Bw. Wankyo Nyigesa amesema "Majeruhi wapo katika hospitali ya Tumbi pamoja na mwili wa marehemu lakini ninawashauri wasafiri wanaotokea Dar es Salaam watumie barabara ya Bagamoyo ili tuweze kuifungua hii barabara kwa sababu foleni ni kubwa sana" -