Gari la Nimrod Mkono lachezewa "foul" katika ya barabara

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,987
144,318
Mkono: Nina hofu na usalama wangu

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM) amesema maisha yake yako hatarini, kutokana na kuwepo genge la watu ambalo amedai wana nia mbaya na yeye, hivyo ameomba jeshi la Polisi kuchunguza watu hao.

Mkono, ambaye amelazimika kufungua jarida la malalamiko kwenye Kituo cha Polisi Kawe jijini Dar es Salaam, KW/RB/12156/2014, alisema tukio hilo limemwongozea hofu juu ya maisha yake, kutokana na kufuatiliwa nyendo zake na watu asiowajua.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Mkono alidai juzi saa 4 asubuhi akiwa na wasaidizi wake wawili wakitokea Bagamoyo, wakiwa ndani ya gari lake dogo aina ya Mercedes Benz, walipofika maeneo ya Mbezi Tangi Bovu, ghafla yalitokea magari aina ya Prado na Land Cruiser CX na kufunga njia.

Mkono alisema hali hiyo ilisababisha wasiendelee na safari yao na ndipo dereva wake alipoamua kulitoa gari na kulipitisha pembeni na kufanikiwa kutoka katika maeneo hayo.

Taarifa hiyo ya Mkono ilifafanua kuwa wakiwa bado wako njiani, yalitokea tena hayo magari mawili yakiwa mwendo wa kasi, yakiwafukuza na ndipo kijana mmoja akiwa amevaa miwani myeusi, ambaye alikuwa ndani ya gari aina ya Land Cruiser VX, alishusha kioo na kuwaamuru wasimamishe gari lao.

"Katika hali hiyo dereva wangu aliendesha gari kwa kasi hadi njia panda ambako tulimkuta askari wa doria akiwa pembezoni mwa barabara, tukamweleza na kuomba msaada wake.

Baada ya sisi kusimama mbele ya askari huyo magari hayo yalipita kwa kasi na kuelekea maeneo ya Mbezi Beach," ilisema taarifa hiyo ya Mkono.

Alisema yeye na wasaidizi wake, walipomweleza yule askari wa doria yaliyowatokea njiani, aliwashauri kuwa ni vyema wakaenda kutoa taarifa katika kituo cha polisi kilicho karibu na eneo la tukio kwa msaada zaidi.

"Kutokana na tukio hilo nilipata mshituko na kuwaomba wasaidizi wangu wanipeleke nyumbani kwangu Masaki kwa mapumziko," alidai Mkono.

Alisema alipofika nyumbani ndipo alimwagiza msaidizi wake aende kutoa taarifa katika kituo cha polisi cha Kawe, kama alivyoshauriwa na askari aliyekuwa doria na kufungua jalada hilo.

Hilo ni tukio la pili ndani ya siku za hivi karibuni, ambalo Mkono amejitokeza kwenye vyombo vya habari na kueleza maisha yake kuwa hatarini. Tukio la kwanza Mkono alidai kulishwa sumu wakati akiwa safari ya kikazi na wabunge wenzake nchini Uingereza.


Chanzo:Habarileo



MY TAKE:
Mh.Kafulila,mwenzako akinyolewa,wewe tia maji.
 
Mungu wa Israeli atakupigania Mbunge wangu! Atawasambalatisha hao maadui kutoka kwako kwa njia saba,Eee Mungu mlinde mjori wako aendelee kusimamia shughuli za maendeleo jimboni.
 
Mkono ni mpinzani typical anajali wapiga kula wake basi tu anaogopa maharamia wa CCM! Hao wanaomtafuta ni baadhi ya majambazi wa CCM.
 
Vijana wepi Ccm haina vijana wa kulikomboa taifa. Maana wao kaz yao ni kuiba na kutetea Mafisadi. Ona Nape, Lusinde, Komba nk. kaz taarabu na matusi ndiowanavyojua.
 
Mkono aache kutuyeyusha na hizo drama zake... he is no saint either!!
 
