Gari la Naibu Waziri lapatikana

Bubu Msemaovyo

JF-Expert Member
May 9, 2007
3,832
2,790
Kuna taarifa na picha ya gari hilo la rangi ya kijani likiwa limeegeshwa katika nyumba moja huko Tabata maeneo ya Jiandae. Taarifa zaidi hapo baadaye.
 
Bubu, garli limepatikana lakini leo nimesoma kwenye Majira ni masikini dereva wake amekutwa amechinjwa..... Soma:
http://majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=5485

Mungu ailaze roho ya marehemu pema na pole kwa familia, ndugu na jamaa.....

Maswali ya kujiuliza:
1. Serikali inanunua magari ya kifahari yenye kutamaniwa na kuibiwa, ni roho ngapi za madereva zipotee ndipo tugungue hili na kuanza kununa magari yasiyo tamaa kwa wezi??
2. Ni lini serikali itaanzisha utaratibu wa kulaza magari yake kwenye vituo maalumu kupunguza wizi/vifo/udokozi?
3. Dereva alifariki akiwa na gari ya umma, je hii ni kifo kazini au familia itapewa kifuta jasho kisha mchezo uishie hapo.... Hii nina maana kwenye swala zima la mafao ya kifo kazini (mwajiri), insurance (magari ya serikali ni insured??), na swala zima la kuisaidia fanmilia

Naomba kuwakilisha, narudia kutoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki wa Marehemu T Mbaga
 
Swala sio hata magari mkuu ni kazi kwa serikali kupambana na uhalifu. Serikali isiponunua hayo magari basi watu binafsi na pesa zao watachinjwa pia kwa sababu ya magari kutamaniwa na majambazi. Nadhani hao majambazi walikosea wangteka hilo gari wakati waziri akiwa ndani ili washughulike swala la uhalifu.

Nakumbuka mkuu wa nnchi alishawahi kusema anawafahamu majambazi na akawaambia waache. Juzi pia alipiga mkwara wa kumaliza majambazi. sisi tumechosha na hayo maneno tunataka vitendo sasa.


Nadhani magari ya serikali hayanaga insuarance mkuu kama sikosei.
 
Hapo bado haijaniingia kichwani, lengo la hao majambazi lilikuwa ni nini?. Maana gari wamelitelekeza, hivyo nawezas sema lengo lao halikuwa kuiba gari ila kumuondoa dereva au!!!
 
hapa kuna uwalakini?kwanini jamaa hawakuiba gari?kuna changa la macho na inaonesha wale wauaji walikuwa wanhitaji roho ya yule dereva.Je Dereva ana Siri gani??Je tunaweza kuambiwa?mie naanza kupata na wasiwasi wa TISS wanafanya nini?hivi tibaigana ana mawazo yapi??
 
Nami nimewaza kama wewe Gembe,iweje huyu jamaa atenganishwe kichwa chake na kiwiliwili,alafu mazingira aliyookotwa ni njia panda ili wapita njia wamwone watoe taarifa kituo cha polisi.
Hawa mabedui walipanga kabisa kumwondoa roho na ili wasifuatiliwe kwa karibu kabla ya kutimiza azima yao wakawa wametuma SMS kwa mamsapu ili ajue tu jamaa katumwa na mheshimiwa.Tibagaina tupe ripoti na hao wauaji watiwe nguvuni haraka.
 
Nami nimewaza kama wewe Gembe,iweje huyu jamaa atenganishwe kichwa chake na kiwiliwili,alafu mazingira aliyookotwa ni njia panda ili wapita njia wamwone watoe taarifa kituo cha polisi.
Hawa mabedui walipanga kabisa kumwondoa roho na ili wasifuatiliwe kwa karibu kabla ya kutimiza azima yao wakawa wametuma SMS kwa mamsapu ili ajue tu jamaa katumwa na mheshimiwa.Tibagaina tupe ripoti na hao wauaji watiwe nguvuni haraka.

Bila shaka tusubiri uchunguzi wa Polisi maana ni mapema mno kuharakisha kupata taarifa zao, ila nakumbuka gari hili lilitiwa dawa maalum kabla halijaondolewa pale tabata Kimanga na kukawa na alama za vidole nyingi tu ambapo Polisi wa IB walichukua picha kwa ajili ya kufanyia kazi. Nadhani pia kuna haja ya kutumia utaalamu wa DNA kupata wahusika halisi wa tukio hili.
 
Bila shaka tusubiri uchunguzi wa Polisi maana ni mapema mno kuharakisha kupata taarifa zao, ila nakumbuka gari hili lilitiwa dawa maalum kabla halijaondolewa pale tabata Kimanga na kukawa na alama za vidole nyingi tu ambapo Polisi wa IB walichukua picha kwa ajili ya kufanyia kazi. Nadhani pia kuna haja ya kutumia utaalamu wa DNA kupata wahusika halisi wa tukio hili.

duh tungojee basi bosi wao wote aje na kutuundia tume maalumu ya watu 20 kuchunguza hi issue...
 
1. Haya yawezekana ni mauaji ya kulipiza kisasi- yawezekana ni wivu wa mapenzi-- yaani marehemu alikuwa mkware na akawa anatanua na mke wa mtu.. ndo akafanyiziwa!

2. Naskia Wapare tena hakatizi binti mzuri machoni - hata awe ameolewa! Na akina dada/mama hawajui kusema hapana hata kama ana mzee!

Anyway- just speculations, tusubiri uchunguzi!
 
Inawezekana waliliteka hilo gari wakaenda kufanyia uhalifu..walipomaliza wakamuua dereva kupoteza ushahidi
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom