Jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro,inayashikilia magari matatu kwa ajili ya uchunguzi juu ya uhalali wa umiliki wake likiwamo la mfanyakazi wa benki ya CRDB tawi la Moshi Haika Mawalla .
Magari hayo ni T 140 DAE aina ya Hondq na T803 CBY aina ya Isuzu Pick Up ambayo kwa mujibu wa jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro,yalikuwa yamefichwa uwani nyumbani kwa mtu mmoja aliyetajwa kwa jina la Steven Makuri mkazi wa Marangu .
Gari jingine ni T991 DMS aina ya Toyota Vangurd mali ya mfanyakazi huyo wa benki ya CRDB ambayo ilikutwa imefichwa nyumbani kwa mwalimu wa Shule ya Msingi Kirareni,Deogratius Benito Mtui(30)mwalimu huyo ni mkazi wa Marangu Mshiri wilaya ya Moshi Vijijini.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro,Hamis Issah,watu watatu wanashikiliwa kutokana na tuhuma hizo ambao ni pamoja na mzee wa miaka 60,James Rudovick Kyara,mlinzi anayelinda kwa masister wa Ushirika wa Neema tawi la Marangu,Deogratius Benito mtui(30) na Christopher Obeid Kipuyo,fundi madishi na anatajwa kuwa ndiye dereva aliyekuwa akifanya kazi ya kuyaficha magari hayo.
Mzee Kyara anatajwa kuwa na uhusiano wa karibu na Mfanyabiashara Bosco Beda Kyara ambaye anakabiliwa na mashitaka mawili likiwamo la unyang'anyi wa kutumia silaha na kupatikana na mali inayoaminika kuwa ni ya wizi ambayo ni gari aina ya Nissan Patrol V8 mali ya Kampuni ya Nisk Capital Limited ya Kenya.
Mfanyabiashara huyo ambaye kwa sasa anasota katika gereza Kuu la Mkoa la Karanga na mwenzake,Gabriel Jerome Mombuli, ndiye mume wa Mfanyakazi huyo wa CRDB,Haika Mawalla na amekiri kuwa Gari hilo Toyota Vangurd ni mali yake halali na liliwahi kukamtwa tena na polisi wa Bomang'ombe lakini liliachiliwa.
"Hiyo Gari ni mali yangu halali,na ilishakamatwa na polisi wilaya ya Hai na kuachiliwa baada ya kujiridhisha kwamba ni mali yangu halali,Asante",amesema Haika kwa ufupi.
Habar yako haielewek af pia acha kufua jina la kampuni hcho kicha cha habari yako akiendan na ulichoandika kwann huyo mtuumiwa ucmtaje kwa majina ake had utaje CRDB?