Gambo ataka Halmashauri ya Jiji la Arusha ichunguzwe, anusa harufu ya upigaji wa mamilioni

Nyakijooga

Senior Member
Dec 9, 2018
121
202
Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo ameitaka Serikali ifanye uchunguzi wa kina dhidi ya Halmashauri ya Jiji la Arusha akidai limekithiri kwa ubadhirifu wa fedha za umma. Amedai imeghushi risiti za EFD kiasi cha Sh. 699 milioni, imemlipa mdhabuni kiasi cha Sh. 36.5 milioni bila kutoa huduma, vifaa vyenye thamani zaidi ya Sh. 123 milioni vilivyodaiwa kununuliwa havijafikishwa eneo la ujenzi.

“Halmashauri ya Jiji la Arusha changamoto kubwa ni ubadhirifu na usimamizi mbovu wa fedha za halmashauri, wanachukua hela hawajali sababu wanajua ngazi ya mkoa na wilaya hakuna cha kuwafanya. Ni vizuri Waziri wa TAMISEMI wakafanya utaratibu wa kuweka jicho la ziada kwenye jiji letu kuangalia matumizi fedha za umma,” amesema Gambo.
 
Tunakupongeza Mh kwa jitihada zako za kupinga ubadhirifu katika halmashauri ya Jiji la Arusha
Lakini nikuombe kwa heshima na taadhima,utukumbuke na Sisi wakazi wa Olerian Mwanama ,barabara ya lami imalizike kwa kuibana TARURA...Hii itapunguza ADHA kubwa ya usafiri inayotukabili wakazi wa Kata hii..Kiukweli TUNATESEKA Mh

La Pili,shirikiana na LATRA na Jeshi la POLICE Arusha Mjini ili kuruhusu Bajaj kupita njia hii...Kwa sasa kuna WAHUNI wameanzisha Serikali yao,wanazuia Bajaji na Magari mengine binafsi kutoa huduma ya Usafiri katika njia hii ya Kijenge- Mwanama- Engutoto

La Mwisho,tupiganie hii lami inayoishia ndani ya nyumba za matajiri PPF Kijenge iweze kuendelea hadi huku Mshono kupita Kituo cha Afya Moshono..Hii itasaidia sisi wapiga kura kufika kirahisi katika kituo hiki cha Afya Moshono kwa ajili ya kupata huduma.
 
Mbunge wa Arusha Mjini, Mrisho Gambo ameitaka Serikali ifanye uchunguzi wa kina dhidi ya Halmashauri ya Jiji la Arusha akidai limekithiri kwa ubadhirifu wa fedha za umma. Amedai imeghushi risiti za EFD kiasi cha Sh. 699 milioni, imemlipa mdhabuni kiasi cha Sh. 36.5 milioni bila kutoa huduma, vifaa vyenye thamani zaidi ya Sh. 123 milioni vilivyodaiwa kununuliwa havijafikishwa eneo la ujenzi.

“Halmashauri ya Jiji la Arusha changamoto kubwa ni ubadhirifu na usimamizi mbovu wa fedha za halmashauri, wanachukua hela hawajali sababu wanajua ngazi ya mkoa na wilaya hakuna cha kuwafanya. Ni vizuri Waziri wa TAMISEMI wakafanya utaratibu wa kuweka jicho la ziada kwenye jiji letu kuangalia matumizi fedha za umma,” amesema Gambo.

Sio Arusha tu, ni kwamba yeye kawa makini na ni mnoko
 
Back
Top Bottom