Hili halina cha Kafula wala nani. Tumeona Mwinyi alipigwa kibao, Wazioba amebondwa juzi juzi, kina Masele wamevamiwa n.k hiyo ndiyo Tanzania tunayojenga hata wewe unayefurahia leo au hata kuandaa ushezi wa namna hii kwa wengine au ku-support kwa namna yoyote vibaka hawa hawatakuacha, watatumiwa na mwingine dhidi yako. Leo kwangu kesho kwako. Ndiyo ajira yao hiyo. Tusipo jenga misingi ya kuheshimu sheria na wale wenye mamlaka kusimamia misingi kwa haki, tutachinjana sana tu.
 
Mimi nashangazwa na hizi tabia za hawa vigogo ,wanapofanya madili ya mabilioni hatuwasikii kuliakulia ili wapate kuhurumiwa na wananchi au kupata support ya wananchi,hula hizo pesa wao na ndugu zao na vimada vyao kimya kimya wakati sisi tunapata maumivu,linaposanuka hukimbilia kwa wananchi ili wapate huruma na waungwe mkono na hao hao wanaowaibia,hii tabia anayo sana mzee Mengi na sasa naiona kwa Mzee Mkono,hapana wananchi tukatae kutumiwa kama karatasi za chooni na kila mtu aubebe mzigo wake,kwenye raha ni wao ,kwenye shida ni sote,jamani tusiwe wajinga ,wacha wahukumiwe kwa matendo yao,ambayo wamefanya wao na sio sisi.
 
Mbunge wa Musoma vijijini,mh. Nimrod Mkono ameripotiwa kuingia matatani tena baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kutaka kufanyiwa hujuma huku likiwa barabarani na kusababisha mbunge huyo kuahirisha safari na kurudi alikotoka.

Kwa mujibu wa gazeti moja la leo(silikumbuki),wakati mh.Mkono akiwa anasafiri ndani ya gari lake,alijikuta ghafla akizingirwa na magari mawili akiwa barabarani jambo lilimfanya akatishe safari yake na kuamua kurudi alikotoka.

CHANZO:Magazeti kupitia Radio Free Africa.

MY TAKE:
Mh.Kafulila,mwenzako akinyolewa,wewe tia maji.

Kuna Picha moja ilirushwa mitandaoni watu watatu -Mkono ,Chenge na Werema na kama kawaida picha huzungumza maneno mengi-itafuteni ile picha ipegigwa nje ya Jengo la Bunge.
 
Alizungukwa na magari mawili!? then akageuza na kurudi alikotoka!? Chai hizi. Kama walitaka kummaliza, wasingeshindwa kufanya hivyo.

Huyu nae amezidi kulia kulia sana nowadays.
 
Hata kama ni promo tusizipuuze , kwa Serikali inayoongozwa na watu wang'oa kucha na meno bila ganzi haya siyo mambo ya kushangaa.
 

Kuna Picha moja ilirushwa mitandaoni watu watatu -Mkono ,Chenge na Werema na kama kawaida picha huzungumza maneno mengi-itafuteni ile picha ipegigwa nje ya Jengo la Bunge.

wadau walisema kuwa ile picha ya zamani walikua hawana bifu.
 
Hata kama ni promo tusizipuuze , kwa Serikali inayoongozwa na watu wang'oa kucha na meno bila ganzi haya siyo mambo ya kushangaa.

Kama yeye ni mbunge watu wanakufa na majambazi, ajali, magonjwa, watu wanalala giza kafanya nini??!!
Kujenga shule na kutoa pesa binafsi wakati nazo zinatoka shirika la umma haya ndio ya ku sympathize na viongozi??!!!

Yanatakiwa kupuuzwa saba mara sabini na wengine pia yawasibu ili wananchi wakilia wawe wanaelewa uchungu wa hali isiyo salama!!

Inafikia polisi wanauwawa kituoni na maharamia hawa viongozi wapo tu tena wabunge hawakuweka hata motion kubana wizara juu ya matukio kama hayo, sasa yakiwakuta wao ndio lugha itaeleweka kirahisi zaid!!

Wakiumwa wanaenda nje, mishahara mizuri, mikopo imenona sasa bila majanga hawaelewi real life ya Mtanzania!!!
 
Back
Top Bottom